Msaada: UTAFUTAJI WA MAISHA SUDANI

Msaada: UTAFUTAJI WA MAISHA SUDANI

the-need

Member
Joined
Jan 2, 2014
Posts
56
Reaction score
29
Ndugu wana jf...kutokana na ugumu wa maisha nilionao sasa. Nimesikia sudani kuna kazi nyingi sana tofauti na hapa kwetu. Nina elimu ya degree ya BA. Sina kazi kwa muda mrefu sana. Nataka niende huko sudani kutafuta maisha.


Sina mtu ninayemjua huko. Sina pa kufikia. Lakini nipo tayari kuishi maisha ya mtaani huku nikitafuta chochote.


Kwa mwenye taarifa za huko anipe ramani. Ni mji gani naweza kufikia na kuanza harakati za maisha?


Ni kweli kwamba kuna ajira za nyingi tofauti na hapa?
 
hata mimi nataka kuzamia huko mkuu....ngoja waje waliowahifika huko mkuu
 
Sudan ni nchi kubwa sana siui wewe unataka kwenda wapi?
Kuna majimbo kama Cordovan,Abyei,Darfur,au Khartum?
Kazi zipo ila baadhi ya majimbo usalama ni mdogo.
Unaweza kufanya mpango ktk mashirika ya UN au makampuni ya uchimbaji wa mafuta ktk majimbo hayo.
 
Kazi mbona nyingi tu,si Sudan pekee,jaribu kucheki Central Africa,Somalia,Syria,Mashariki DRC na Afghanistan.
 
Nipo serious kwenye hili. Kwa kua upo kwenye kiyoyozi umemaliza kula chakula kizuri na maji ya kilimanjaro pembeni unaona raha kujibu mavi kwenye thread za watu. Acheni kufuru. Mi nna shida...acheni porojo....kama hujui lolote sio lazima kjibu.
 
Ukienda uko Jiandae kujitoa muhanga ama tafuta mabomu ya kujilinda
 
Kama una nia ya kwenda sudan tafuta kazi un ama kwenye mashirika yaliyo chini ya un. Usitegemee kwenda na vyeti ukapata kazi kule kimsingi haziko kihivyo hata wao wana wasomi lakini hawana kazi
 
Jamaniii... the guy is serious hapa. Mumelazimishwa ku reply? Au limbukeni.
 
Sudan kusini nadhani ndio ulikua unamaanisha,maana ni taifa jipya lililoanza kujengwa kwa kasi sana kabla ya haya machafuko....Aljazeera kuna siku walionesha documentary na kunaonekana kunafursa nyingi sana na hata ishu za kodi kule ni kidogo sana...ndio maana kwa upande wa magari ya kifahari hakuna mji wa afrika unafikia Juba japo ni mji mchanga na maghorofa ndo kwanza yalianza kuibuka,,,mi sijafika huko ila nimejifunza kupitia tv na jamaa yangu aliefanya kazi huko...wakenya na waganda huko ni wengi sana na wanapiga hadi dili za kuuza maji na mitumba walihojiwa wakaonekana kufurahia sana maisha ya huko na wanaonekana kupiga hela...kwa hiyo kama unampango huo labda uende sudan kusini pakitulia...wawekezaji wanapatolea macho sana
 
Pole sana the need.Kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea kwa sasa wafanyakazi karibu wote wamepewa likizo ya dharura na wengi wamerudi ktk nchi zao.Labda usubirie ipatikane amani kwanza ndipo uanze harakati ya kutaguta kazi huko.Hata hivyo sikushauri uende kwa kuzamia askari wa huko hawana mchezo.Ninachojua bado nchi hii ina nafasi nyingi za kazi jitahidi kuwa una search nafasi mbalimbali za kazi hatimaye unaweza kufanikiwa.Mimi.nilijatibu mwaka jana nikafanikiwa waliniita lakini sikwenda kwanza mshahara waliokuwa wanilipe ulikuwa kidogo na pia eneo au jimbo nililokuwa niende usalama wake ulikuwa ni mdogo nika decline offer.
 
