Wa-ndugu, kwani JF imegeuka kuwa FB; watu wanataka mambo ya mahusiano tu (mapenzi). Tunaanza kukosa msaada JF, siamini macho yangu. Watu 28 wame-visit hii thread, hakuna msaada wowote. Jamaani tumekuwa hivi....!!!!????
Ngoja mimi nivunje ukimya,
Kutoka Dom mpaka Iringa ni mwendo wa masaa manne kama ni gari binafsi na hamna haraka sana,ni km 250 hivi. Cha maana utakachoona njiani ni nyumba za kiasili za wagogo maeneo ya Chipogolo, baadae utaweza kuliona bwawa la Mtera na kuvuka juu yake. Kwa kipindi hiki kuna uoto wa kijani njia nzima.
Hakuna Hotel kwa kiwango chako,ila unaweza kupata chakula pale stand Mtera, kama mpenzi wa nyama choma utaipata Migori. Barabara ni ya vumbi Dom mpaka Iringa. Kingine utakachoona ni Uwanja wa ndege wa Nduli na shamba la ng`ombe wa maziwa.Ukishavuka Mtera, basi utakuwa uko chini ya himaya ya Lukuvi.
Angalizo, mitaa ya kati hapo usile ovyo,waweza pata tumbo baya ghafla. Karibu Iringa, vipi nikuchagulie mahali salama pa kulala?
Asante Malila; taarifa nzuri sana. Naomba kuuliza, hivi kutoka Iringa mpaka Makambako inaweza kuwa masaa 4, maana nilisafiri hiyo njia muda kidogo. Halafu unaweza kuniambia gharama ya guest house hapo Iringa (Double room).
Ni masaa mawili na nusu mpaka matatu kwa mwendo wa kitalii kama mna gari yenu. Tahadhari Iringa mjini usiku kuna tatizo la misosi baada ya saa nne usiku. Baada ya muda huo itabidi mwende ktk mahotel ya gharama kubwa zaidi, au mkale nyama choma pale Miami, lakini kuna walevi kiasi. Sehemu nzuri ya chakula kwa pale ktkt ya mji ni Staff Inn, wana chakula kizuri au MR Hotel iko karibu na stand ya mabasi.
Gharama za G/House zinategemea jinsi ww ulivyo,labda kama unataka mambo makubwa au ya kawaida. Lakini kwa nyumba nzuri zenye usalama, andaa kt ya 15,000/ mpaka 25,000/ kwa double yenye ukisasa. Iko moja pale karibu na Stand, ina parking ya magari ndani ya fence, kwa sababu hamna haraka, basi pale patawafaa. Pale no totoz, no maji ya mende,na car park ya uhakika kama hupendi makuu.
Mara nyingi tunalala pale kwa sababu ya usafi na usalama.
Hivi Malila pale Babanusa kwa mambo ya misosi si 24/7? Na hiyo nyumba ya kulala wageni unamaanisha MR Hotel? Kusema ukweli jamaa wanajitahidi but hata Kalenga ni nzuri pia but tatizo lao ni parking
Makambako pale nilishiwahi kulala hotel fulani ipo mwanzoni kabisa, baada ya kukata kona ya kwenda Njombe (upande wa kulia). Sijui inaitwa Midland (Sorry, jina limenitoka wadau), huduma zao ni nzuri sana na bei ni reasonable kabisa
Hivi Malila ulishafika pale Miami siku za karibuni? Wale vijana wamejitahidi sana kufanya renovation, na huduma zao ni za kuridhisha mno kwa mtu wa kawaida ila kwa mtu asiyependa ulevi/walevi pale patamkwaza sana. Na pale Babanusa kwa mambo ya misosi si 24/7? Ila kama jamaa wanataka ukisasa zaidi hapatawafaa, kwani watu wa kima cha chini ni wengi sana. Nadhani wakishindwa kote huko waende SAJUS kwa Mama Pindi Chana, pale mpaka saa sita usiku utapata huduma.
