Msaada wa kazi ndugu watanzania wenzangu.

Msaada wa kazi ndugu watanzania wenzangu.

Joined
Feb 12, 2013
Posts
18
Reaction score
1
wapendwa watanzania wenzangu, naombeni connection ya kazi,nilikuwa nafanya kazi ya mkataba na wazungu lakini mkataba umeisha na mda wa wao kuishi hapa tanzania umeisha hivyo sina kazi.

nimezunguka sana maofisini na zaidi naingia galama zingine na kupoteza fedha nyingi kwa waajili bila mafanikio zaidi napewa danadana tu.

nimeleta maombi kwenu watanzania wenye huruma na wenye kuguswa nami, wanisaidie japo niweze kupata chochote ili wadogo zangu waendelee kusoma.

elimu yangu ni shahada ya sanaa na elimu "bachelor of arts with education' toka saint augustine university tanzania 2011.

sibagui kazi wala mazingira,0753 750 219 / 0714 212 268

napatikana mwanza(nyamagana)
 
Sredi yako inatia simanzi dah,hujajaribu kuwaomba wazungu muende nao labda?
 
Sijawaomba kwa sababu za kifamilia zaid, wazaz wangu ni wazee sana hivyo wadogo zangu wananitegemea hasa kwa kuwasomesha, hivyo kutoka nje ya nchi itakuwa ngumu kwa sasa.
 
Kwa nin hukuomba wizara ya elimu?
 
Niliomba lakin inaonekana nilikuwa namtumia wrong person mimi nikijua ndo top wa pale, lakin inaonekana haitowezekana kwa sasa au itachukuwa mda sana kupata nafasi.
 
Watanzania tumekusikia kama yupo anayekuhitaji atakupigia bt usikate tamaa endelea kujaribu shule za private na mashirika binafsi hope utapata
 
Fuga kuku wa cross breed. Achana na dhana ya kuajiriwa. Jiajiri pia.
 
Niliomba lakin inaonekana nilikuwa namtumia wrong person mimi nikijua ndo top wa pale, lakin inaonekana haitowezekana kwa sasa au itachukuwa mda sana kupata nafasi.

Kwa nini unamtumia mtu badala ya kufuata taratibu??Na je umeulizia mbalimbali pale tume ya ajira?umewahi kufikiri kuhus kuwa mfanyabiashara????Huko Mwanza hakuna opportunities za kufanya biashara?
 
pole kaka!kwa hyo koz yako ya arts with education nadhan inawezekana ukafundisha?mi naona ungejaribu kuapply kufundisha ata kwenye shule za private.
 
Kwa nini unamtumia mtu badala ya kufuata taratibu??Na je umeulizia mbalimbali pale tume ya ajira?umewahi kufikiri kuhus kuwa mfanyabiashara????Huko Mwanza hakuna opportunities za kufanya biashara?
< <


i concur with u!
 
Kwa nini unamtumia mtu badala ya kufuata taratibu??Na je umeulizia mbalimbali pale tume ya ajira?umewahi kufikiri kuhus kuwa mfanyabiashara????Huko Mwanza hakuna opportunities za kufanya biashara?

niliamini kumtumia m2 kungesababisha kuleta mafanikio haraka zaidi kwani nimeanza nimeanza kufuatilia suala hili tangu sept 2012, kuhusu fursa ya biashara ipo, nilikuwa na salon ya kike hapa mjini lakin kutokana na mizunguko mingi pindi niko na hawa wazungu , msimamizi wangu akawa ametokomea na v2 vya salon na kukuta frame iko tupu, na kwa sasa sina mtaji maana hela niliyokuwa nayo ikabid niwalipie ada wadogo zangu 3, wawili chuo na wa mwisho form 3.
 
pole kaka!kwa hyo koz yako ya arts with education nadhan inawezekana ukafundisha?mi naona ungejaribu kuapply kufundisha ata kwenye shule za private.

nimejaribu kuapply sana, lakin nimegundua kikwazo ni hii kazi niliyokuwa nafanya ilikuwa haiendani na teaching, nilikuwa nafanya kazi Research and Publication work as Assistant to Research Director.
 
Pole! Vip kile ulichokuwa umekusanya! Cdhani kama chote ulikuwa unawasaidia ndugu!zako I mean your salary percentage! Ulikuwa ubakizi hata kidogo!
Ushauri!! Fanya biashara,,KUAJIRIWA MBELE YA SAFARI!
 
Pole! Vip kile ulichokuwa umekusanya! Cdhani kama chote ulikuwa unawasaidia ndugu!zako I mean your salary percentage! Ulikuwa ubakizi hata kidogo!
Ushauri!! Fanya biashara,,KUAJIRIWA MBELE YA SAFARI!

niliinvest kwenye salon ya kike lakin mjanja katokemea nayo mitin, nami napenda sana biashara ila kwa sasa niko empty guyz, hawa wadogo zangu wa chou ni private scholaz saut na sokoine hivyo cost zao mimi, cjui nifanyeje........
 
nakutakia mafanikio ndugu but usiache kuwasumbua hao mabosi,pita kwenye makampuni kama kichaa kuliko kukaa tu ndani(kukata tamaa),halafu suala la kufanya kazi nje ya nchi mi nadhani kama kuna chance ya wewe kupata ungefanya tu kwani kama ni kuiangalia familia hata ukilala nao na kuamka nao kama hamna kitu cha kula watakukula wewe nyama? au ukiwa karibu mgonjwa anapona?u just go ukipata kitu kidogo unawakumbuka.Au pia jaribu kuongea nao kwanza,uone response yao itakuwaje.
Pia naamini kupitia hapa JF kuna watu watakusaidia kutokana na position zao
 
nakutakia mafanikio ndugu but usiache kuwasumbua hao mabosi,pita kwenye makampuni kama kichaa kuliko kukaa tu ndani(kukata tamaa),halafu suala la kufanya kazi nje ya nchi mi nadhani kama kuna chance ya wewe kupata ungefanya tu kwani kama ni kuiangalia familia hata ukilala nao na kuamka nao kama hamna kitu cha kula watakukula wewe nyama? au ukiwa karibu mgonjwa anapona?u just go ukipata kitu kidogo unawakumbuka.Au pia jaribu kuongea nao kwanza,uone response yao itakuwaje.
Pia naamini kupitia hapa JF kuna watu watakusaidia kutokana na position zao

shukran kwa mawazo mazuri ndugu, zaidi sitoweza kukata tamaa na kukaa ndani tu, pia wazo la kufanya kazi nje naliafiki na jana nimetoka kujaza form za VSO( Voluntary Service Overseas) lakini nimelazimika kufanya hivyo kwa sababu ya uhaba wa ajira though itachukua mda mrefu, na kuwa mbali na wazee co tatizo lakini sikupenda iwe nje ya Africa, hata hivyo mimi niko Mwanza lakin wazee wangu wako Ipinda(kyela /Mbeya) lakini nawafikia kiurahisi.

N.b bado sijakata tamaa na niko tayali kufanya kazi Yoyote ndani ya Tanzania kama itapatikana.

thanx in advance best for your courageous
 
Kwa 'profiling' ya haraka haraka inaonyesha unapenda zaidi kufanya kazi na wageni -nakushauri hii weka pembeni. Kazi zipo sana lakini kwanza 'you have to be very good'. Pili usichague kazi. Unaweza kupata hata kazi ambayo hujaisomea ikiwa tu unaweza kutetea hoja zako vizuri katika usaili. Tatu uandishi wa CV pia una-'put off' sana waajiri hivyo jitazame.Kwa kuandika CV vizuri inaweza kukufanya uitwe kwenye usaili hata kama huna sifa za kutosha..
 
Tumia elimu yako kujiajiri.hukuweka akiba ulipokuwa na wazungu?.kumbuka "a degree holder should be a job creator and not a job seeker".
 
Back
Top Bottom