Msaada sina mtoto mpaka sasa

Msaada sina mtoto mpaka sasa

Sagara

Senior Member
Joined
Apr 23, 2014
Posts
101
Reaction score
15
Mi ni mwanaume Mimba zangu zote ninazompa mke wangu zinatoka nahisi nimefanyiziwa na mwanamke ambaye nimewahi kutembea nae kabla sijaoa. Nifanyeje?
Mimba nne zimetoka sielewi au nimelogwa.

USHAURI WAKO.
 
Mi ni mwanaume Mimba zangu zote ninazompa mke wangu zinatoka nahis nimefanyiziwa na mwanamke ambaye nimewahi kutembea nae kabla sijao nifanyeje. mimba 4 zmetoka sielewi au nimelogwa.! NIMEFANYIZIWA MWANAMKE MIMBA ZOTE ZINATOKA USHAURI WAKO

You can't be serious!
 
Mmmnh...... Achana na imani potofu bana..!

Umeshaenda kuonana na Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya wanawake au umekalia kulia lia tuu eti Umefanyiziwa?
 
umewahi kwenda hospital kucheki hilo tatizo lako mkuu au umewaza mambo ya kufanyiziwa tu
 
Nini kimekufanya ufikirie kurogwa...?

Wanaoacha wangekuwa wanarogwa kiwango cha ongezeko la watu Tz kingekuwa chini sana...
 
Unajua zile za kuchimba biti...ukute bidada alimtisha tu sasa yamemkuta ya kumkuta ...anakumbuka alichoambiwa...

hahaa zile za kusema "yaani umefanyia hivi nakwambia tutaona labda sio mimi au nife ila kama niko hai nakwambia tutaona na kiapo huku

jamaa akiunganisha matukio anahisi tayari
 
nendeni hospitali wote wawili mkachunguzwe na wataalam
 
Jipe moyo na mwombe sana mungu na ufunge novena mungu atakusaidia,jaribu maombi husiamini ktk uchawi
 
Mi ni mwanaume Mimba zangu zote ninazompa mke wangu zinatoka nahis nimefanyiziwa na mwanamke ambaye nimewahi kutembea nae kabla sijao nifanyeje. mimba 4 zmetoka sielewi au nimelogwa.! NIMEFANYIZIWA MWANAMKE MIMBA ZOTE ZINATOKA USHAURI WAKO
kuna sababu kadhaa ambazo zinasababisha
  1. muulize mkeo kama alishawahi kutumia njia yoyote ile ya kuzuia mimba kabla hamjaoana
  2. Vipi mnatumia pombe wote wawili? kama jibu ni ndiyo basi mkeo asitumie kabisa kilevi miezi minne ya kwanza baada ya kupata mimba.
  3. Mkeo akiugua kipindi ana mimba asinywe dawa yoyote ile mpaka apate ushauri wa daktari maana kuna dawa zinasababisha mimba kutoka.
  4. Mkeo asinywe kabisa chai ya rangi. majani ya chai yanatoa mimba.
  5. Mkeo mimba anazopata nyingi zinaonekana zinatunga nje ya tumbo la uzazi hivyo kutoka ni rahisi. Mimba hizi nyingi zinaoneka zinatunga kwenye mirija ya Fallopian.
  6. Mkeo yawezekana amewahi kupata magonjwa ya zinaa hasa "Chlamydia" na hivyo kupata kitu inaitwa kitaalamu "Pelvic Inflammatory Diseases" (PID) ambayo inaweza kusababisha mimba kutoka na hata utasa kwa mwanamke ikiwa haitapata tiba kwa muda mwafaka. Ungonjwa huu unatibika hivyo wahi kumwona daktari mapema.
  7. Yawezekana pia kuna "chromosomal abnormalities" hivyo kufanya vipimo husika hospitali vitasaidia kubaini tatizo hilo.
  8. Ukipata matatizo usikimbilie kwa waganga wa kienyeji.
  9. Mwanaume jaribu kula sana mboga zilizoungwa viungo vya asili kama karanga, ufuta na tangawizi kwa wingi.
  10. Acha michepuko
 
Unapaswa wewe na mkeo kwenda hospitali.... mchunguzwe chanzo ni nini
 
bado tatizo limejirudia coz nakumbuka kama ulisha tuma tena huu uzi
 
Nyie ndo mnafanya vibao vya waganga vijae nchini,mpeleke kwa madaktari bingwa kwanza.
 
Nitafute tui solve kwanza hiyo issue kwa njia za kawaida ikishindikana nitakushauri uende huko kwenye magic/black power
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom