Mhanga Mkuu
Member
- Oct 21, 2020
- 11
- 5
Habari za muda huu, na poleni na harakati za kimaisha.
Nikiwa na imani na members wa jukwaa hili, nina imani kubwa nitapata mchango wa mawazo ya biashara kulingana na maeneo niliyopo na vitangulizi nilivyo navyo. Kwa uzoefu wenu, naomba nisaidiwe wazo la biashara niweze kujikwamua kiuchumi.
MAHALI NILIPO: Dar es salaam
MTAJI: Laki Tisa. Pia nina vifaa vifiatavyo; Camera Canon 7D, Printer Epson L382, Laptop na Vifaa baadhi vya saluni ya kiume, kama kiti, vioo na mashine.
Kwasasa sina kazi, nategemea madili ya kupiga picha na kuuza vitabu vya masomo ya sekondari ya fizikia na kemia, ambavyo nimekua niki viandaa na kuvi print mwenyewe. Shughuli zote hizi zimekua hazinipatii kipato cha kukizi mahitaji yangu walau ya chakula na malazi.
Kabla nimewahi kufanya biashara ya saloon ya kiume, mara mbili kwa nyakati tofauti na sehemu tofauti tofauti, ambapo ilikumbwa na changamoto mbali mbali na kushindwa kuendelea kutokana na mapato yake kutotosha walau kulipia pango ya flem. Nilijaribu kufanya biashara ya fedha za mitandao (mpesa, tigo pesa na airtel money) nazo niliishia kuuza laini baada ya kushindwa kufikia malengo ya kibiashara kwa kukosekana mzunguko wa wateja.
Nimekuja kwenu mnisaidie wazo la biashara kulingana na mtaji nilio nao na vifaa hivyo. Nimejaribu kupitia mawazo mbali mbali yaliyo kwisha kutolewa, ingawaje nimeona mawazo ambayo yatakua specific na hali yangu yatakua bora zaidi.
Nje ya mada, elimu yangu ni Shahada ya ualimu wa masomo ya sayansi, fizikia na kemia. Hivyo kama nitapata connection huku nitashukuru pia.
Mwanzo nilikua na mtaji wa around 2.5M, lakini kutokana na kila biashara ninayo ianzisha kushindwa kufanikiwa mimejikuta natumia pesa bila faida na kubakiwa na hii 900k tu. Nimekuja kwenu kabla hali haijawa mbaya zaidi ili niweze kupata wazo lenye tija kutoka kwa wazoefu, maana nahisi huenda nakosea mahali.
Natangulisha Shukrani.
======
Kwa maoni zaidi soma>>>Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?
Nikiwa na imani na members wa jukwaa hili, nina imani kubwa nitapata mchango wa mawazo ya biashara kulingana na maeneo niliyopo na vitangulizi nilivyo navyo. Kwa uzoefu wenu, naomba nisaidiwe wazo la biashara niweze kujikwamua kiuchumi.
MAHALI NILIPO: Dar es salaam
MTAJI: Laki Tisa. Pia nina vifaa vifiatavyo; Camera Canon 7D, Printer Epson L382, Laptop na Vifaa baadhi vya saluni ya kiume, kama kiti, vioo na mashine.
Kwasasa sina kazi, nategemea madili ya kupiga picha na kuuza vitabu vya masomo ya sekondari ya fizikia na kemia, ambavyo nimekua niki viandaa na kuvi print mwenyewe. Shughuli zote hizi zimekua hazinipatii kipato cha kukizi mahitaji yangu walau ya chakula na malazi.
Kabla nimewahi kufanya biashara ya saloon ya kiume, mara mbili kwa nyakati tofauti na sehemu tofauti tofauti, ambapo ilikumbwa na changamoto mbali mbali na kushindwa kuendelea kutokana na mapato yake kutotosha walau kulipia pango ya flem. Nilijaribu kufanya biashara ya fedha za mitandao (mpesa, tigo pesa na airtel money) nazo niliishia kuuza laini baada ya kushindwa kufikia malengo ya kibiashara kwa kukosekana mzunguko wa wateja.
Nimekuja kwenu mnisaidie wazo la biashara kulingana na mtaji nilio nao na vifaa hivyo. Nimejaribu kupitia mawazo mbali mbali yaliyo kwisha kutolewa, ingawaje nimeona mawazo ambayo yatakua specific na hali yangu yatakua bora zaidi.
Nje ya mada, elimu yangu ni Shahada ya ualimu wa masomo ya sayansi, fizikia na kemia. Hivyo kama nitapata connection huku nitashukuru pia.
Mwanzo nilikua na mtaji wa around 2.5M, lakini kutokana na kila biashara ninayo ianzisha kushindwa kufanikiwa mimejikuta natumia pesa bila faida na kubakiwa na hii 900k tu. Nimekuja kwenu kabla hali haijawa mbaya zaidi ili niweze kupata wazo lenye tija kutoka kwa wazoefu, maana nahisi huenda nakosea mahali.
Natangulisha Shukrani.
======
Kwa maoni zaidi soma>>>Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?