Msaada, nimueleze kaka juu ya tabia hii ya mkewe?

Msaada, nimueleze kaka juu ya tabia hii ya mkewe?

mwayungi

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2017
Posts
1,814
Reaction score
3,081
Wakubwa poleni na majukumu baada ya hapo naomba niende moja kwa moja kwenye maada yangu mimi ni kijana wa umri wa miaka 19.

Kaka yangu alioa miaka 3 iliyopita. Kaka huwa ananiomba niende kumsaidia kusimamia shughuli zake lakini cha kusikitisha mke wa kaka yangu ananihitaji kimapenzi kwa muda wa miaka 2 sasa.

Nimekuwa nikijitahidi kumkwepa na kumpotezea. Sasa nimemalza shule kaka anataka tukaishi wote kwake ili kumsaidia kusimamia shughuli zake lakini nasita sana kwenda sababu ya shemeji na kaka ndiye ninayemtegemea.

Je wadau nimueleze kaka juu ya tabia ya mkewe? Maana sipendi hao watu wagombane.
 
Mkuu wasiwas wangu ni kwamba naweza kumueleza ukweli baadae kaka akapatana na mkewe bifu likabak kwangu
Sasa mkuu utafanyaje, ni bora kuwa muwazi inasaidia..shem mkatie mazoea hayo ya kimapenzimapenzi..mazoea ya kawaida ndio yawepo tu...Ukianza kuchanganya mapenzi na kazi utaharibu ufanisi wa kazi...Kuwa na msimamo huohuo..Japokuwa shem atakuchukia lakini komaa simamia kwenye ukweli...Tamaa muda mwingine sio nzuri masta!
 
Mitihani ya dunia ndo hiyo.

Jaribu kumueleza shemeji yako athari zinazoweza kutokea kaka yako akibaini, msistize sana anaweza kukuelewa akatafta baharia mwingine.

Suala la kumueleza kaka sio zuri, wanaume sometimes wanaweza kuwa dhaifu sana kwa wake zao...ukimwambia kaka yako ni sawa na umempa option ya kuchagua Kati yako na shemeji yako.
 
19yrs...hongera kwa msimamo wako bwana mdogo..fahamu mwanamke wa mtu sumu..wewe jikite kwenye biashara wala usimuonyeshe uko interested....maji yakizidi unga hapo pasua mbarika..
 
Mitihani ya dunia ndo hiyo.

Jaribu kumueleza shemeji yako athari zinazoweza kutokea kaka yako akibaini, msistize sana anaweza kukuelewa akatafta baharia mwingine.

Suala la kumueleza kaka sio zuri, wanaume sometimes wanaweza kuwa dhaifu sana kwa wake zao...ukimwambia kaka yako ni sawa na umempa option ya kuchagua Kati yako na shemeji yako.
Asante sana mkuu ninafanyia kazi ushaur huu
 
Cha kukushauri;dont ever try kumweleza bro. ..lazma mwisho wa cku ataelewana na mkewe alaf we ndo utabaki kuonekana mbaya......just jiweke bize na kaz zako...dont give much of ur time kumzoea mke wa bro xana!!!
 
Hakuna njia nyingine isipokuwa kumueleza mhusika ambaye ni shemeji yako. Mwambie kiume ujinga na ajiheshimu fullstop.
 
Wakubwa poleni na majukumu baada ya hapo naomba niende moja kwa moja kwenye maada yangu mimi ni kijana wa umri wa miaka 19.

Kaka yangu alioa miaka 3 iliyopita.Kaka huwa ananiomba niende kumsaidia kusimamia shughuli zake lakini cha kusikitisha mke wa kaka yangu ananihitaji kimapenz kwa muda wa miaka 2 sasa.

Nimekuwa nikijitahid kumkwepa na kumpotezea.Sasa nimemalza shule kaka anataka tukaishi wote kwake ili kumsaidia kusimamia shughuli zake lakin nasita sana kwenda sababu ya shemej na kaka ndiye ninayemtegemea, je wadau nimueleze kaka juu ya tabia ya mkewe???Maana sipendi hao watu wagombane

Ukimwambia kaka yako , shemejio nae atamwambia kaka yako ulimtaka,
Kaka yako atamwamini zaidi mkewe.
La maana hama Kwa wema kabla timbiri halijafumuka.
 
Mwambie kaka ako halafu umwambie ni siku gani mnaenda kukutana na upange vizuri na huyo shem wako ili kaka ako afumanie badaye isiwe lawama
Wakubwa poleni na majukumu baada ya hapo naomba niende moja kwa moja kwenye maada yangu mimi ni kijana wa umri wa miaka 19.

Kaka yangu alioa miaka 3 iliyopita.Kaka huwa ananiomba niende kumsaidia kusimamia shughuli zake lakini cha kusikitisha mke wa kaka yangu ananihitaji kimapenz kwa muda wa miaka 2 sasa.

Nimekuwa nikijitahid kumkwepa na kumpotezea.Sasa nimemalza shule kaka anataka tukaishi wote kwake ili kumsaidia kusimamia shughuli zake lakin nasita sana kwenda sababu ya shemej na kaka ndiye ninayemtegemea, je wadau nimueleze kaka juu ya tabia ya mkewe???Maana sipendi hao watu wagombane
 
Usikubali kuangushwa na ibilisi. Fahamu kuwa ibilisi huwa anaitumia sana jinsia ya -ke katika kufanikisha mambo yake. Kumbuka kilichotokea katika bustani ya Edeni.

Pia endelea kuwa imara kama alivyokuwa Yusufu alipokuwa akitakwa kimapenzi na mke wa tajiri yake (Potifa.)
 
Back
Top Bottom