msaada plz nimechoka kukaa kwa ndugu

msaada plz nimechoka kukaa kwa ndugu

bado miaka miwili tu umalize chuo,hold on
 
Hutokea wivu lakin binadamu unatakiwa uishi nae kwa akil sana......ukipanga ratiba yako vizur na ujishughulishe na shughul za nyumbani wataishia poroji tu hapo ndo pakuwabaini.
Yaani katika maisha ya shule haya unatakiwa uwe mvumilivu sana kwa sababu wengi wetu hatukuweza kukaa wa wazazi hasa wakati wa kusoma elimu za juu na vyuo! nakumbuka nikiwa high school nilikaa kwa kakangu/binamu, duh! kama sikuwa mvumilivu basi maisha yasingeenda huyo shemegi yangu alikua noma, akimtia-tia maneno broo ili niondoke pale kaka alishaanza kubadilika lakini shangazi (mamake) alikua makini akamwambia awe na subira tu kwani siku zenyewe chache. Kisa hapa "eti house girl ananipenda mimi zaidi kuliko wao mabosi" yaani nilivumilia wala sikulalamika hata kwa baba yangu (R.I.P) kwa sababu asingeniruhusu kukaa tena pale kwa jinsi alivyokua akinipenda, mama ndio usiseme..
 
Rafiki, maisha ni magumu sana usawa huu. Na kuna elimu ya maisha ambayo haipatikani darasani inapatikana kwa kupata ugumu wa kufika pale unapotaka kwenda... Kwa sasa wewe haka ni kapanya tu ka ugumu katika maisha yako, learn something from it kwa sababu matembo ya matatizo hayajafika bado. Kukimbia sio solution kwa umri mdogo uliokuwa nao. Tafuta wisdom
 
Me mwenyewe nimewai ishi kwa bro kipindi cha nyuma.....sio kwamba wazazi wamekufa hapana wapo tena Dar hapahapa ila bro alinihitaji tu niishi kwake.

Vituko vya huyo wifi mpaka nilikuwa nacheka mwenyewe hapo hom.....ila sasa hiv tunaheshimiana na waliachana kwa mambo yao na bro wangu.

Menu yetu me na msichana wa kazi,ilikuwa majani ya viazi kama matembele tunachuma kwa jiran tunachemsha na chumvi bas na ugali kila siku tukibadili maharagwe.

Bro ana special menu na mkewe na mtoto wao,bro yeye hajui coz anarud late na hata hivyo anajua alichokula yeye ndo sote tumekula hicho hicho.
mathcom anayekunyanyasa anakufundisha maisha nimeamini hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Ukishaonja mtarimbo huwezi tena kuishi kwa ndugu, kapange tu.
 
Itakua umaanza umalaya sio bure,wewe mtoto wa kike ukapange wapi na wapi wakati huna kazi

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
pole saana, mara nyingi ndo inavyokuwa katika familia zetu za ki TZ, kama una uwezo wa kujitegemea baadhi ya vitu nenda kaanze maisha yako coz hapo hutokaa daima lazima ipo siku utaondoka tu so usisubiri matatizo yakuzid. but make sure unamwelewesha vizur Uncle usije ukaondoka akiwa na chuki na wewe coz amekulea na naamini ndo ataendelea kuwa msaada wako, but vipi kuhusu parents wako na ndugu wengine wa kuzaliwa nao kama unao??
 
Kweli lazima kujipanga vilivyo,mjini mambo tight,,,,
 
Nakubaliana na wewe, huyu binti kama alivumilia tangu primary mpaka first year chuo, unashindwa nini kuvumilia kwa miaka miwili au mitatu iliyobaki? Kwa nini asitafute room hostel kama nyumani hakukaliki? \inawezekana kabisa nyumbani kwao pamekuwa pagumu lakini pia inawezekana anatafuta moral support ya kwenda kuishi sehemu anayoiona ina uhuru zaidi wa kufanya mambo yake yasiyo ya kishule. Ni bora avumilie na kukaza kwenye masomo au kama mambo ni magumu zaidi amwombe mjomba wake amtafutie hostel.

