Pantomath
JF-Expert Member
- Jan 4, 2019
- 789
- 3,230
Waziri wa Ardhi Mhe. Jerry Slaa leo amesimamia zoezi la Uvunjwaji wa Nyumba ya Johnson Mahululu ambaye anatuhumiwa kujenga nyumba katika eneo ambalo halimiliki kihalali .
Waziri wa Ardhi amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa eneo hilo ni mali halali ya Bi Naomi ambaye alikuwa akihangaika kulipata eneo lake kwa zaidi ya miaka 20.
Aidha amewaonya watu wenye tabia ya kuvamia maeneo ambayo si yao, na kusema kuwa Serikali imejipanga ipasavyo kuhakikisha inatatua kero zote za ardhi na kuwashughulikia wanaosababisha migogoro hiyo.