Msaada wenu unahitajika ili kulinda ndoa yangu

Msaada wenu unahitajika ili kulinda ndoa yangu

Hazchem plate

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2011
Posts
11,059
Reaction score
15,530
Habari wana jamvi. Mm nimeoa mke mwaka mmoja sasa. Nilimuoa binti wa Kikristo baada ya kuridhiana nae ikabidi abadili dini na kuwa muislam. Sasa Tatizo ninalo lipata ni kuwa nimegundua huyu binti anakula KITIMOTO. sasa suala hili limeniuma sana. Siku hizi nashindwa hata kula Romance wakuu nimekuwa sina amani na ndoa hasa ukizingatia mimi ni Muislam wa dhati kabisa
Naombeni mchango wenu wakuu kabla sijamface mke wangu. Ila ushahidi ninao kabisa na sio mara moja anakula na marafiki zake.
Wasalamu.
 
Habari wana jamvi. Mm nimeoa mke mwaka mmoja sasa. Nilimuoa binti wa Kikristo baada ya kuridhiana nae ikabidi abadili dini na kuwa muislam. Sasa Tatizo ninalo lipata ni kuwa nimegundua huyu binti anakula KITIMOTO. sasa suala hili limeniuma sana. Siku hizi nashindwa hata kula Romance wakuu nimekuwa sina amani na ndoa hasa ukizingatia mimi ni Muislam wa dhati kabisa
Naombeni mchango wenu wakuu kabla sijamface mke wangu. Ila ushahidi ninao kabisa na sio mara moja anakula na marafiki zake.
Wasalamu.
😕 MIMI SILI HAYO MAKITU ILA DENDA ZA MLA HAYO MAKITU NAZIMEZA BALAA.................
 
Baada ya kumsilimish ulitakiwa
Usimuache baada ya hapo, ungempa vitabu vya Dini, unge mfundisha Dini vizuri, ikiwa wewe hujui ungemtafutia Mwalimu japo umlipe aweze kumfundisha Uislam.

Makosa makubwa yanafanywa sana na Waislam, ni kuwa baada ya kumsilimisha mtu humwacha akaenda zake na hawamfuatilizii wala hawamsaidii kumfundisha Dini wala kujua kama anaswali, anafunga n.k. Jaribu kumsaidia kwa hali na mali kadiri uwezavyo .

Pia makosa makubwa yanatokea kwa kuwa wale wanaowasilimisha watu au kusababisha wasilimu, wao wenyewe hawatekelezi mafundisho ya Dini, hawaswali, hawana tabia njema za Kiislam na hata hawaijui Dini yao wenyewe. Jambo hilo huja kuwachanganya sana wanaosilimu, kwani wanakuta Uislamu unasema vingine na Waislamu wanafanya vingine!

Na ikiwa ni mtu ambaye hufuati mafunzo ya dini yako kamili, basi hukuchelewa sana, nakusihi, uanze kutekeleza na kujifunza kwa kusoma au kuhudhuria madarsa na mihadhara ya Dini n.k. kwani usipofanya hivyo ujue kuwa mkeo huyo uliyemsilimisha amesilimu jina tu lakini kivitendo hatopata mafunzo na mifano kutoka kwako atabaki kama alivyokuwa katika ukristo wake kwani anakutegemea sana wewe khaswa kwa kupata mafunzo ya dini .
 
huu unafiki wa kiislamu sijui utaisha lini, mkiwa chemba mnakula sana ila mbele ya alaiki wanajifanya wakali.njoo zenji hapa uone inavyoliwa na hao mashekhe wenu
Unafiki upo katika dini zote zile.... kwa sababu ya unafiki wako, huwezi kuhalalisha kilichoharamishwa. Mbona watu wana zini? waislam na wakiristo wanazini... je tusihoji zinaa kisa watu wanafanya ama?
 
Umenikumbusha shosti angu Fatuma lol akiwa njiani kuja home ananiambia kabisaaa shosti nikukute maeneo nna hamu nayo balaa,.

Pole mkuu,onàna na viongozi wa dini na wazazi kwa ushauri zaidi.
 
huu unafiki wa kiislamu sijui utaisha lini, mkiwa chemba mnakula sana ila mbele ya alaiki wanajifanya wakali.njoo zenji hapa uone inavyoliwa na hao mashekhe wenu
Kwani baadhi ya wakristo wanavyofanya uzinifu Ovyoo ndivyo uzinifuu usikemewe kuna baadhi ya waislam wanakula nguruwe kwa kificho na wengine waziwazi lakini haiondoshi maana ukweli utabaki palepale nguruwe ni haramu kwa mujibu wa dini. Lazima huyo mke akemewe
 
Habari wana jamvi. Mm nimeoa mke mwaka mmoja sasa. Nilimuoa binti wa Kikristo baada ya kuridhiana nae ikabidi abadili dini na kuwa muislam. Sasa Tatizo ninalo lipata ni kuwa nimegundua huyu binti anakula KITIMOTO. sasa suala hili limeniuma sana. Siku hizi nashindwa hata kula Romance wakuu nimekuwa sina amani na ndoa hasa ukizingatia mimi ni Muislam wa dhati kabisa
Naombeni mchango wenu wakuu kabla sijamface mke wangu. Ila ushahidi ninao kabisa na sio mara moja anakula na marafiki zake.
Wasalamu.
Mkuu huyo ni mke wako wa ndoa una chelea nini kumwambia? ushahidi unao vigezo unavyo tatizo nini? muite mweleze ajue kama sio sawa na muombe sana mwenyezi mungu akunusuru kila jambo unaogopa kula Romance lakini kwengine unakula mbona sielewi au haviusiani mkuu?
 
Yaani bado hujaongea nae na kumsikiliza ana sababu gani ya kula mdudu, unakuja kutuomba ushauri?

Ongea naye kwanza mkeo shekhe! then ulete mrejesho anatatizo gani?
 
Mmh! Haya mambo ya dini kwenye ndoa huwa ni magumu sana kwakweli!! Huenda alibadili dini kwakuwa anakupenda asikukose.lakini je mlikubaliana Vipi?...lakini nawewe unamchunguzaje mkeo kama anakula kmoto or not huo ni mwanzo wa migogoro ..kifupi huyo hajakubaliana na baadhi ya masharti ya kiislamu ,jaribu kuongea naye kwa upole mtaelewana tu!
 
Mwambie awe anapiga mswaki vizuri baada ya kula, hapo denda itapendeza
 
Kwani baadhi ya wakristo wanavyofanya uzinifu Ovyoo ndivyo uzinifuu usikemewe kuna baadhi ya waislam wanakula nguruwe kwa kificho na wengine waziwazi lakini haiondoshi maana ukweli utabaki palepale nguruwe ni haramu kwa mujibu wa dini. Lazima huyo mke akemewe
unayajua maandiko au umekariri haramu tu? si mwislamu au mkristo nguruwe si haramu soma maandiko usifuatemkumbo
 
Kitimoto tamu jaman asiwambie mtu halafu pawe na balimi au kilimanjaro pembeni, ongeza na chachandu daaah,
 
Tatizo mlikubaliana abadilishe dini kwa ajili ya ndoa.
Ulidhani siku moja inaweza ikambadilisha mtu imani yake ya maisha yake yote kabla?
Huyo bado si muislam.
Ni kama mmemuandikisha tu.
Tujaribu kuwa realistic ili tusitarajie kisichowezekana.
 
Back
Top Bottom