Ndugu wana jf...kutokana na ugumu wa maisha nilionao sasa. Nimesikia sudani kuna kazi nyingi sana tofauti na hapa kwetu. Nina elimu ya degree ya BA. Sina kazi kwa muda mrefu sana. Nataka niende huko sudani kutafuta maisha.


Sina mtu ninayemjua huko. Sina pa kufikia. Lakini nipo tayari kuishi maisha ya mtaani huku nikitafuta chochote.


Kwa mwenye taarifa za huko anipe ramani. Ni mji gani naweza kufikia na kuanza harakati za maisha?


Ni kweli kwamba kuna ajira za nyingi tofauti na hapa?

Unataka kwenda sudan gani?
sudan au sudan kusini?
 
Mr.Mark....nataka kwenda Sudan yenye unafuu. I mean....jimbo au sehem ambayo naweza kufight maisha na kutoka. Najua mwanzo utakua mgumu. Na kama nilivyotangulia kusema awali...nipo tayari hata kwa kuanza kua kuri...au mjenzi. Kwa kazi za chini kabisa za mtu ambae hajasoma.
 
Watu wanakimbia wewe ndio unataka kwenda. Fursa ambazo zipo kama we ni mfanyabiashara
 
Mr.Mark....nataka kwenda Sudan yenye unafuu. I mean....jimbo au sehem ambayo naweza kufight maisha na kutoka. Najua mwanzo utakua mgumu. Na kama nilivyotangulia kusema awali...nipo tayari hata kwa kuanza kua kuri...au mjenzi. Kwa kazi za chini kabisa za mtu ambae hajasoma.

unataka kuendaje kwanza kwa kuzamia au kwa kufuata taratibu halari?

kwa khartoum na miji yake labda naweza kuwa na idea.

1.Lugha ya mawasiliano pale inaitwa darijia hii ni sleng ya kiarabu, kama utakuwa hujui kiarabu communication itakupa tabu sana.

2.lugha ya kingereza zaidi inatumiwa na watoto wa familia bora na wageni na mostly waganda na wasudani kusini ambao wengi pale waliishi kama daraja la chini mno.

3.khartoum ni mji wenye maendeleo makubwa mno, jinsi ilivyo khartoum ina mikoa/wilaya tatu nazo ni bahari,omduruman na khartoum yenyewe. kwakuwa ni mji ulioendelea sana basi hata population yake ni kubwa sana na kazi hasa za ujenzi ni nyingi sana.

4.tatizo kubwa nililoliona pale ili uwe na amani unatakiwa uwe na work permit siyo rahisi kuishi bila permit, kwani misako ni mingi na ni any time, police wanaweza amua funga mtaa mfano msimbazi kisha wakakusanywa vijana wote wasioeleweka eleweka na kupelekwa shurutwa/police kisha unahojiwa ukichemka tu unafungwa

5.ukitaka uende vizuri kwanza ni uwe na mwenyeji kule, kisha uende kihalali kabisa ukifika kule ulipie working permit kisha ndio uanze kusaka kazi. kama una proffesional am sure unaweza pata kwenye UN aggencies zipo nyingi sana na wanakuwa wanahitaji wanaojua kizungu. wasudani wengi kizungu wameanza kukisoma miaka hii hii ya 2000.

6.kwa sasa kuna vijana wengi wa kizambia wanafanya kazi za kufundisha kwenye academy na british council center.

7.pale kulikuwa na mabaharia wengi sana na bado wako ila kutokana na life ilivyongumu na walikuwa hawako kiharali I saw them just surfaring there.

8.mabaharia wajanja ili kumudu life na kupata backup ya kuishi pale waliamua kuowa watoto wa kisudani, watoto wa kisudan ni wakali ila kwa kwakuwa wewe ni ngozi nyeusi kama utakuwa unafanya kazi za box utaishia kwa wadinka(they are very very very black by nature)

...............
.........
 
kama ni BA in political science nakushauri utafute jimbo au kata hapahapa nyumbani ujaribu kugombea
 
Back
Top Bottom