kijana mkimya
Pengine una allergy. Onana na daktari wa ngozi (dermatologist).
Kama ni shuka, itakuwa sabuni ina manukato fulani ambayo ambayo huifanya ngozi yako kuwasha. Pia, kutakuwa na vumbi ambalo linaifanya ngozi yako kuwasha. Au kuna chakula ambacho damu yako haipatani nacho.
Unaweza ukapima damu au skin test kujua kitu gani kinakufanya ujiwashe washe.
Kuna Kliniki ya Mashia wa Ithnashree karibu na msikiti wao , Mtaa wa India na Morogoro Road. Wanapima Damu kujua "allergy triggers" pale.
Pia, wanaweza kujua allergy kwa kupima katika ngozi yako. Wanaweka "allergen" ndani ya ngozi yako halafu wanaangalia kama itakuwasha. Watajua kama pollen au chakula fulani kinakudhuru.
Kumbuka, wakati mwingine ukiwa na allergy, haina dawa. Hasa, kama inatokana na kula chakula fulani au ipo katika hewa "pollen". Ila unaweza kupewa dawa (cream au vidonge) kupunguza uwasho.
Kwa Kiingereza, vipimo utakavyohitaji ni hivi:
Allergy blood test (immunoassay tests)
1. Enzyme-linked immunosorbent assay (ELISA)
2. Radioallergosorbent test (RAST)
Na
3. Skin test (intradermal test)