Elections 2010 Msafara Wa Mamba

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Miaka 15 ya mfumo wa vyama vingi Tanzania. Mengi tumeyaona, lakini yaliyotokea juzi na jana kule Dodoma yamenipa funzo kubwa kwamba upinzani Tanzania umejaa waganga njaa na wanafiki wanaoweza kuonesha usaliti wao mchana kweupe.

Nilistuka sana niliposikia kuwa kumeundwa kitu kinachoitwa 'minority opposition'. Hata wakati wa upigaji kura matokeo yalionesha pasipo na shaka kuwa siyo CCM peke yake wanaokichukia Chadema, bali hata vyama vingine vya upinzani.

Hivi kosa la Chadema ni nini? Mbona silioni?

Au kwa kuwa safari hii kimevuna wabunge hata kusiko kuwa na Wachaga?

Kwamba wazazi wangu CCM damu amekipigia kura Chadema(na wameapa hawatapigia kura CCM tena)?

Kwamba kwa nini Chadema kimeanza kupigiwa kura hata na wasukuma badala ya kupigiwa kura na wachaga kama ilivyokuwa zamani?

Kwamba Chadema kimewaamsha Watanzania kwa kuwaondolea fikra pandikizi za CCM?

Kwamba Chadema kimesheheni(na kitaendeleakusheheni) wanachama na wafuasi wasomi wa vyuo vikuu?

Kuna maswali mengi ninayojiuliza kuhusu chuki kwa chama hiki makini.

Somo moja nililopata baa da ya harakati za jana na juzi:

Vyama vya upinzani Tanzania havina tofauti na Msafara wa mamba ambamo Kenge na Mijusi huwa hawakosi.

Viva Chadema. Stand on Your Feet.

Tuko Nyuma Yenu.

Change is Inevitable. It's just a matter of time.
 
Miaka 15 ya mfumo wa vyama vingi Tanzania. Mengi tumeyaona, lakini yaliyotokea juzi na jana kule Dodoma yamenipa funzo kubwa kwamba upinzani Tanzania umejaa waganga njaa na wanafiki wanaoweza kuonesha usaliti wao mchana kweupe.

Nilistuka sana niliposikia kuwa kumeundwa kitu kinachoitwa 'minority opposition'. Hata wakati wa upigaji kura matokeo yalionesha pasipo na shaka kuwa siyo CCM peke yake wanaokichukia Chadema, bali hata vyama vingine vya upinzani.

Hivi kosa la Chadema ni nini? Mbona silioni?

Au kwa kuwa safari hii kimevuna wabunge hata kusiko kuwa na Wachaga?

Kwamba wazazi wangu CCM damu amekipigia kura Chadema(na wameapa hawatapigia kura CCM tena)?

Kwamba kwa nini Chadema kimeanza kupigiwa kura hata na wasukuma badala ya kupigiwa kura na wachaga kama ilivyokuwa zamani?

Kwamba Chadema kimewaamsha Watanzania kwa kuwaondolea fikra pandikizi za CCM?

Kwamba Chadema kimesheheni(na kitaendeleakusheheni) wanachama na wafuasi wasomi wa vyuo vikuu?

Kuna maswali mengi ninayojiuliza kuhusu chuki kwa chama hiki makini.

Somo moja nililopata baa da ya harakati za jana na juzi:

Vyama vya upinzani Tanzania havina tofauti na Msafara wa mamba ambamo Kenge na Mijusi huwa hawakosi.

Viva Chadema. Stand on Your Feet.

Tuko Nyuma Yenu.

Change is Inevitable. It's just a matter of time.


Mkuu mtu akionesha juhudi za kweli kukunyang'anya ulichonacho mkononi wakati unakitaka hakika utamzulia mengi, ndicho kinachotokea.
 
Back
Top Bottom