Na hiyo nyumba ya kulala wageni unamaanisha MR Hotel? Kusema ukweli jamaa wanajitahidi but hata Kalenga ni nzuri pia but tatizo lao ni parking. Kuhusu Makambako, kuna hotel fulani ipo mwanzoni kabisa, baada ya kukata kona ya kwenda Njombe (upande wa kulia) inaitwa Midland, huduma zao ni nzuri sana na bei ni reasonable kabisa, vilevile kuna Gold Tower upande wa kushoto, ila kama jamaa wanataka ukisasa zaidi waende DURBAN HOTEL ni nzuri sana kwa maeneo yale
Nakubaliana na wewe kwa habari ya Makambako,nilishalala pale siku moja mwaka jana. Kipindi hiki ni kizuri hakuna baridi.Ukifika Njombe mwanzoni kabisa baada ya kupita Polisi, upande wa kulia, nunua NUMBU za kutafuna. Wauzaji wameshaziosha tayari kwa kuliwa.
Mkuu Entrepreneur; Asante sana kwa taarifa nzuri, nitaendelea kuheshimu jukwaa hili. Vipi kuhusu gharama za malazi na hapo inakaribia 15,000/= - 25,000/= kwa double room?. Vipi kuna guest ya bei nafuu zaidi ya hapo na inafaa kwa kulala, maana ukiangalia safari yangu kila mahali nitalala usiku mmoja tu.
Vipi kati ya Iringa na Makambako, kuna kivutio kinginecho zaidi ya zile nguzo za umeme zilizopisha makaburi (nimesahau hilo eneo).
Mkuu Entrepreneur; Asante sana kwa taarifa nzuri, nitaendelea kuheshimu jukwaa hili. Vipi kuhusu gharama za malazi na hapo inakaribia 15,000/= - 25,000/= kwa double room?. Vipi kuna guest ya bei nafuu zaidi ya hapo na inafaa kwa kulala, maana ukiangalia safari yangu kila mahali nitalala usiku mmoja tu.
Vipi kati ya Iringa na Makambako, kuna kivutio kinginecho zaidi ya zile nguzo za umeme zilizopisha makaburi (nimesahau hilo eneo).
Mkuu Malila; unaweza kunisaidia jina la kisayansi la huyo ndege/mnyama, ili niweze ku-google na kupata picha yake.
Pole Mkuu, hicho kivutio cha makaburi na nguzo hutakiona tena kwani makaburi yalihamishwa kupisha upanuzi wa barabara. Na kwa budget hiyo uliyonayo hapo Midland patakuwa muafaka zaidi.
Kivutio kikubwa utakachokutana nacho (Iringa to Makambako) hasa baada ya kutoka Mafinga, ni misitu minene ya miti inayozalisha mabao laini na makaratasi
Huyu si ndege wala mnyama,ni mmea jamii ya beatroot, isipokuwa zenyewe ni nyeupe na zina maji mengi sana, zinalimwa kama carrots. Ukila nyingi kidogo zinafanya meno kugeuka rangi hasa ukila mbichi. Zilizopikwa ni bomba zaidi. Ukiweza kumpata Fidel wa humu jamvini au Next level wanaweza kukupa jina la kisayansi. Mimi huwa nazipiga sana nikifika Njombe,hadi nasahau chakula kingine.
Asanta sana mkuu; natumaini FIDEL au NEXT LEVEL watapita na kutusaidia jina la kisayansi.
Hata kama hutakuwa na muda wa kukaa sana huko,ni vizuri ukijua salamu zao, kuanzia Mtera mpaka Makambako unaweza kutumia neno kamwene kama salaamu kwa ye yote. Ukifika makambako/njombe utakutana na salaamu tofauti tofauti kama vile mapembelo, kamwene,ughonile,nk.
kwa Songea karibu sana mkuu. Ukifika unaweza kulala Top one pale msamala chumba elfu 30 (chukua tahadhali na vitasa vya mlango huwa mara nyingi vimetobolewa katundu for chaboringing). Toka songea mpaka tunduru ni barabara ya vungu na it take 8-10hrs hasa hii masika.
Kwa vivutio songea waweza kwenda ukumbi wa mashujaa ambapo wale majimaji heroes taarifa zao zipo pale.