Msaada, Simu inawaka na Kuzima, nini tatizo?

Msaada, Simu inawaka na Kuzima, nini tatizo?

Lady Ra

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
886
Reaction score
1,011
Kwema Wanandugu,

Kuna ndugu yangu ana simu yake Samsung toka jana asubuhi inawaka na kuzima tu. Yaani akiwasha inakaa sekunde kama 5 hivi inazima, na kujiwasha tena, kisha after 5sec itajizima tena. Hivyo hivyo mpaka inaisha chaja. Ni simu ambayo huwezi kutoa betri.

Simu hii anasema ina vitu vyake vingi sana vya muhimu ambavyo hataki vipotee kama ataiflash, hivyo anauliza kama kuna njia ingine ya kuitengeneza lakini ikaendelea kua na vitu vyake. Ukiiwasha unaweza kukaa nayo ukafanya chochote lakini after 5sec itazima.

Msaada wataalamu
 
Aina gani ya simu ya samsung.
Je ina warranty?
Ni genuine?
Amewahi kuflash?
Upo mji gani hapa Tanzania?
 
Labda mfanye backup kwanza ya user data kwa kutumia recovery mode au flashing tool..ungetaja na aina ya sim kwanza
 
Aina gani ya simu ya samsung.
Je ina warranty?
Ni genuine?
Amewahi kuflash?
Upo mji gani hapa Tanzania?
Samsung Galaxy Tablet,
Warranty yake itakua imeshaisha,
Ni Genuine Kabisa,
Hajawahi Kui flash,
Yuko hapa hapa Dar
 
Labda mfanye backup kwanza ya user data kwa kutumia recovery mode au flashing tool..ungetaja na aina ya sim kwanza
Inawezekana kufanya backup ya SMS chat?
Ni Samsung Galaxy Tab
 
Jaribu soft reset, shikilia power button na volume down button kwa muda, baadae utapata menu, chagua normal boot kwa kutumia volume up and down. Hii soft reset haiathiri data yoyote.
 
Jaribu soft reset, shikilia power button na volume down button kwa muda, baadae utapata menu, chagua normal boot kwa kutumia volume up and down. Hii soft reset haiathiri data yoyote.
Hapa ndio napopaogopa aisee
 
Kwema Wanandugu,

Kuna ndugu yangu ana simu yake Samsung toka jana asubuhi inawaka na kuzima tu. Yaani akiwasha inakaa sekunde kama 5 hivi inazima, na kujiwasha tena, kisha after 5sec itajizima tena. Hivyo hivyo mpaka inaisha chaja. Ni simu ambayo huwezi kutoa betri.

Simu hii anasema ina vitu vyake vingi sana vya muhimu ambavyo hataki vipotee kama ataiflash, hivyo anauliza kama kuna njia ingine ya kuitengeneza lakini ikaendelea kua na vitu vyake. Ukiiwasha unaweza kukaa nayo ukafanya chochote lakini after 5sec itazima.

Msaada wataalamu
Mwambie aiwashe kwa kubonyeza power botton na volume down. Itawaka vizuri na haitazima tena
 
Mwambie aiwashe kwa kubonyeza power botton na volume down. Itawaka vizuri na haitazima tena
Amefanya hivyo ikamletea menu, amechagua reboot system now.
Imewaka, but still imezima tena
 
Back
Top Bottom