Msaada sina mtoto mpaka sasa

Msaada sina mtoto mpaka sasa

Mi ni mwanaume Mimba zangu zote ninazompa mke wangu zinatoka nahis nimefanyiziwa na mwanamke ambaye nimewahi kutembea nae kabla sijao nifanyeje. mimba 4 zmetoka sielewi au nimelogwa.! NIMEFANYIZIWA MWANAMKE MIMBA ZOTE ZINATOKA USHAURI WAKO
Mwanaume hashiki mimba rafiki, kama mkeo mimba zinatoka usiamini kulogwa mwone daktari
 
Umeenda hospitali mkuu? Nenda kachek tatzo ni nini, kuna mambo ya rhesus factors hapa, kumbuka uchawi ni kama imani, ukiendekeza kichwani utakuwa muumini kabisa, consult the doctor please!

Mkuu uko sahihi kuna jamaa alijua hivyo hivyo kuwa kalogwa alivyonoshirikisha nkamwambia aende kucheck rh-factors kweli tatizo lilikuwa ndio hlo,
 
Mkuu kitu cha kwanza nenda hospital ukachekiwe kuona tatizo nini lakini pia kaeni wewe na mkeo umjichunguze kwa kuuliza wazazi wenu au wazazi wa wazazi wenu kama kuna matambiko/laana za/yaliyofanywa generations nne za nyuma yenu.Hizi zinaweza sababisha hivi vitu.Hili la pili ni kama wewe una amini uwepo wa mungu
 
Daa
Totally confused..!!
its seems na wewe ni muumini wa hayo mambo ndio maana akili yako yote iko huko. Acha kuwa na imani haba, mrudie Mungu wako na mkaonane na daktari kama wengine walivyoshauri
 
kuna wataalamu wakaushauri nakutibu pia...nenda ukamuone mganga wa mambo ya kinamama utapata jibu, ila ujue ikiwa uliwahi kudondosha kienyeji hayo ni miongoni mwa madhara.....
 
Mpeleke hospital wamcheki nahisi mfuko wa mimba umelegea inabidi waukaze uweze kuhimili kubeba kiumbe kisichoropoke
 
Sasa kama ndiyo angekufanyizia usiwe na uwezo hata wa kutia hizo mimba.....mpeleke mkeo kwa wataalam wakachunguze tatizo ni nini.....
 
Kwanini anafikiri huyo mwanamke amekufanyizia? Au kuna kitu kibaya sana uliwahi kufanyia sasa ndo unaunganisha matukio.
 
unajiloga mwenyewe kwa mawazo yako mgando
nenda hispitali
 
Achana na mambo ya uchawi ingawa yapo apa duniani,kwanza nenda hsptl
 

Attachments

  • 1407387447423.jpg
    1407387447423.jpg
    25.3 KB · Views: 152
Sasa kama ndiyo angekufanyizia usiwe na uwezo hata wa kutia hizo mimba.....mpeleke mkeo kwa wataalam wakachunguze tatizo ni nini.....

Mimba zinatiwaje sister?
 
Last edited by a moderator:
Ndo kamshike mguu sasa huyo unayejua kuwa kakuroga, maana akiwazacho mjinga ndicho kinachomtokea. Wewe unamjua vizuri huyo bibie wa kwanza, hawa wachangiaji wengine wanakuletea mambo ya kitabibu na ya kiteknolojia wamesahau mambo ya jadi yapo na yanatokea.

Mind you my dia kuna vitu vingii vipo humu duniani and we don't have a clue of them simply because we are not subjected to those environment au hatujawahi kupata fursa ya kujifunza..Mwanamke wako wa kwanza angekuwa anashiriki ibada na mnyenyekevu kwa mola hata usingepata hizo fikra, wewe unamjua fika ni mtu wa namna gani.

Sasa mtu phonebook yake imejaa namba za waganga wa kienyeji mara wa Sumbawanga,Lushoto,Biti Ndembo afu uache kuwa na hofu nani kasema.Kama haitoshi wanajuaana vizuri.Wewe uliingiia chaka chaguo lako la kwanza.

Na umerogwa kweli hizo mambo za Rh factor ni very rare, hazitokei kabisa ni mmoja kati ya milioni sasa weh una mkosi gani hata ukutane na mambo hayo.Zaidi itakuwa ndumba tu, mfuate bhana oohooo mi nakwambia akiona hujaenda utageuzwa GASHO hapo sasa jamii nzima itakuona Punga kumbe watu wanaku control.
By the way pole sana.
 
Mi ni mwanaume Mimba zangu zote ninazompa mke wangu zinatoka nahis nimefanyiziwa na mwanamke ambaye nimewahi kutembea nae kabla sijao nifanyeje. mimba 4 zmetoka sielewi au nimelogwa.! NIMEFANYIZIWA MWANAMKE MIMBA ZOTE ZINATOKA USHAURI WAKO
Mkuu pole sana, sielewi mazingira uliyopo ila kuna umuhuimu wa kufanyiwa counselling juu ya imani potofu uliyojijengea. Baada ya hayo nendeni hospitali mkafanye check-up juu ya vizazi vyenu wewe na mwenza wako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom