charging system /charging unit/charging pcb ni saketi ya ndani kabisa kwenye simu ambayo hii ndio inayocontrol jinsi umeme unavyotoka kwenye charge/adapter kuingia kwenye simu na battery wakati wa kuchaji simu.
Usb port ni hilo tundu ambapo unapochomeka charger/adapter , tundu hilo inaweza kuwa micro usb 2.0 au usb 3.0 kwa simu kubwa kubwa kama vile galaxy note 3. Mara nyingi tundu hili ndilo linasababisha matatizo ya kuchaji simu yako endapo kuna pini zilizoachia (dry joints) au kama ile plastic ya ndani ya port imepata crack/pengo au imevunjika.
Matatizo haya mara nyingine tunayasababisha wenyewe kwa -:
1. Kutumia chaja zisizo na ubora, zingine zinabana sana lakini tunaziingiza kwa kulazimisha...
2. Makosa wakati wa kuchomoa chaja, ukitwist chaja wakati wa kuichomoa huchangia kulegeza au kusababisa dry joints..
3. Kudondosha simu wakati unachaji, hii ni hatari sana na inaweza kung'oa usb port kabisa.
4. Kuegemeza simu vibaya wakati umechomeka usb cable/charger, yaani unakuta ile cable ndio egemeo la simu.