Mbuzi usifuge, wanunue/wakusanye unawafanyia fattening/kunenepesha miezi miwili mitatu unawauza.
Ukifuga mbuzi kwa leo la kuwazalisha wawe wengi hayo maisha yako hayatabadirika. Waige wasomali, wananunua mbuzi wadogo wadogo minadani, wanawaweka kwenye mazizi yao ya muda, wwananenepesha miezi mitatu l, wana sort wanawauza mikoani. Hujawahi kutana na fuso tandam imejaa mbuzi wanapelekwa mjini?
Mbuzi wakutengeneze mzunguko, nunua uza. Maana mbuzi hana magonjwa, ila ni msumbufu kumfuga kwa lengo la kumzalisha.
Nenda pembeni kwa kutulia, unanunua mbuzi ambae ukimhudumia miezi mitatu anafaa kuliwa na kuuzwa. Unakusanya kwa bei ndogo, unakuja muuza kwa bei kubwa. Kila baada ya miezi minne unatoa mbuzi shambani kupeleka sokoni, wanazunguka. Ukianza sijui uwazalishe wafike kadhaa utachelewa.