Kuna rafiki yangu tunaishi nae Kibamba, ni mfanya biashara wa kununua mashamba na kuuza. Hivi karibuni aliingia kwy matatizo baada ya kununua eneo akaamua kulikatakata viwanja, aliuza viwanja kwa wateja Kama watatu hivi, ndipo ilipokuja kubainika eneo Hilo kuwa Lina mgogoro wa kifamilia, ili bidi aanze kuwabadilishia wateja wake viwanja vingine,wateja wawili walikubali kubadilisha viwanja lakini mteja mmoja alikataa kabisa alihitaji pesa zake tu, mauziano ya kiwanja yalikuwa ni milioni mbili na laki moja. Rafiki yangu alikubali kurejesha pesa hizo, alilipa awamu ya kwa tshs 1,900,00/= zikabaki laki 2 ambazo zilitakiwa kulipwa tangu tarehe 31 mwezi wa nane 2020. Cha kushangaza zaidi mteja alikuja na magari mawili ya Police wakiwa na silaha za kivita huku wamefunika nyuso zao, akidai kuwa wametumwa kuja kumkamata huyo rafiki yangu kwa sababu ameshindwa kutimiza ahadi ya hiyo pesa. Mimi nikawaambia hiyo laki mbili mm nitawapatia Sasa hivi kwa sababu rafiki yangu hayupo amesafiri. Yule mteja alinijibu kuwa yeye anadai Tshs 1,100,000/= sio laki mbili, mm nikamuulia aonyeshe mkataba wake wa mauziano, alipouonyesha ulikuwa umeandikwa eneo alinunua kwa Tshs 2,100,000/=. Baada ya majadiliano kushindikana Mimi niliamua kuondoka, na wao waliondoka. Sasa Cha ajabu ni kwamba usiku walirudi tena nyumbani kwa rafiki yangu, wakaamua kumchukua mke wa rafiki yangu wakidai kuwa hadi walipwe pesa ndipo wamrejeshe. Sasa tumefuatilia huko central police walikodai wanampeleka, tukakuta maelezo kuwa pale walimleta kweli lkn mhusika(mdai) aliamua kumchukua na kumpeleka kwake. Mhusika nae inasemekana ni Police. Sasa happy katika swala la kisheria hili Jambo limekaaje? Je? Sheria zinaruhusu kumkamata mke wa mdaiwa? Naombeni msaada katika hili Jambo.