Ngomile
Member
- Mar 18, 2018
- 18
- 14
Wakuu habari za majukumu!! Niende moja kwa moja kwenye Mada.
Ninaomba ushauri nini natakiwa kufanya kuhusu hili suala langu.
Mimi ni mwajiriwa serikalini kupitia moja ya wizara.
Nilifanya usaili katika taasisi ya umma mwaka huu mwezi wa nane na nikafanikiwa kupata kazi katika taasisi Hiyo.
Hivyo basi niliandika maombi ya kuomba kuhamisha taarifa zangu za Utumishi kwenda kwa muajiri huyo mpya taasisi hiyo ya umma na nikajibiwa kukubaliwa name mwajiri wangukuwa " ombi langu la kusitisha ajira wizara limekubaliwa" na kunielekeza nielekeze maombi yangu menejiment ya Utumishi wa umma kwa hatua zaidi.
Nilielekeza maombi yangu Kama nilivyotakiwa.
Sasa shida ikaja kwenye suala la uelewa wangu kuhusu taratibu hizo ulikuwa potofu, maana baada ya kupata tu barua ya mwajiri kuwa amesitisha ajira nami nikaondoka kituo cha kazi na kwenda kusign mkataba kwenye taasisi hiyo.
Kumbe ilinipasa kungojea mpaka kibali cha uhamisho kinikute kituoni kwangu.
Sasa wakati naendelea kusubiri kibali nikiwa nje ya kituo cha kazi msimamizi wa kituo alituma taarifa kuwa mie mtoro kazini, ila pia ikumbukwe tu kuwa nakala ya barua niliipeleka kwa msimamizi wa kituo na akasign ingawa hakikuwa Kibali uhamisho toka Utumishi.
Barua nilipata tar 31 Oct 2018 na nakala nikapeka ikasiniwa kuwa imepokelewa tar 2 November 2018.
Mwezi huo huo Nov 2018 mshahara ukasimama sikushtuka nikajua ndo labda taratibu za Utumishi kwa kuwa mwajiri amekubali ombi na kusitisha Akira.
Lakini nilipokumbuka kucheck kwenye salary slip baada ya kudownload nikakuta " Stop pay abseetism" hold pay.
Basi nikafuatilia ndo nikajua kuwa sikutakiwa kuondoka mpka kibali.
Nilipofika Wizarani kujieleza wananiambia wamenitoa kwenye Lawson na Hawana cha kunisaidia.
Sasa naomba wajuzi wa mambo mnishauri nifanyeje na ombi Tayari liko Utumishi kuomba uhamisho na wakati huo mshahara ndo hivyo.
Je ndo imekula kwangu jumla ama Vipi?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ninaomba ushauri nini natakiwa kufanya kuhusu hili suala langu.
Mimi ni mwajiriwa serikalini kupitia moja ya wizara.
Nilifanya usaili katika taasisi ya umma mwaka huu mwezi wa nane na nikafanikiwa kupata kazi katika taasisi Hiyo.
Hivyo basi niliandika maombi ya kuomba kuhamisha taarifa zangu za Utumishi kwenda kwa muajiri huyo mpya taasisi hiyo ya umma na nikajibiwa kukubaliwa name mwajiri wangukuwa " ombi langu la kusitisha ajira wizara limekubaliwa" na kunielekeza nielekeze maombi yangu menejiment ya Utumishi wa umma kwa hatua zaidi.
Nilielekeza maombi yangu Kama nilivyotakiwa.
Sasa shida ikaja kwenye suala la uelewa wangu kuhusu taratibu hizo ulikuwa potofu, maana baada ya kupata tu barua ya mwajiri kuwa amesitisha ajira nami nikaondoka kituo cha kazi na kwenda kusign mkataba kwenye taasisi hiyo.
Kumbe ilinipasa kungojea mpaka kibali cha uhamisho kinikute kituoni kwangu.
Sasa wakati naendelea kusubiri kibali nikiwa nje ya kituo cha kazi msimamizi wa kituo alituma taarifa kuwa mie mtoro kazini, ila pia ikumbukwe tu kuwa nakala ya barua niliipeleka kwa msimamizi wa kituo na akasign ingawa hakikuwa Kibali uhamisho toka Utumishi.
Barua nilipata tar 31 Oct 2018 na nakala nikapeka ikasiniwa kuwa imepokelewa tar 2 November 2018.
Mwezi huo huo Nov 2018 mshahara ukasimama sikushtuka nikajua ndo labda taratibu za Utumishi kwa kuwa mwajiri amekubali ombi na kusitisha Akira.
Lakini nilipokumbuka kucheck kwenye salary slip baada ya kudownload nikakuta " Stop pay abseetism" hold pay.
Basi nikafuatilia ndo nikajua kuwa sikutakiwa kuondoka mpka kibali.
Nilipofika Wizarani kujieleza wananiambia wamenitoa kwenye Lawson na Hawana cha kunisaidia.
Sasa naomba wajuzi wa mambo mnishauri nifanyeje na ombi Tayari liko Utumishi kuomba uhamisho na wakati huo mshahara ndo hivyo.
Je ndo imekula kwangu jumla ama Vipi?
Sent using Jamii Forums mobile app