Msaada wa haraka jamani

Miken

Member
Jan 17, 2011
15
1
Naombeni mnisaidie katika hili:
Nina mpenzi wangu anasoma pale UDOM na tumepanga kuoana japo kuna mambo yananikwaza.Tulianza mapenzi siku nyingi kidogo na baadaye yeye kaenda kusoma.Alipofika tu pale chuoni akakutana na jamaa mmoja ambaye amemteka na wamekuwa wakifanya mapenzi mara kwa mara Dom,Arusha na hata Moshi kwa ni wote wanatoka Moshi.Nikimuuliza huyu wangu anakana na nimewahi kumpigia huyo jamaa naye kagoma,namba yake niliifuma kwenye simu ya huyu mpenzi wangu japo huwa hamwandiki jina huyo jamaa ila nalijua.Tangia waanze mchezo huo huyu wangu amekuwa na tabia ya kunisuspect kuwa nina mpenzi mwingine japo kweli nimewahi kuzaa na dada mmoja kabla ya kuanza mapenzi na huyu N wa UDOM.Nimeweka mtego nimkamate huyo mwizi wangu ila huyu N kategua na hadi sasa watafiti wangu wananipa habari kwamba bado wanaendeleza mchezo na kila nikimwuliza anagoma.Tumepanga kuoana naye lakini sasa nakatishwa tamaa,nifanyeje?mimi nipo dar.
 
Huyu ameshakuona sio type yake,so We anza tu mbele kwa mbele achana nae kwani Ita ku cost ndugu
 
Naombeni mnisaidie katika hili:
Nina mpenzi wangu anasoma pale UDOM na tumepanga kuoana japo kuna mambo yananikwaza.Tulianza mapenzi siku nyingi kidogo na baadaye yeye kaenda kusoma.Alipofika tu pale chuoni akakutana na jamaa mmoja ambaye amemteka na wamekuwa wakifanya mapenzi mara kwa mara Dom,Arusha na hata Moshi kwa ni wote wanatoka Moshi.Nikimuuliza huyu wangu anakana na nimewahi kumpigia huyo jamaa naye kagoma,namba yake niliifuma kwenye simu ya huyu mpenzi wangu japo huwa hamwandiki jina huyo jamaa ila nalijua.Tangia waanze mchezo huo huyu wangu amekuwa na tabia ya kunisuspect kuwa nina mpenzi mwingine japo kweli nimewahi kuzaa na dada mmoja kabla ya kuanza mapenzi na huyu N wa UDOM.Nimeweka mtego nimkamate huyo mwizi wangu ila huyu N kategua na hadi sasa watafiti wangu wananipa habari kwamba bado wanaendeleza mchezo na kila nikimwuliza anagoma.Tumepanga kuoana naye lakini sasa nakatishwa tamaa,nifanyeje?mimi nipo dar.

kaka najua inakuuma na itakua ngumu kwako kufanya hili nikwambialo.chakufanya ni wewe kujityuni na kufanya maamuz ya kumpiga chini.na kujilazisha kihisia kumsahau vinginevyo ukilazimisha yatakuja kukuta makubwa zaid kipindi ambacho kitakua nikigumu kuachana nae,funua page mpya ya mapenz na usikulupuke kumtafuta mwingine kwani machungu uliyo nayo yatakufanya uangukie pabaya zaid.mshukuru mungu kwa kuweza kumgundua mapema na pia muombe mungu akuletee mzuri,mwema,mwaminifu zaid ya huyo.mwamini mungu anaweza!pole sana kaka
 
thank god umegundua na si vizuri kuwa na mtu uliye na mashaka naye, cha msingi usikurupuke, fanya uchunguzi kwanza then ndo uamue, merriage its not a word but sentence to life(for christian)
 
Mmmh...wewe utakuwa ni mtu wa nne kusikia habari kama yako,ninao rafiki zangu watatu nao walikuwa na wapenzi wao hapohapo udom lakini hawajadumu nao na wao wanawake nao walikuja na tuhuma kama yako uliyopewa eti wanasikia rafiki zangu wanawapenzi wengne yani ni foolishness na stupidy ideas...bro think wisely and act wisely ktk swala kama hlo,otherwise pole na take care bro kwani udom ni hataaari
 
Haupendeki tena kaka wewe angalia ustaarabu mwingine shukuru Mungu amekuonyesha mapema kabla hujafunga zile pingu
 
Kuthibitisha muhimu, lakini sio kila kitu kinaweza kuthibitishwa bro, wataalam wanasema ukigundua tatizo kabla ya ndoa ni bora ukalifanyia kazi kabla ya ndoa, usitegemee mabadiliko baada ya ndoa (ni bahati sana). Achana na mitego ya kukamatana unaweza ishia kuua au kuuawa, elekeza nguvu zako kutafuta pesa na utapata the right one kama ni huyo au mwingine.
 
Pole sana kwa masaibu yaliyokupata. Hata hivyo bora umegundua mapema. Kama mambo mabaya sasa, yatakuwa mabaya zaidi baadaye.

Kwa mtazamo wangu, huyo si wako, waachie wenyewe! Ndoa si suala la haraka. Nakushauri utulie na umuombe Mungu akupe aliye wako. Kwa sisi wakristo hatuoi kwa ajili yetu pekee, tunaoa kwa ajili ya Mungu pia! Tunaoa yule atakayekuwa msaada katika safari yetu ya kumtumikia Mungu na hatimaye kufika mbinguni. Kwa mtazamo wangu, binti huyo anaweza kuwa mzigo mkubwa si tu kwa familia mtakayoianzisha bali hata katika kumtumikia Mungu ambalo ndilo dhumuni kubwa la uwepo wetu. Kumbuka pia, ndoa ya kikristo ikishafungwa, HAKUNA WA KUIVUNJA! Nje ya hapo ni uzinzi tu!

Mungu akusaidie sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom