Msaada tafadhali, hebu nishaurini

Liverpool_Jr

JF-Expert Member
Sep 7, 2019
1,220
1,411
Iko hivi

Kifupi nilianza kuajiriwa private nikiwa na Diploma, na kwasababu ya njaa ya kusoma nilitafuta kazi serikalini ili nipate ruhusa ya kusoma (Bachelor na Masters) maana private sector walinibaniaga (nilifanya ofisi 3 tofauti na zote walinibania kusoma).

Nilivyohitimu Masters yangu niliachana na serikali (lengo lilikuwa ni kusomeshwa tu).
Na kwasababu ya kupenda kusoma nilionaga fursa kwenye makala fulani hivi ya biashara, hivyo nilivyoacha kazi serikalini nilijiajiri humo.

Kwasasa biashara ni bora na nzuri. Ashukuriwe Mungu.

Ila tatizo linakuja hapa:

Kifupi napenda sana na kila siku kwenye shughuli zangu nisipokuwa kwenye biashara basi nipo juu ya PC nasoma au namfanyia mtu academic activities (research, business plan, proposal, etc).

Na hata kwenye biashara nikiwa bored huwa nachomoa simu na kuanza kusoma google au vitabu (PDF).

Sasa tokea nihitimu Masters yangu mwaka juzi (MSc. Finance) nimekuwa bado natamani kusoma tena Masters ya Uchumi (MSc. Economics)

Yaani mwaka jana na hasa wiki hii ninavyoona watu wana hitimu Masters zao roho inaniuma balaa.

Nina BSc. Economics & Finance, MSc. Finance na bado natamani MSc. Economics.

Wapo wanaonishauri "niachane na kusoma kwa vile nimejiajiri, Eti kusoma kuna maliza pesa" Huwa nawajibu "Tunatafuta pesa ili kufurahisha moyo"

Wapo wanaosema niende nikasomee nje (Ilaya au USA) ila tatizo nikitoka biashara zangu zitayumba.

Wakanishauri nioe kwanza then nimuachie mke asimamie biashara halafu mimi niende kusoma nje, hili pia hapana maana kwanza, sina mpango wa kuoa leo wala kesho na pia huwa siamini mtu kabisa asimamie biashara zangu.

Sasa wana JF hebu nisaidieni niweze kutoa hii njaa maana huwa inatesa sana.

Moyo unaniuma Masters ya pili naitaka na huku sometimes sielewi.

Aliyepataga njaa kama hii alitumia njia gani aka escape?
 
Mkuu OA.
Utanunua haka kakitabu hapa chini utakua unasoma maisha yako yote.
PS: Hii ni summary (pocket edition) vol I kuna mabaharia wapo volume 12 now.
03636B02-367A-4DC3-B83D-E0DD7535F2EB.jpeg
 
Labda ungetuambia kwanza kwa nini unataka kwenda kuongeza elimu na unatarajia ikusaidie zaidi kwa upande gani? Je huwezi kuajiri mtu mwenye hiyo elimu ? Kwa nini MSC Na sio PhD?
 
Labda ungetuambia kwanza kwa nini unataka kwenda kuongeza elimu na unatarajia ikusaidie zaidi kwa upande gani? Je huwezi kuajiri mtu mwenye hiyo elimu ? Kwa nini MSC Na sio PhD?
PhD ni LAZIMA..
Mpango ni kuwa darasani kabla ya JPM hajatoka madarakani ila pia hii masters NAITAMANI SANAA

#YNWA
 
Soma mkuu kila mtu humu duniani ana kitu anachokipenda wewe upo kama mimi chakula ya ubongo wangu ni mandishi na napenda maeneo ya madarasa au vyuo.

Ili kuufurhisha moyo wako rudi shule
 
haya kasomee urubani sasa hivi,ukimaliza tafuta chuo kinachofundisha ufundi wa meri kapige book mwana wane hainaga kupoa.
MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imesema nchi inakabiliwa na uhaba wa marubani wazawa na wataalam wa mitambo ya ndege.

/https://bit.ly/2sNdnLX
 
Iko hivi

Kifupi nilianza kuajiriwa private nikiwa na Diploma, na kwasababu ya njaa ya kusoma nilitafuta kazi serikalini ili nipate ruhusa ya kusoma (Bachelor na Masters) maana private sector walinibaniaga (nilifanya ofisi 3 tofauti na zote walinibania kusoma).

Nilivyohitimu Masters yangu niliachana na serikali (lengo lilikuwa ni kusomeshwa tu).
Na kwasababu ya kupenda kusoma nilionaga fursa kwenye makala fulani hivi ya biashara, hivyo nilivyoacha kazi serikalini nilijiajiri humo.

Kwasasa biashara ni bora na nzuri. Ashukuriwe Mungu.

Ila tatizo linakuja hapa:

Kifupi napenda sana na kila siku kwenye shughuli zangu nisipokuwa kwenye biashara basi nipo juu ya PC nasoma au namfanyia mtu academic activities (research, business plan, proposal, etc).

Na hata kwenye biashara nikiwa bored huwa nachomoa simu na kuanza kusoma google au vitabu (PDF).

Sasa tokea nihitimu Masters yangu mwaka juzi (MSc. Finance) nimekuwa bado natamani kusoma tena Masters ya Uchumi (MSc. Economics)

Yaani mwaka jana na hasa wiki hii ninavyoona watu wana hitimu Masters zao roho inaniuma balaa.

Nina BSc. Economics & Finance, MSc. Finance na bado natamani MSc. Economics.

Wapo wanaonishauri "niachane na kusoma kwa vile nimejiajiri, Eti kusoma kuna maliza pesa" Huwa nawajibu "Tunatafuta pesa ili kufurahisha moyo"

Wapo wanaosema niende nikasomee nje (Ilaya au USA) ila tatizo nikitoka biashara zangu zitayumba.

Wakanishauri nioe kwanza then nimuachie mke asimamie biashara halafu mimi niende kusoma nje, hili pia hapana maana kwanza, sina mpango wa kuoa leo wala kesho na pia huwa siamini mtu kabisa asimamie biashara zangu.

Sasa wana JF hebu nisaidieni niweze kutoa hii njaa maana huwa inatesa sana.

Moyo unaniuma Masters ya pili naitaka na huku sometimes sielewi.

Aliyepataga njaa kama hii alitumia njia gani aka escape?
Wewe ni mhaya?
 
Back
Top Bottom