Nelson nely
JF-Expert Member
- Jan 25, 2014
- 4,251
- 2,870
Habari za asubuhi,wakuu wiki iliyopita jumanne huku porini nikiwa nachimbua visiki kwa ajili ya maandalizi ya kuchoma mkaa kwa bahati mbaya sururu iliteleza na kukita kwa juu kidogo ya vidole vya mguu wa kulia,maumivu niliyoyapata siwezi kuelezea,sikutumia dawa yoyote zaidi ya panadol maana sikuwa na pesa.Ndani ya siku mbili maumivu yalipungua na nikawa na matumaini ya kuendelea na shughuli,lakini ghafla usiku wa kuamkia jumatatu nilipata maumivu makali mno kwenye mguu ule ule na mbaya zaidi wiki yote hii kwangu imekuwa ni kukesha na kulia tu na mguu unavimba na nahisi kama kunakuwa na baridi kali kwa ndani.Kwa kifupi hali yangu si nzuri na inabadilika kila kukicha,naomba kwa atakayeguswa na akawa ana uwezo wa kunikwamua kwa kiasi chochote ili nifikishe hiyo elfu 20 ili niweze kutoka huku kijijini nifike hospital nipate walau vipimo...0693265348,NATANGULIZA SHUKURANI.