MSD watoa tenda ya kusambaza dawa nchini kwa viwanda vya China na India miaka miwili mfululizo

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,767
36,625
Huku serikali ikitenga bilioni mia moja kwaajili ya kuviboresha viwanda vyake vya ndani, viwanda vya kuzalisha dawa za binadamu vilivyopo nchini havitafanya kazi na serikali katika kipindi cha miaka miwili ijayo, imefahamika.

Bohari kuu ya dawa nchini MSD imeingia ubia na viwanda vya China pamoja na India ili visambaze dawa za binadamu nchini kupitia Bohari hiyo kwa asilimia mia moja miaka miwili mfululizo kuanzia mwaka ujao wa serikali unaoanza mwezi wa tano. Hiyo ni kwa mujibu wa tenda iliyofanyika hivi karibuni ambapo viwanda vya ndani havikutakiwa kushiriki.

Kwa maana hiyo sioni haja ya serikali kujikwamua hadi kuwaza kuviboresha viwanda vyake huku ikishindwa kuvitumia ili vijiendeshe.
 
Sasa mkuu ulitaka waache 10%, viwanda vya ndani vikauze nchi za jirani kama Burundi na Rwanda, watu wanataka kula kwanza uzalendo baadaye
 
Dawa za India na China hazina ubora mzuri sana, Acheni siasa katika mambo ya msingi. Ciprofloxacin ya Ujerumani ni nzuri mno kuliko ya India
 
Tena?! sasa hiyo Tanzania ya viwanda itakuwaje kama tunafanya haya? Halafu dawa za INDIA! nahuku ni kucheza na afya za watanzania au kuna mpango wa kupunguza watu kwa style fulani? Kweli sio serikali ya viwanda bali ni serikali kwa msaada wa watu wa china.
 
Back
Top Bottom