Msaada tafadhali, naachikaje?

Msaada tafadhali, naachikaje?

Mkunde Original

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
807
Reaction score
647
Habari za jumapili waungwana,

Kimya kingi kina mshindo mwingi....... iko hivi nataka kuachika...... sababu nimechoka. (vituko vya pombe)

Vituko vimezidi nimekuwa nikiongea na tunayazungumza na mwenzangu ila anarudia yale yale. Nataka kusonga mbele niendelee na maisha maana kama kulia nimelia sana kama kuvumilia nimevumilia sana.

Msaada wako ni niambie nifanyaje au nitumie njia ipi niachike bila ugomvi bila mimi kuwa na mchepuko bila kumlipizia visa alivonifanyia. Pia sitaki kutoroka nataka nikiachika niondoke na mwanangu na si kuwa baada ya hapo ntaanza mahusiano mapya laah.

Nataka nijitawale mwenyewe nifanye yale nnayotaka na kumpa mwongozo mzuri mwanangu aje kuwa mtu mzuri baadae.Mwenzenu nimechoka nimechoka sitaki cha padri wala askofu wala maongezi ya familia wala kikao cha ukoo.

Naomba nisaidie ikiwezekana January nianze 2016 maisha mapya.

Ubarikiwe kwa maoni yako.
 
Nenda mahakamani ukafungue shauri la kuomba talaka. Ila hakikisha unazo sababu za kuishawishi mahakama kwamba ndoa yako imefikia kiwango ambacho haiweza kurekebishika (irepairable damage). Vinginevyo utapoteza kesi na jamaa atakucheka.

Halafu ukumbuke kuwa mali zote mlizochuma mkiwa wanandoa (zako na zake) mnagawana pasu kwa pasu. Kama uko tayari, basi tafuta wanasheria na keshokutwa shauri linafunguliwa mahakamani!
 
Mkunde Jina lako linaniambia Wewe ni DaDa Yangu kikabila Ingawa Sitaki kuamini Hivyo.

Ingawa Sipo katika ndoa lakini kwa Hili nitajaribu kukushauri kwa Kiasi nijuavyo. Mapenzi au ndoa ni Ya mke na mume na Hata ikitokea mikwaruzano Hukaa na Kuijadili kisha Kutafuta Suluhu na Hatimaye kumaliza Ugomvi.

Kutaka Kujitawala bila kujua Athari Zake ni kukosa Maono Ya Mbele Uendako... Usiongee kwa kuwa upo na uwezo wa Hilo lakini angalia ni Athari Zipi ambazo zitampata mtoto kwa kukosa malezi Ya Baba?

Kusema Kuwa Huna Mchepuko na Wala Hata Ukiachwa Hutaanzisha Uhusiano mpya hapo ni Kujitetea tu lakini watu wenye Akili zetu tunaelewa kuwa yupo ambaye ameshakushika Sikio na Unataka Kuondoka Ili Ukajitawale Kwa Huyo Mtu..

Lakini Kumbuka Thamani ya mtu haipimwi kwa kulipa ovu kwa ovu bali kwa wema..

NDOA NI
UVUMILIVU
KUJALI
KUTHAMINI
KUHESHIMU.

Kuwa Muangalifu Dada Usije kuruka mkojo ukakanyaga Kinyesi.
 
Nenda mahakamani ukafungue shauri la kuomba talaka. Ila hakikisha unazo sababu za kuishawishi mahakama kwamba ndoa yako imefikia kiwango ambacho haiweza kurekebishika (irepairable damage). Vinginevyo utapoteza kesi na jamaa atakucheka.

Halafu ukumbuke kuwa mali zote mlizochuma mkiwa wanandoa (zako na zake) mnagawana pasu kwa pasu. Kama uko tayari, basi tafuta wanasheria na keshokutwa shauri linafunguliwa mahakamani!

Hapo kwenye pasu kwa pasu, mimi hua nakua mpole sana.
 
beba mwanao nenda kwenu ukitaka mambo ya kwenda mahakamani au kuita wazee utashindwa maana inavyoonyesha ujawahi kuwaambia ukweli watu wa kwenu kuhusu matatizo ya mume wako
 
Waonekana tayari. Ushafanya maamuzi Jiondokeee zako tu mwaya huna cha kupoteza hadi hapo,
 
Angalia episodes kadhaa za Snapped: Women who kill, unaweza pata some great ideas. I'm just playing.

On a serious note; kwanini unazungumzia kuachika, na sio kumuacha?
 
Angalia episodes kadhaa za Snapped: Women who kill, unaweza pata some great ideas. I'm just playing.

