Msaada wa ushauri kuhusu solar Power

Msaada wa ushauri kuhusu solar Power

Mtaalam nisaidie hili. Nina Sola 60Wt betri N50 haijaisha maji ipo full lakini jua likizima tu basi Inveter nayo haipeleki moto, likiwa tu inafanya kazi kama kawaida hata nikiunga direct toka sola na inveta bado hali ni ileile. Sijajua sola ndo mbovu au betri.
Inverter ya wats ngapi unatumia?
 
Mkuu inawezeka kufanya wiring mbili kwa wakati mmoja kwa maana ya umeme wa tanesco kivyake na wa solar kivya(Njia), maana yangu ni kwamba endapo umeme wa Tanesco umekatia/huitaji kutumia - unafanya matumizi kwa njia ya solar..
Sio lazima hapa unaweka kitu kinaitwa change over switch kubadilisha na kuna zingine ni automatic
 
wakuu nina solar kutoka Mobisol ni imara sana. Nimenunua 200w na sasa ni zaidi ya miaka miwili inapiga kazi vizuri na tv inch 32, sabufa, feni na pasi na taa 8 na walinifanyia wayaring bure.. Hiyo battery ni OG from Germany ni nzito mno na haina maji, yaani dry cell. Mobisol wana bidhaa bora sana za sola. Tembelea ofisi zao
 
wakuu nina solar kutoka Mobisol ni imara sana. Nimenunua 200w na sasa ni zaidi ya miaka miwili inapiga kazi vizuri na tv inch 32, sabufa, feni na pasi na taa 8 na walinifanyia wayaring bure.. Hiyo battery ni OG from Germany ni nzito mno na haina maji, yaani dry cell. Mobisol wana bidhaa bora sana za sola. Tembelea ofisi zao
Bei gani kwa system hiyo?
 
Mtaalam nisaidie hili. Nina Sola 60Wt betri N50 haijaisha maji ipo full lakini jua likizima tu basi Inveter nayo haipeleki moto, likiwa tu inafanya kazi kama kawaida hata nikiunga direct toka sola na inveta bado hali ni ileile. Sijajua sola ndo mbovu au betri.
Je umefunga charge control au bado? Labda nikukumbushe kuwa sora raha yake ni nilizevu ya moto. Ukitaka ufaidi sora hata kwa panel kama hiyo funga betri kubwa ya N 150 _ 200. Halafu usitumie betri mpaka ijae kama una charge control Kama huna charge control utaua betri mara moja na pia hiyo betri yako ni ndogo sana itatumika kwa muda mfupi sana .Kumbuka taa kutumia DC badala ya AC na taa zichukulie kwenye charge control ili usiwe unakomba kabisa moto.
 
pia mkuu baada ya kuweka maji hayo mapole nitatakiwa kuanika kwenye jua au sio lazima kuanika kwenye jua
Anika kwenye jua kama umeweka maji mapya na isiwe chini ya dakika 20, lakini kama ni maji ya kuongezea hayana haja ya kuanika juani.
 
Kama maji yamepungua kutokana na kumwagika basi unatakiwa kumwaga maji yote na kuweka mapya. Lakini kama yamepungua kwasababu za kawaida yaani kwa sababu ya kutumia (evaporation due to chemical processes) basi unatakiwa kuweka maji mapole (distilled water) hadi cell zote zijae. Usiweke maji hadi kufunika vitundu vilivyoko ndani kwaajili ya kupumulia kwani maji yatamwagika. Tafuta maji ambayo ni genuine.
asante kwa ushauri mwanana mkuu
 
maji makali usijazilize ongeza maji mapole yapo kwenye maduka ya vifaa vya magari kama hujawa tayari kuyamwaga yote, lakini maji kama uamechoka mwaga uweke mapya. TAFADHARI USIONGEZE MAJI MAKALI utaua betri.
hivi mkuu kama hutajari sababu ya kuweka maji mapore ni ipi ukizingatia yaliyomo ndani ya betri ni makali
 
hivi mkuu kama hutajari sababu ya kuweka maji mapore ni ipi ukizingatia yaliyomo ndani ya betri ni makali
Wakuu kuepukana na matapeli au kununua vitu usivyovijua ni bora uwaone Mobisol upate taarifa sahihi. Usije ukashikishiwa masola ya wahindi na wachina yanakufa baada ya siku chache. PIGA 0800755000 BURE KABISA KWA LINE YA VODA. UTAPEWA MAELEKEZO NA MAFUNDI WATAALAM WALIOPATA MAFUNZO KUTOKA UJERUMANI...
 