Haya mambo ya kupanga chumba kwa mtoto wa kike tena wa first year, kuna madhara makubwa na hasa mjomba atakapokasirishwa na kitendo cha kuhama nyumbani na kuamua kusitisha huduma, anaweza kuishia kujiuza.

Ushauri mzuri, ila huenda uncle naye ameanza kale ka tabia ila ameshindwa kusema wazi wazi hapa, si bora akapange akimbie ufataki?
%%%ANGALIZO%%%
Ni kweli mtoto wa kike kupanga, kuna mambo mengi, achukue uamzi wa busara, hana wazazi? kama wapo aende kwao, kama hamna, akafunge novena kabla ya kuamua.
 
ushadanganyika na kale kajamaa kanachokununulia handout siyo? nahisi unataka ukomae kabla ya umri wako, ni vema ukawa uso mbuzi umalize miaka mbili uliyobakisha then uchungulie huko utakapo mda huu, kinyume na hapo unataka CHINI YA 2.9 GPA nahisi.

Wangu mtizamo tu lakini
 
Ushauri mzuri, ila huenda uncle naye ameanza kale ka tabia ila ameshindwa kusema wazi wazi hapa, si bora akapange akimbie ufataki?
%%%ANGALIZO%%%
Ni kweli mtoto wa kike kupanga, kuna mambo mengi, achukue uamzi wa busara, hana wazazi? kama wapo aende kwao, kama hamna, akafunge novena kabla ya kuamua.

Amesema wazi tatizo si uncle, uncle hana tatizo ila shangazi na ndg wa shangazo ndiyo tatizo ....
Ila kwa uzoefu nilionao na kwa haka ka umri, wengi wa vibinti vikishafika chuo hujiona vimefika na baadhi yao kwa sababu ya kielimu kidogo huanza kiburi nyumbani. Hatuujui ukweli kwa sababu tumesikia maongezi ya upande mmoja ila kuna uwezekano kuwa ka ujeuri, uvivu kwenye kazi au suala la kupata uhuru zaidi wa kufanya mambo yake ndiyo sababu kubwa ya kutafuta moral support ya kuondoka hapo nyumbani!

Ni mtazamo tu!
 
acha upuuzi ww mtt!
Kwani hyo likizo muda gami mpaka ushindwe kuvumilia?
....tulia hapo mpaka umalize chuo,fanya kazi zako nenda chuo huko kapoteze muda,usishinde sn hom
 
mtoa mada ..........nijambo la kuvumilia uweze kumaliza elimu yako kwanza ili uweze kuondoka kwa huyo uncle wako manake maisha ya kupanga kwa msichana sio mazuri kabisa unaweza kujidanganya na hiyo hela ya MKOPO ukadhani inaweza kukufanya uishi kwa kujitegemea ...I can tell you ni kwamba me nimekaa kwa baba mdogo mpaka nimemaliza chuo nikivumilia mambo mengi magumu sana.....kwa maelezo zaidi you can pm me.
 
Habari ya jioni wana jf. Naomba ushauri. Naishi kwa uncle ambaye ni kama baba yangu kanisomesha toka primary mpaka chuo first year namshukuru kwa hilo sana. Nimeishi nae kutoka 2006 mpaka sasa miezi ya likizo. Uncle hana tatizo lakini kuanzia shangazi, ndugu yake shangazi na wasichana wake wa kazi wamenifanya nichoke kabisa kuishi pale. Nimemwambia uncle kuwa maisha ya pale kwake yamenishinda nataka nikaishi sehemu nyingine tofauti na pale. Kanijibu mtoto wa kike haachi wazazi wake na kupanga pia dharau.

dadaangu kuwa mvumilivu kama ulivo vumilia mpaka unafika elimu ya juu, usione watu wanajitegemea wamepanga ukazan maisha n rahis, huku mtaan maisha n ngumu mno dadaangu,,, wacha kabisa mawazo hayo,,, pambana usome mpaka umalize,,, huez amin ukihamia mtaan kuanza maisha ya kujitegemea! matokeo yako shuleni lazma yatashuka tu,,, sababu utawaza masomo, utawaza chakula, utawaza mavazi! utawaza pesa ya matumizi na hapo ndipo utakapo data.

.
 
Siko mbali sana na wadau wengine naona ni vema ukaendelea kukaa hapo kwa mjomba wako. Kama umekaa hapo kwa muda huu wote jiulize kwanini wamebadilika , pengine wewe mwenyewe umechange. Kosa ulilofanya ni hapo ulipomwambia uncle wako kua hapo home pamekushinda hii si lugha nzuri. Ungetaka mjomba wako akubaliane na wewe kwamba mkewe ana tatizo wakati umekaa nao muda huo wote? Kumbuka uvumilivu siku zote unalipa na si vizuri hata kidogo kuwalaumu unaoishi nao hata kama wanakunyanyasa, wewe ni kijana/binti mkubwa sasa . Kumbuka hao si wazazi wako hivyo yakupasa uwavumilie na ujaribu wakati wote kuongea kwa busara na mjomba wako. Hata akiona umenyanyaswa na akakuuliza unaonaje maisha ya nyumbani we sema mazuri tu tena namshuru sana shangazi amekua msaada sana kwangu. Tumia muda wako mwingi chuoni au kwa marafiki zako na bila kusahau kushirikiana na hao wadada wa kazi uwapo home. Kumbuka mtaka cha uvunguni sharti ainame

ni kweli ulichosema, hawa watoto wa ndugu bana inabidi wajifunze kuishi na watu wengine ambao si wazazi wao na wawaheshimu..wengi wao wanakuwa defensive tuu na wanawaheshimu wale ndugu zao wa damu(mfn mjomba) lkn shangazi hana time nae..
na pia unakuta mtu anakaa home hasaidii kabisa kazi za nyumbani eti kisa anasoma, hata sisi si tumesoma? mbona tulikuwa tuna mmuda wa kusaidia vitu vidogo vidogo km kupika, kuosha vyombo japo mara moja moja, na ww unaonekana wa maana, na mtu hata ukiondoka kwake anakumis, lkn hawa wa siku hizi, akirudi home kutoka chuon yeye na fesi buku, au jamii forum, ilimradi yuko na simu au yuko kwenye tv..hasaidii chochote na yeye anahudumiwa na mahouse girl...kwa kweli hiyo ni ngumu sana labda kama ni nyumbani kwenu kwa wazazi wako ndio uko huru lkn ikiwa kwa ndugu unatakiwa ujitume na usiwe mwepes wa kukasirika na vitu vidogo vidogo...

mimi binafsi ni muathirika wa haya matatizo ya ndugu, mtu mzima anatoka shule anakaa kwenye tv hasaidii chochote hapo nyumbani eti kwa sbb tuna dada wa kazi, kwani dad wa kazi ndio hasaidiwi? ni lazima uonyeshe uwepo wako na ww uonekana wa maana na sio unaonekana mzigo...
i tell you hakuna mama anyemchukia mtu mwenye kujituma nyumbani hata kama hapendwi na baba huyo atakaa tu, lkn ukijidai mjuaji na kutumia muda wako vizuri kwenye fesibuku na tv basi mama mwenye nyumba atakuchukia tu
 
-Kila nyumba ina standards zake ni vyema kutimiza hizo standards na swala si mjomba tuu hata kama ungekuwa unakaa na rafiki yako ni haya haya tuu
-sasa ni muhimu usubiri mpaka umalize na kupata kazi kisha uwashukuru na kuangalia kujitegemea katika misingi inayompendeza MUNGU
-pia angalia inawezekana wao hawaja change ila wewe ndio una change miaka yote ilikuwa safi umeingia chuo unataka kufuata tabia za mtoto wa waziri, kupanga sio lele mama unasahau kwamba unanunua chakula,unalipa bili, na ukizidiwa hauwezi kurudi ulipotoka kwa hiyo kuwa makini mwanangu
 
Unajidanganya na visenti vya kuhongwa,
Jaribu ukapange kama utawaona.

Hapo tu hujapata hata kazi unaleta mapozi
ungekuwa na kazi je; acha uvivu.
 
Back
Top Bottom