msaada,sina raha leo

hujaelewa nini?

mwenzio kaumia wakati wa kujisaidia....lol

kula vyakula laini.....na maji mengi

Aaahah!
Kula vyakula vyenye fibers, ambazo huact kama sponji na kufionza maji; hivyo choo huwa laini!

Majani, whole grain meals na matunda! Kwa ushauri zaidi, fuatilia nyuzi za Mzizi Mkavu!
 
Aaahah!
Kula vyakula vyenye fibers, ambazo huact kama sponji na kufionza maji; hivyo choo huwa laini!

Majani, whole grain meals na matunda! Kwa ushauri zaidi, fuatilia nyuzi za Mzizi Mkavu!

ukiumia na wewe uniambie
niku kande kande lol
 
ahh nilisahau...
basi ukihitaji massage ya wowowo...
najua huyo mme mpya hayajui haya...lol
mlokole sana

Eiyer uko wapi? Kuna mtu ananifuatafuata hadi humu dipsensary!

The Boss huoni haya kuchakachua hadi JF Dr? Ka vipi twende ChitChat.
 
Last edited by a moderator:
pole
sasa si itabidi upate mtu wa kutazama kama umepasuka?

hapana The boss, haina haja ya kutafuta mtu wa kuniangalia kwa maana nahisi maumivi it means nimechanika, nafata ushauri wa mdau m1 hapo kuwa nipake mafuta hapo kati na maumivu yakiisha nitakuwa nimepona.
 
Aaahah!
Kula vyakula vyenye fibers, ambazo huact kama sponji na kufionza maji; hivyo choo huwa laini!

Majani, whole grain meals na matunda! Kwa ushauri zaidi, fuatilia nyuzi za Mzizi Mkavu!

kumbe we ni mshauri mzuri, ukielewesha unaelewaga vizuri. asante kwa ushauri Kaunga
 
hapana The boss, haina haja ya kutafuta mtu wa kuniangalia kwa maana nahisi maumivi it means nimechanika, nafata ushauri wa mdau m1 hapo kuwa nipake mafuta hapo kati na maumivu yakiisha nitakuwa nimepona.

kupaka mwenyewe mafuta itakuwa ngumu
bora upate mtu.....
 
habari za siku nyingi wanajamvi. kuna msemo kwamba "kukata gogo ni starehe" nimetumia tafsida kidogo ili nisiwakwaze. leo mwenzenu starehe imegeuka kilio kwani nimetoa chozi wakati nakata gogo kwan lilikuwa gumu mpaka sasa sina amani kunako katkat ya makalio. nahisi kama nimechanika. kama kunywa maji huwa nakunywa sijui kama nitakuwa na tatizo jingine. msaada jf doctors na wadau wote
Mkuu. Nyakwaratony Una Matatizo ya
UKOSEFU WA CHOO KUTOPATA KIRAHISI ( Constipation): Soma tiba rahisi

UKOSEFU wa choo ni tatizo sugu miongoni mwa watu wengi. Bila kujua kuwa ni tatizo ambalo linahitaji tiba ya haraka, watu wengi hupuuzia na kuona siyo tatizo kubwa na ni hali ya kawaida. Ukosefu wa choo wa muda mrefu, huwa ndiyo chanzo cha magonjwa mengine hatari.


Mtu anapokosa choo kikubwa kwa siku kadhaa, uchafu hujikusanya tumboni na unapokosa sehemu ya kutokea hukimbilia kwenye damu na kuingia kwenye mfumo mzima wa damu. Uchafu huo unapoingia kwenye mfumo wa damu huwa sumu na chanzo cha maradhi mengine ambayo hujitokeza baadae na kuanza kumuathiri mtu, bila kujua chanzo chake.


Kwa kawaida mtu unapaswa kupata choo cha uhakika japo mara moja kwa siku, kutegemeana na mlo wake wa kila siku, unapokosa choo kwa siku nzima ili hali una kula milo yote kwa siku, elewa una tatizo katika mfumo wako wa kusaga chakula hivyo unapaswa kuchukua hatua haraka.


MTU MWENYE TATIZO HILI ANA DALILI GANI?
Mtu mwenye tatizo la ukosefu wa choo huwa na dalili kadhaa, ikiwemo kutumia nguvu na muda mwingi wakati wa kujisadia haja kubwa. Pili ulimi wake huwa na utandu mweupe na hutoa harufu mbaya mdomoni. Mtu huyu pia hukosa hamu ya chakula na wakati wote tumbo huwa limejaa.


NINI HUSABABISHA TATIZO?
Tatizo la ukosefu wa choo husababishwa zaidi na ulaji mbaya wa vyakula, kuacha kula matunda na mboga na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku.


NINI KIFANYIKE?
Ili kuondoa tatizo kabla halijawa sugu, fanya moja miongoni mwa haya yafuatayo: Kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi mapema, kisha tembea tembea, baada ya muda utasikia haja ya kwenda chooni. Ili usifanye haraka na upate muda wa kutosha kujiandaa kwenda kazini, amka mapema zaidi. Kula kiasi cha kutosha cha salad ya mboga mboga na juisi ya matunda halisi asubuhi kabla ya kula chochote.


Kila siku kabla ya kwenda kulala, kunywa maji ya uvugu yaliyochanganywa na kijiko kimoja cha asali. Kunywa maji ya uvugu yaliyochanganywa na limau asubuhi na mapema kabla hujala kitu chochote. Kunywa ‘castor Oil’ muda mfupi kabla ya kwenda kulala. Ili kujiepusha kabisa na tatizo la ukosefu wa choo, jenga mazoea ya kunywa maji mengi, kula mboga na matunda kwa wingi kila siku na kuacha kabisa ulaji wa vyakula vilivyoondolewa virutubisho kama vile mikate myeupe, ugali wa unga mweupe, keki vyakula vyenye sukari nyingi na vyakula vingine vitamu.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom