Msajili wa Vyama vya siasa Nchini Francis Mutungi amekiomba chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA kutoa majibu kuhusiana na madai ya Samson Mwigamba aliyefukuzwa uenyekiti wa chama Arusha.
Akizungumza ofisini kwake Kaimu Katibu Mkuu CHADEMA Victor Kimesera amesema alipokea barua kutoka kwa Msajili akikiomba chama hicho kutoa ufafanuzi kuhusu malalamiko ya Mwigamba kwamba Katiba ya chama hicho si sahihi hususan suala la Ukomo wa Uongozi.
Kiongozi huyo alisema tayari chama hicho kimemsaidia Msajili kutoa ufafanuzi na vielelezo vyote alivyoomba.
Itakumbukwa kwamba CHADEMA kupitia Kamati Kuu mwezi uliopita kiliwafukuza nyadhifa zote za uongozi Zitto Kabwe,Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba kwa usaliti na kuhujumu chama.Huku hatima ya uanachama wao ikiwa mikononi mwa Kamati Kuu.
Source: Nipashe.
Akizungumza ofisini kwake Kaimu Katibu Mkuu CHADEMA Victor Kimesera amesema alipokea barua kutoka kwa Msajili akikiomba chama hicho kutoa ufafanuzi kuhusu malalamiko ya Mwigamba kwamba Katiba ya chama hicho si sahihi hususan suala la Ukomo wa Uongozi.
Kiongozi huyo alisema tayari chama hicho kimemsaidia Msajili kutoa ufafanuzi na vielelezo vyote alivyoomba.
Itakumbukwa kwamba CHADEMA kupitia Kamati Kuu mwezi uliopita kiliwafukuza nyadhifa zote za uongozi Zitto Kabwe,Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba kwa usaliti na kuhujumu chama.Huku hatima ya uanachama wao ikiwa mikononi mwa Kamati Kuu.
Source: Nipashe.