msaada wana jf

msaada wana jf

Sidhani kama hili jamabo linaweza sababisha kuvunja ndoa yako iliyodumu miaka saba!

Pengine hapo ndio mwanzo wa ndoa yenu inabidi huwe mvumilivu usifikiri wengine hayawakuti hayo kwenye ndoa zao labda kwa sababu hawapati wasaa wa kuandika kama wewe!

Calm down na uongee na mumeo vizuri pengine anayo kueleza ni ukweli na huo sio ushahidi mzuri wa kuvunja ndoa!
 
Pole dada lakini sidhani kama ni sahihi kwa wewe kufikiria kuacha ndoa kisa sms. Miaka saba inakutosha kuielewa vema taasis hii. Please sali sana na jifunze kujichunguza na kuchunguza mahusiano yenu wewe na mumeoi kama yana mapungufu rekebisheni.

Hilo tendo la ndoa unalopewa kama dozi ya Panadol, inakuwaje? kwani wewe wasubiria akugaie tu? Siku nyingine usisubirie dada yangu!
 
ndugu mtoa mada kwanza kabisa makosa uliyoyaleta hapa hayatoshi kukufanya uachane ama utengane na mumeo. kimsingi kabisa hapa hakuna kosa ila naweza kusema ulitaka tu kujua wengine tunalichukuliaje.

Ukweli ni kwamba huyo mdada kumwita mumeo mpenzi inawezekana ni mpenzi wake kweli ama sio nasema sio kwani kuna watu ambao wanahualka ya kuwa na maneno ama majina matamu kwa watu wengine. mfano mimi binafsi huwa ninatabia ya kumwita mtu kaka yangu wa moyoni ama dearest ama mpendwa wangu ama mpenzi lakini kamwe hunikuti namwita mtu dear wangu hili liko served for huzzy. sasa wewe huyu kumwita mumeo mpenzi yaweza kuanguka kwenye hayo makundi mawili.

sikatai kama ni mpenzi wa kweli inaumiza sana lkn mpaka sasa bado huna proof so bado ni suspicious tu ambazo zaweza kuwa kweliama uongo.

istoshe swala la uroda kutolewa mara mbili kwa mwezi basi kosa ni lako mwenyewe. labda nikuulize wajua kuitafuta network wewe kama haipatikani?? je umeshajaribu kuona unahitaj king'amuzi gani kwa signal zilizoko?? mwenzio pengine signal zilizoko ni short wave wakati yeye anataka long wave inakuwaje??

ulishakaa nae chini mkaelezana juu ya hali halisi?? ulishajaribu silaha zako zote za maangamizi za kike ukashindwa?? kumbuka silaha za maangamizi za kike zina nguvu inayoweza kumfanya hata jitu kama samsoni akawa kama mwana mpotevu, tena zina nguvu kuliko upanga as zinaweza kubadili ulimwengu kwa sekunde.

hivyo kama huji kuzitumia njoo uombe ushauri utapatiwa ila mwanamke kukosa kupewa uroda kabla ya kulalamika pima silaha zako za maangamizi kwanza.

Zifafanue silaha za maangamizi kinaga ubaga apate somo ati , maana umeishia kati kati


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
jichekeage tu best maana naona lugha gongana inataka kuzua ya kuzua....je, angekuta mumewe anaandaliwa chai huko ofisini, si angezirai kwa breini konkasheni ya digriii tatu!!!

Ha,ha,ha....USITUKUMBUSHE YA KANUMBA,

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
pole sana mdada hayo ni majaribu yabidi kuyashinda.
 
Haha haaaaaaa Asnam .. Kwa R.B kila siku kunawaka lolz daaaa..

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

yeye ameona ana matatizo kumbe yake madogo kuliko ya R.B siunajua mtu akikueleza yanayomsibu ndo unaona kumbe afadhali yako.Ndo maana nimeomba amfuate huyo apate experiance ili afanye maamuzi.
 
Nipo kwenye ndoa kwa muda wa miaka saba, lakini naona nataka kuyashindwa haya maisha ya ndoa, maana nimekuta msg kwenye simu ya mume wangu ameandikiwa na dada mmoja nanukuu'' mpenzi samahani kwa kukucheleweshea...'' Nilipomuuliza mume wangu akaniambia eti ofisini kwao kuna huyo mdada anamwita kila mtu mpenzi. Pia hata tendo la ndoa uwa anatoa mara mkama mara tatu kwa mwezi.

Sasa wewe kwenye simmu ya mumeo ulikua unatafuta nini au unatafuta ugonjwa wa moyo?
 
Makubwa,,,, madogo yana nafuuu. Fanya hivi: MPENDE ZAIDI ajishangae...Atarudi tuuu...ila usishike tena simu yake....
 
Pengine alimkopa mumeo hela akachelewa kurudisha, deal na mumeo hakikisha unamtimizia yoteee yatakayomfanya asitamani vya nje. Pika vizuri...usafi kwa sana..ubunifu 6x6..sio uone umekaa miaka 7 uanze mazoea! Uwe mpya kila siku 🙂
 
Ha,ha,ha....USITUKUMBUSHE YA KANUMBA,

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Halafu mpenzi nilikua nakutafuta sana...kesho kama utakuja mjini naomba tuonane, please!!!
 
Back
Top Bottom