On a serious note; kwanini unazungumzia kuachika, na sio kumuacha?
Nilishaondokaga kipindi fulani for a week alihaha na kutumia njia zote nikarudi. Nikimuacha najua itakuwa vilevile atanirudisha, note anajeuri ya pesa. Nataka njia ambayo yeye ndo aniambie ondoa nyumbani kwangu au aniambie sikutaka tena au aniambie kuanzia sasa wewe si mke wangu. Means asihangaike kunifata na kutaka nirudi tuishi wote.
Na hii itokee bila mimi kuwa na mahusiano na mwanaume mwingine, Bila kumfanyia visa anavonifanyia wala sitaki tugombane.
Kama ni njia au jinsi iwe moja yaani nikifanya hivo yeye mwenyewe aseme basi ondoka sio nifanye mlolongo wa visa.
Am totally fed up.
 
Nilishaondokaga kipindi fulani for a week alihaha na kutumia njia zote nikarudi. Nikimuacha najua itakuwa vilevile atanirudisha, note anajeuri ya pesa. Nataka njia ambayo yeye ndo aniambie ondoa nyumbani kwangu au aniambie sikutaka tena au aniambie kuanzia sasa wewe si mke wangu. Means asihangaike kunifata na kutaka nirudi tuishi wote.
Na hii itokee bila mimi kuwa na mahusiano na mwanaume mwingine, Bila kumfanyia visa anavonifanyia wala sitaki tugombane.
Kama ni njia au jinsi iwe moja yaani nikifanya hivo yeye mwenyewe aseme basi ondoka sio nifanye mlolongo wa visa.
Am totally fed up.

Basi kama ni Hivyo tafuta mwanaume kisha muingize ndani na ukiona muda wa mr kurudi umewadia mnavua nguo '''''hataka kama sio zote kisha mnakaa sebuleni huku mmepandishiana miguu nadhani hiyo itakua mbinu safi kabisaa
 
Mpikie mihogo wiki moja mfululizo lazima akupige then unapata sababu. Ukiachika usisahau walevi bado wengi huku mtaani
 
Nilishaondokaga kipindi fulani for a week alihaha na kutumia njia zote nikarudi. Nikimuacha najua itakuwa vilevile atanirudisha, note anajeuri ya pesa. Nataka njia ambayo yeye ndo aniambie ondoa nyumbani kwangu au aniambie sikutaka tena au aniambie kuanzia sasa wewe si mke wangu. Means asihangaike kunifata na kutaka nirudi tuishi wote.
Na hii itokee bila mimi kuwa na mahusiano na mwanaume mwingine, Bila kumfanyia visa anavonifanyia wala sitaki tugombane.
Kama ni njia au jinsi iwe moja yaani nikifanya hivo yeye mwenyewe aseme basi ondoka sio nifanye mlolongo wa visa.
Am totally fed up.

Jeuri yake ya pesa inahusika vipi na mahusiano yenu?

Na mtu anakuchoka vipi sasa bila visa?

But anyway, here's the plan. Jaribu kuwa mlokole, unashinda kanisani kila siku. Siku ambazo yuko home, waalike wapendwa mnene zile scripted languages. Akivumilia hayo, baki tu. Good luck.
 
Mungu Ambariki Sana Heaven Sent... Amefanikiwa kuwabadili vijana kutoka kwenye Ukamataji wa Fursa Mpaka Kufikia kulitambua neno na kumjua Mungu. Imani Ya bwana iwe nawe
 
Asante sana nashuhulikia hilo la ulokole
Jeuri yake ya pesa inahusika vipi na mahusiano yenu?

Na mtu anakuchoka vipi sasa bila visa?

But anyway, here's the plan. Jaribu kuwa mlokole, unashinda kanisani kila siku. Siku ambazo yuko home, waalike wapendwa mnene zile scripted languages. Akivumilia hayo, baki tu. Good luck.
 
Hapo kwenye pasu kwa pasu, mimi hua nakua mpole sana.

Ndiyo cost ya uamuzi wenyewe mkuu. Mara nyingi na akina na mama wengi hudhani kwamba mali zinazopigwa panga la 50 kwa 50% ni za mwanamume tu. Ni mali zote zilizochumwa kwenye ndoa na kama mnaweza kudhibitisha pasi na shaka kwamba kweli ni za wanandoa wote au mmoja wao.
 
Nenda mahakamani ukafungue shauri la kuomba talaka. Ila hakikisha unazo sababu za kuishawishi mahakama kwamba ndoa yako imefikia kiwango ambacho haiweza kurekebishika (irepairable damage). Vinginevyo utapoteza kesi na jamaa atakucheka.

Halafu ukumbuke kuwa mali zote mlizochuma mkiwa wanandoa (zako na zake) mnagawana pasu kwa pasu. Kama uko tayari, basi tafuta wanasheria na keshokutwa shauri linafunguliwa mahakamani!

Hahaa huyo ndiye Dark City NA KESHOKUTWA SHAURI LINAFUNGULIWA MAHAKAMANI"
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom