Msaada: TV yangu imezima na haiwaki tena

normally

Senior Member
Aug 1, 2018
194
166
Habari wakuu,

Naomba ushauri wenu majuzi kati nilipata vijesent vyangu nikanunua tv ya hisense sasa nimetumia wiki mbili tu.

Juzi wakati nataka kuunganisha na subwoofer nashika wire naona tv imezima ghafla nikajaribu kila njia naona haiwaki, sasa wakuu naomba ushauri wenu nifanyaje.
 
IMG_5155.jpg

Kagua hiyo fuse kama ipo okey
Sasa sijui utapaje na wewe sio fundi
 
Watakuja kukuambia Hisense ni mchina mwenye jina lake mjini.

Or ilikuwa box la khaki au jeupe

Mara ooh this and that.

Pole boss
Rudisha dukani
Warrant bado unayo.

Humu sisi wote maboss tunatumia Samsung Curved 😂😂
Mambo za kichina hatujui
 
Stabalizer unayo !
alafu sab ufa yako ni ya kichina ! maana kesi za sab ufa za kichina zinatabia ya kurudisha umeme kwenye njia ya kupokea sauti kwa waya
 
Wiki 2,warudishie dukani kaka, ila kuepusha usumbufu test fuse kwanza kitendo cha dk 2 tu.
 
Stabalizer unayo !
alafu sab ufa yako ni ya kichina ! maana kesi za sab ufa za kichina zinatabia ya kurudisha umeme kwenye njia ya kupokea sauti kwa waya
😂😂 kwamba na mie iko siku vitaniamkia?
 
Habari wakuu . Naomba ushauri wenu majuzi kati nilipata vijesent vyangu nikanunua tv ya hisense sasa nimetumia wiki mbili tu. Juzi wakati nataka kuunganisha na subwoofer nashika wire naona tv imezima ghafla nikajaribu kila njia naona haiwaki sasa wakuu naomba ushauri wenu nifanyaje.
Kama hiyo cable yake ina fuse ibadilishe, isipowaka km ulipatiwa warranty nenda kabasilishe nyingine.
 
Sawa wakuu nimesha irudisha dukani nasubiri wanipe majibu kama watabadilsha au laa
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom