msaada plz nimechoka kukaa kwa ndugu

msaada plz nimechoka kukaa kwa ndugu

Dada naona unataka uhuru wako vumilia umalize chuo upate uhuru wa kweli uondoke kwa mjomba ako ukiwa umeacha furaha na heshima itakusaidia katika maisha
 
ni kweli ulichosema, hawa watoto wa ndugu bana inabidi wajifunze kuishi na watu wengine ambao si wazazi wao na wawaheshimu..wengi wao wanakuwa defensive tuu na wanawaheshimu wale ndugu zao wa damu(mfn mjomba) lkn shangazi hana time nae..
na pia unakuta mtu anakaa home hasaidii kabisa kazi za nyumbani eti kisa anasoma, hata sisi si tumesoma? mbona tulikuwa tuna mmuda wa kusaidia vitu vidogo vidogo km kupika, kuosha vyombo japo mara moja moja, na ww unaonekana wa maana, na mtu hata ukiondoka kwake anakumis, lkn hawa wa siku hizi, akirudi home kutoka chuon yeye na fesi buku, au jamii forum, ilimradi yuko na simu au yuko kwenye tv..hasaidii chochote na yeye anahudumiwa na mahouse girl...kwa kweli hiyo ni ngumu sana labda kama ni nyumbani kwenu kwa wazazi wako ndio uko huru lkn ikiwa kwa ndugu unatakiwa ujitume na usiwe mwepes wa kukasirika na vitu vidogo vidogo...

mimi binafsi ni muathirika wa haya matatizo ya ndugu, mtu mzima anatoka shule anakaa kwenye tv hasaidii chochote hapo nyumbani eti kwa sbb tuna dada wa kazi, kwani dad wa kazi ndio hasaidiwi? ni lazima uonyeshe uwepo wako na ww uonekana wa maana na sio unaonekana mzigo...
i tell you hakuna mama anyemchukia mtu mwenye kujituma nyumbani hata kama hapendwi na baba huyo atakaa tu, lkn ukijidai mjuaji na kutumia muda wako vizuri kwenye fesibuku na tv basi mama mwenye nyumba atakuchukia tu
Unachosema ni kweli kabisa tatizo watoto wa siku hizi hawana uvumilivu. Hakuna mama atakaekuchukia kama unatimiza wajibu wako. Inawezekana kukawa na tatizo upande wa shangazi lkn huna budi kunyenyekea tu . Nimeishi na mabinti wengi nyumbani kwangu yaani ni shida tu wanataka hadi dada awahudumie. Walikua radhi wakitoka shule wanaingia vyumbani mwao wanalala na kujifanya wanasoma. Kiukweli sitaki tena kuishi na ndugu mwisho wa siku wana lawama nyingi halafu mbaya zaidi hata wazazi wakati mwingine huwa hawatumii hekima huungana na watoto wao kukuumiza kinafsi. Hebu ona kama huyu anamwambia mjomba hapa nyumbani pamenishinda, hii si lugha nzuri.
 
Unachosema ni kweli kabisa tatizo watoto wa siku hizi hawana uvumilivu. Hakuna mama atakaekuchukia kama unatimiza wajibu wako. Inawezekana kukawa na tatizo upande wa shangazi lkn huna budi kunyenyekea tu . Nimeishi na mabinti wengi nyumbani kwangu yaani ni shida tu wanataka hadi dada awahudumie. Walikua radhi wakitoka shule wanaingia vyumbani mwao wanalala na kujifanya wanasoma. Kiukweli sitaki tena kuishi na ndugu mwisho wa siku wana lawama nyingi halafu mbaya zaidi hata wazazi wakati mwingine huwa hawatumii hekima huungana na watoto wao kukuumiza kinafsi. Hebu ona kama huyu anamwambia mjomba hapa nyumbani pamenishinda, hii si lugha nzuri.


uzuri na yeye ni mtt wa kike ataolewa na watakuja ndugu kama yeye alivyoenda kwa mjomba....atajionea mwenyewe jinsi alivyokuwa kero/mzigo kwa shangazi yake ndio ataona ni jinsi gani shangazi yake alimvumilia...

waliosema ndugu lawama hawajakosea kabisa,..kuishi na ndugu halafu aje kukushukuru ni wachache sana wengi wao wanaishia kulalama tu, hawana jema...hata mimi wamenichosha kwa kweli ni bora kuwasaidia huko huko waliko kuliko kuwaleta home manake mwisho wa siku wanageuka mwiba kwenye ndoa yenu na mahusiano yenu na ndugu wengine yanakuwa sio mazuri kutokana na maneno maneno..
 
Back
Top Bottom