Msaada wa kimawazo: Nijenge au ninunue gari

Msaada wa kimawazo: Nijenge au ninunue gari

Beira Boy

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2016
Posts
23,986
Reaction score
42,210
Amani iwe nanyi wapendwa,

Husika na kichwa cha habari hapo juu,

Mimi ni mfanya biashara mwenye chini ya miaka 25 kwa sasa biashara zangu zinaenda tu fresh ukizangatia na saizi wafanyabiashara tumekuwa wachache sana sio kama zamani.

Sasa basi kuna milioni kumi na tano yangu iko bank nimeiweka yaani kila baada ya mda flani huwa naogeza milioni moja au laki kadhaa bank lakini inategemea na biashara itakavyosimama kwa mwezi au kwa week.

Nina viwanja viwili kwa sasa sina nyumba wala gari nimepanga na mishe mishe zangu huwa napiga kwa kupanda gari.

Sasa basi naomba ushauri wenu wadau, je nijenge nyumba au ninunue gari ili nirahisishe mishe mishe yangu kwa town.

Naombeni ushauri naogopa kunuua gari wakati nimepanga nahisi ndugu wataniona lofa lakin mimi mwenyewe ni sharo kinoma kamoyo kangu kanataka gari.


Nawasilisha


LONDON BABY
 
Kweli unahitaji msaada wa kimawazo. Utanunuaje gari huna mahali pa kuipaki?? Mwenye nyumba ukamwombe ujenge gereji ya kulaza gari au ukailaze ofisi ya ccm mtaa wa 4 kutoka nyumbani!! Yataka moyo.
Ushauri;
Jenga nyumba kwanza, weka frem nzuri mbili au tatu. Wapo watakao pangisha ka unavyo pangisha na nyingine tumia wewe. Mola akijalia, weka na sehemu ya gereji kwenye jengo lako. Utakuja ingiza gari siku moja kwako sio kwa mtu.
 
Gari ni working tool itakusaidia kwenye mishe zako ila nunua inayoendana na shughuli zako isije ikawa liability badala ya asset.
Mkuu nataka ninunue verossa nilipata ya 12 milion
 
Boss jipime tu wewe mwenyewe then amua kipi mhim, maana gari ni mhim sana kama itatumika kukurahisishia biashara, ila kama biashara inaenda vizuri bila gari bas anza kujenga nyumba ila pia nyumba hutafikia mbali ila itategemea ni nyumba ya ukubwa gan unaitaka.
 
Sikukatishi tamaa ,,bila kujali utafanya kipi Kati ya kujenga nyumba au kununua gari hutakuja kufilisika kabla ya 2022,,hauna akili ya biashara.
 
Kweli unahitaji msaada wa kimawazo. Utanunuaje gari huna mahali pa kuipaki?? Mwenye nyumba ukamwombe ujenge gereji ya kulaza gari au ukailaze ofisi ya ccm mtaa wa 4 kutoka nyumbani!! Yataka moyo.
Ushauri;
Jenga nyumba kwanza, weka frem nzuri mbili au tatu. Wapo watakao pangisha ka unavyo pangisha na nyingine tumia wewe. Mola akijalia, weka na sehemu ya gereji kwenye jengo lako. Utakuja ingiza gari siku moja kwako sio kwa mtu.
Asante sana mkuu mwenyez MUNGU akubalik
 
Back
Top Bottom