Msaada wa haraka hii hesabu!!!

Wale wataalam wa hesabu hebu nisaidieni namna ya kusolve hii haraka, nimejaribu njia zote nimeshindwa (Log... etc), sasa sijui ni uzee unanisumbua!!


2[SUP]x[/SUP]=4X

The answer is 4, sasa tatizo ni namna ya kuipata hiyo 4.

kaka hiyo sio Hesabu ni HISABATI hesabu kila mtu anaweza zile za kuuzia machungwa ndo hesabu!!!
 
nami nakubali hiyo sio hesabu ila ni hisabati, na naomba watu wawakubali watu waliofanya vizuri ktk mambo mbalimbali. "APPRECIATION WANDUGU"
 
2^x =4x......log
log2 ^x=log4x.
Xlog2=log(2^2)X.
Xlog2=log(2^2)+logX.
Xlog2=2log2+logX
logX=Xlog2-2log2
logX=(X-2)Log2
X=(X-2)2
X=2X-4
4=2X-X
X=4.

Kuanzia leo!!! I salute u! Mweleshe tu kama base na log ya namba zinafanana jibu lake ni moja
 

Huyu ndie mke nilipaswa kua nae!!! kichwa nzuri hata nikikuambie tusinunue cheni na tununue matofari haraka utanielewa!!! hongera sana!! proud of u!!
 
hapa bila kuchora graph au kutumia try and error method hamna jibu.
 
Nimeipenda hii.
Nimeanza kufanya mazoezi ya kukokotoa maana dogo anakuja kwa kasi sana, nisije nikaumbuka bure
 
hapa bila kuchora graph au kutumia try and error method hamna jibu.

Wajua hisabati kweli?

Njia aliyotumia mdada ni sawa kabisa hakuna cha graph hapo!! kaaply theory za log tu!!

amenikumbusha mbali sana niliwapeleka noma
 
kaka hiyo sio Hesabu ni HISABATI hesabu kila mtu anaweza zile za kuuzia machungwa ndo hesabu!!!


Za kuuzia machungwa ni MA.GA.ZI.JU.TO........... Remember? kwangu mimi hesabu ni jenero tem hata kuhesabu vidole ni Hesabu.
 

hapo kapitiwa
 

wakuu sikupenda kujiingiza kwenye hii mada lakini nimelazimika na huyu husninyo anavyokuwa anajibadilisha jinsi kama siyo jinsia kwa kila mada hii anakuwa anategemea nini au watu hawafuatilii michangoo yake humu jamvini...huyuhuyu kuna sehemau amejitambulisha kuwa yeye ni he na siyo she....hapa bwana Dasa amembana na ghafla amekanusha kuwa yeye siyo he ni she........

Nini kulikoni..jamani ni wazo tu na halitaki kujibiwa ila siyo vizuri kukanganya wanajamii kwa namna hiyo
 
logx =1............................ .............................. ...andika
hiyo katika mfumo wa
log under base, log2(x-2) log 2(x-2) X=1........................... .............................. .........................ibadi lishe katika exponential
form 2(x-2)^1=x
Husninyo,hapo ndo penye uongo! Huwezi ibadili kiivyo.(X-2)log2 sio sawa na log2(X-2),bali ni (X-2)log2=log2^(X-2) na sio vinginevyo.Ishu hapo ni kutumia gragh tu! Kutumia log concept ni kulazimishana uongo tu!
 
Last edited by a moderator:
Husninyo na dasa mnanikumbusha mbali, asanteni ndugu zangu. Ninachoweza kusema kwa leo na siku zote ni numbers do not lie. Big up.
 
Hapo mie naona kama niko gengeni nanunua nazi, mwe!

yaan,,,naichukia hesabu kama msiba wa kambarage,,,,mliosoma lyamungo sec,,,miaka,ya,1989/92,,,mnamkumbuka mama pallagyo,,,,akitukusanya,,,form/either/jktu,,mnajazwa class ya wa2 35 mnaingia 150,,hata ufanyaje,atakuacha,,sasa siwezi kuipenda tena japo pr loo bonge ya mkali enzi hizoooooooo,acha tu,,
 
Heshima mkuu. lakini kwenye red hiyo sheria ni ipi hiyo!!. hiyo Log jinsi ilivyopotea hapo!!.

maana nilitegemea iwe:

LogX=(X-2)Log2
X=2[SUP](X-2)[/SUP] then uendelee kutoka hapo.

Hiyo sheria uliyotumia hapo juu, naomba ifafanue zaidi.

safi sana husininyo.Hapo kwenye red,their is no such a law.
 
Hapo ndo tungundue tatizo la mfumo wetu wa elimu! Nijuavyo mimi nivigumu kwa mtu ambaye amemaliza shule 20 years ago,hata kama alikuwa mkali kwenye masomo husika endapo hilo somo sio eneo lake la kazi (walau anajikumbushia kila mara)usishangae kumkuta mtu anajiuliza endapo aliwahi kuona kitu kama hicho. Kwa sisi tuliowahi kuwa walimu nadhani huwa inaudhi unapowauliza wanafunzi kuhusu topic fulani ambayo walikuwa wanafundishwa na mwalimu aliyetangulia kisha unaambiwa HATUKUFNDIHWA HAPO! Kumbe wanafunzi wameandika kwa ajili ya test na kisha wanaweka material kapuni. Kwa mtindo huu unawezekana kabisa kushindwa hata mambo madogo ya msingi
Hizi ngoma nilikuwaga vema sana, tatizo ni hizi shule za kufanyia mitihani huwezi amini ngoma imekataa kabisa shiiit. Alafu leo hii nipo kazini kwasababu nilifanya vizuri katika masomo yangu
 
SASA NAONA WOTE CHALI KI2 HICHI SIMCHEZO.
O-level MTUPISHE KIDOGO
IT'S GOING DOWN LIKE THIS...
2^x = 4x
1 = 4x*2^(-x)
1/4 = x*2^(-x)
1/4 = x*e^(-x ln(2))
-ln(2)/4 = -x ln(2)*e^(-x ln(2))
W(-ln(2)/4) = -x ln(2)
W(-ln(2)/4) / -ln(2) = x
Where W is the Lambert W-Function.
Wolfram Alpha approximates the
solution as
0.309906932380
KAMA HUJAELEWA AU KUNA SEHEMU
UMEACHWA ULIZA. MATHEMATICS BONGO NI
UGONJWA WA TAIFA.
 
Elineema 🙌
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…