Msaada wenu wa kimawazo kwenye hili

Msaada wenu wa kimawazo kwenye hili

Kibajaji01

Member
Joined
Sep 22, 2023
Posts
15
Reaction score
39
Wakuu naombeni msaada wenu wa kimawazo kwenye hili.

Mimi ni mwalimu wa physics na chemistry ila sijabahatika kupata ajira serikalini, sasa kuna shule mbili nafundisha let say shule X na shule Y. Shule X nalipwa laki tatu, wakati shule Y nalipwa 250,000/=

Shida inapokuja shule Y wanao nilipa 250 wao hawana shida walinambia sababu ya hela wanayonipa ni ndogo basi niwe naenda muda wa vipindi tu kufundisha na kuondoka, ila hawa shule X wanaonipa 300 wao hawataki nifundishe shule nyingine tofauti na wao, yaani niwepo kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi, Jumatatu hadi Ijumaa tunatoka saa 11 isipokua Jumamosi tu ndio tunatoka saa nane mchana.

Sasa wiki hii shule X wameniita na kuniambia nichague shule moja nitakayo fanya kazi. Naombeni ushauri wakuu, nibaki na hii ya 250 niwe naenda muda wa vipindi tu ambapo ni siku tatu kwa wiki au niendelee na shule X ya 300?
 
Nenda ambako pesa unaipata kwa uhakika,
Pesa hata kama ni laki ikiwa unaipata kwa wakati angalau you can survive
 
Sehemu wanayolipa kwa uhakika ndio pa kwenda

Watu tuli survive kwa malipo ya 70 ila tu iwe uhakika siku fulani inaingia una clear vimeo kwa ukamilifu
 
Kaka nenda sehemu ambayo wanalipa kwa uhakaika na kwa wakat kama hapo y wanalipa kwa uhakaika n vzur zaid
 
Nenda kwenye 250k, mana utakuwa free na kufanya ishu zingine baada na kabla ya kwenda kufundisha.

Ila kwanza ongea na hiyo shule nyngn khs malipo waongeze mpaka 500k Ili ubaki kama wanavyotaka, wakikataa bc Achana nao na uende kwenye 250k
 
Nenda ambako pesa unaipata kwa uhakika,
Pesa hata kama ni laki ikiwa unaipata kwa wakati angalau you can survive

Sehemu wanayolipa kwa uhakika ndio pa kwenda

Watu tuli survive kwa malipo ya 70 ila tu iwe uhakika siku fulani inaingia una clear vimeo kwa ukamilifu

Kaka nenda sehemu ambayo wanalipa kwa uhakaika na kwa wakat kama hapo y wanalipa kwa uhakaika n vzur zaid
Kuhusu muda wa kulipa wote ni tarehe 30 ya mwezi
 
Wakuu naombeni msaada wenu wa kimawazo kwenye hili.

Mimi ni mwalimu wa physics na chemistry ila sijabahatika kupata ajira serikalini, sasa kuna shule mbili nafundisha let say shule X na shule Y. Shule X nalipwa laki tatu, wakati shule Y nalipwa 250,000/=

Shida inapokuja shule Y wanao nilipa 250 wao hawana shida walinambia sababu ya hela wanayonipa ni ndogo basi niwe naenda muda wa vipindi tu kufundisha na kuondoka, ila hawa shule X wanaonipa 300 wao hawataki nifundishe shule nyingine tofauti na wao, yaani niwepo kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi, Jumatatu hadi Ijumaa tunatoka saa 11 isipokua Jumamosi tu ndio tunatoka saa nane mchana.

Sasa wiki hii shule X wameniita na kuniambia nichague shule moja nitakayo fanya kazi. Naombeni ushauri wakuu, nibaki na hii ya 250 niwe naenda muda wa vipindi tu ambapo ni siku tatu kwa wiki au niendelee na shule X ya 300?
Watanzania hatujui thamani ya maisha. Fanya hivi, piga hesabu masaa unayokua kazini kwa siku unazokua kazini kwa mwezi mzima, igawe pesa unayopata kwa namba ya masaa unayofanya kazi. Ukipata jibu utaona hiyo 50k haina thamani yakukushurutisha kwa hayo masaa yanayoongezeka zaidi ya mar
A mbili.

Jali muda wako.
 
Pole mkuu..... kama ingewekezakana, baki hapo kwa 250k, then uwe huru kufanya mambo yako,,,hata tuition centre, ama shughuli nyingine ya kiuchumi !

Mambo on ground magumu mno yan, ebu cheki hiyo salary unaishi mjini umepanga, pengine una famila n.k ngumu sana kutoboa .

Alafu kuna washenzi wanaiba ma_B kadhaa huko wanaambiwa watajwe hadharani waone aibu !
 
We dogo, hacha upumbavu yaani si Bora ukafundishe tuition KUJIAJILI hayo masomo ni dili nenda pale mbuji
 
Back
Top Bottom