Msaada wa kisheria unahtajika hapa!

Msaada wa kisheria unahtajika hapa!

Holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
8,703
Reaction score
19,589
Wakuu, mwaka 1994, kuna mzee aliingia makubaliano ya kuuza eneo na halmashauri ya mji X, serikali ilitoa ahadi kuwa iwapo mwenye eneo atakubali kuiachia serikali basi yeye atanunuliwa kiwanja sehemu nyingine na atajengewa nyumba,mzee alikubali na serikali ikajenga majengo matatu katika eneo hilo,

Ila ile ahadi ya kumnunulia kiwanja na kumjengea nyumba mwenye eneo ikawa ni danadana mpaka leo. amefuatilia sana bila mafanikio mpaka mwaka huu 2026 akaamua aliuze hilo eneo,alipoliuza,mnunuzi akabomoa jengo moja, alipobomoa tu wananchi wa kijiji wakashtaki kuwa amenunua mali ya serikali wakati mwenye eneo hakuchukua hata cent1, wanasheria,yupi mwenye kosa hapo?
 
Tittle Deed finally iko mikononi mwa nani? kama mzee ali-sign au ku-transfer title deed kwa serikali, basi ardhi ilikuwa tayari ya serikali kisheria.

Lakini kama hakukuwa na transfer ya title deed, basi bado alikuwa mmiliki kisheria hata kama serikali ilijenga vitu juu yake.

Mnunuzi naye anaweza kuwa katika hatari, kama alinunua mali ya serikali.. compansation claim inawezekana kama tu mzee alikuwa tayari ameshaachia ardhi (lakini hajalipwa)
 
Back
Top Bottom