Kwa ufupi mimi ni kijana wa chuo, nina ishi na baba na mama. Baba yangu ni mfanyabiashara, miaka 10-15 iliyopita baba alifanya biashara kwa karibu na mfanyabiashara mwenzie ambaye ni ndugu, katika makubaliano yao ya kumaliza kufanya biashara pamoja yule ndugu alikubali kumwachia baba yangu eneo lake tupu lililokuwa kama sehemu ya takataka miaka hiyo ya 90. baba akaliendeleza eneo lile kwa kupanda miti, kujenga fremu za kupangisha na kuendesha biashara yeye mwenyewe pia mahali pale.
Tatizo linakuja baada ya miaka zaidi ya 10-15 yule ndugu analitaka hilo eneo sasa! mwaka jana alifanya fujo kwa kubomoa baadhi ya majengo katika eneo hilo bila kufanya chochote katika eneo hilo, baba akalijenga tena eneo hilo, amebomoa tena mwaka huu! kwa kujali undugu baba hajaenda mahakani bado, na yule ndugu hataki mazungumzo ya kisheria anadai lile eneo ni lake.
Ninaomba ushauri... BABA YANGU ANA HAKI GANI ZA KISHERIA JUU YA ENEO(ARDHI) ILE?
- nikijibiwa kwa mujibu wa sheria nitashukuru zaidi.
Tatizo linakuja baada ya miaka zaidi ya 10-15 yule ndugu analitaka hilo eneo sasa! mwaka jana alifanya fujo kwa kubomoa baadhi ya majengo katika eneo hilo bila kufanya chochote katika eneo hilo, baba akalijenga tena eneo hilo, amebomoa tena mwaka huu! kwa kujali undugu baba hajaenda mahakani bado, na yule ndugu hataki mazungumzo ya kisheria anadai lile eneo ni lake.
Ninaomba ushauri... BABA YANGU ANA HAKI GANI ZA KISHERIA JUU YA ENEO(ARDHI) ILE?
- nikijibiwa kwa mujibu wa sheria nitashukuru zaidi.