USAHIHI wa umeme wa solar unatokana na uimara wa solar system ikiambatanishwa na betry dry na kitaalam tunajifunza kuwa BETRI ZA MAJI....
kwa ajili ya kufanyia ulipuzi "starting machine" huwa zina asili ya kujazwa moto mapema na hupungua kwa muda mfupi.
Na ndio maana ni mara chache kukuta betri kavu zikitumika kwenye pikpk, gari, generator n.k.
Hii inatokana na mfumo wa utengenezwaji wa hizi betry.
BETRY KAVU...
Hizi huwa na sifa zinazotofautiana na za maji na huwa zinajaza kwa taratibu na moto ukishajaa huwa inahifadhi kwa muda mrefu pasina kupungua.
Kwa hiyo basi ktk solar system tunashauriwa kutumia dry betry kukwepa vitu vifuatavyo..
1. Usumbufu wa kubadilibadili maji.
2. Ufahamu wa kujua maji "Acid" hailisi na feki ni ngumu.
3. Ujazwaji wa mapema humsaidia tu yule mwenye direct system ila mwenye kuchaji kwa jirani haimnufaishi kwa betry za maji zinahitaji kila cku zile moto.
4. Kuepuka madhara ya acid endapo itamwagika vibaya wakati wa kufanya changes.
.... Na ni mara chache kukuta kampuni ya solar ikawa inafanya installation na ktk hiyo system wakatumia betry za maji.
Zipo sehemu zimefanywa kazi kwa hizi system na tofauti take hujionesha ndani ya miezi 6 tu.
N. B
Katika uwekaji system tuzingatie vifaa vinaendana kinamna ipi?
Kikanuni solar lazima iwe kubwa zan betry na kipo kiwango ambacho hata usipoweka charger control betry haiwezi kuasiliwa hii hutokana na makadilio sahihi yatakayofanyika wakati wa planning.
Na yapo maeneo kama mbeya, iringa, sumbawanga na maeneo km hayo ambayo jua kwao la kuvizia hawa charge control huhusika sana kwani waweza weka solar 70Watt na betry ikawa 40N ukatumia kwa muda mrefu kutokana na jua kuwa hafifu kwa cku nyingi ila tambua cku likiwaka 12hours betri yako itakuwa matatani kwa hiyo ni muhimu kuweka charge control.
Ila kwa ukanda wa pwani na mikoa ya dodoma na jiranize hawa waweza ukawa na 100Watt na 90N au isipungue chini ya 85 waweza unga bili charge control na isiasiliwe berty.
Na kwa nini tusitumie charge control ni ukweli usiopingika charger control zilizopo nyingi tunazoletewa wabongo kila ifikapo masika huwa zinasumbua na hii inatokana na tafiti wanazofanya ktk utengenezaji wa sola huwa ni kiangazi so bado "binafsi" sijaziona zinazimudu nyakati zote zikahimili kwa miaka mingi.
Cha msingi ni kuoanisha material zinzofanana kitaalam ili kukwepa hizi adha...
... Kwa ufahamu wangu......
 
Mkuu inawezeka kufanya wiring mbili kwa wakati mmoja kwa maana ya umeme wa tanesco kivyake na wa solar kivya(Njia), maana yangu ni kwamba endapo umeme wa Tanesco umekatia/huitaji kutumia - unafanya matumizi kwa njia ya solar..
Unaweza kufanya hivyo vizuri sana na tena unaweka automatic switch kutoka TANESCO kwenda solar au hata generator. Vifaa hivyo vipo madukani nenda Kariakoo. Ukitaka kuinjoi solar fanya isiwe ndogo sana iwe kuanzia 200 watts hivi, mimi nafanya mambo mengi sana na 200 watts tv, laptop kuanzia asubuhi hadi saa 11 jioni na tena masaa 2 tv kuanzia saa 2 hadi 4 na tena taa 5 zinabaki zikiwaka nje hadi asubuhi. Hapo mchana natumia blenda, pasi, nk. Ukiwa na pesa solar ni safi saana!
 
Back
Top Bottom