Unafanya uamuzi mzuri sana wa kuwa na solar power. Navyo andika hapa mimi nipo mbali kijijini Morogoro hakuna umeme wa Tanesco lakini naatumia laptop kuanzia asubuhi hadi jioni ipo kazini, Tv kubwa ya tumbo ipo on mda mrefu tu wa mchana na usiku naangalia walu masaa 2. Taa 5 each 5watts zinawaka nje usiku kucha achilia mbali zile za ndani. Natumia blenda ya juice, pasi ya solar, nachaji simu, nk. Hayo yote ni kwa panel 2 zenye kutoa watts 200 kwa jumla. Nina inverter ya watts 600 na charger ya amps 20. Nina battery moja tu ya maji Amph 100. Sijawahi kujuta au kukosa umeme tangu niweke solar hii mwaka 1 uliopita. Kama unataka kuwa na friji na feni napendekeza uifanye iwe na uwezo mara 2 hivi ya hii ya kwangu.
Nunua panels za watts 400, solar charger amps 30, inverter watts 1000 na battery 3 kila moja Amph 100. Hii system utaweza kupampu maji kutoka kwenye kisima pia na kweli utakuwa huru na Tanesco.
Usinunu battery zile wanaita dry battery kwani sio nzuri kama za maji (uzoefu wangu). Utakapoweka panel zako ziwe pasipo na kivuli na mwelekeo wake kama ni juu ya bati basi ziwekwe on flat surface, kama unaweza jenga mnara mfupi ardhini weka panel juu yake inategemea na usalama uliopo, fanya mnara huo uwe rotatable yaani unaweza kuuzungusha kufuata mwelekeo wa jua na hapo utaongeza ufanishi ya system yako kwa 30%. Enyoy.