Msaada: Nimejifumanisha mwenyewe

Msaada: Nimejifumanisha mwenyewe

Leo usirudi home. Njoo ukae kwangu wiki, ukirudi utakuta soo limeshapoa.
nilipanga niwe narudi usiku sana kwa siku wiki hii halaf asubuhi nasepa sababu wenyewe wanajua naenda kazini... ila halitawekwa kipolo kweli siku kama wikiend likaamshwa kesi upya..!!!
 
sawa hilo nakubaliana nalo ila linahitaji umakini sana sababu sijawahi kugusa mkuu na nikijichanganya watanishtukia maana pombe ina vituko vyake vya ukweli...!!!
Fanya kama alivyokwambia mkuu hapo juu, yani ulikua na stress then ukakubidi ule monde kupunguza mawazo. Wakizingua sentensi yako ya mwisho iwe waamini au wasiamini ni juu yao ila huo ndio ukweli. Unamaliza kwa kusema shithole afu unatambaa ukiwa unadunda kama tozi nyangema...
 
Kama nilivyokwambia, huo ndo ushauri wangu.

Unachotakiwa kukifanya, soma yote unayoambiwa humu, yatafakari, chagua unachoona ni sahihi.

Mwisho wa siku hii ni issue yako, sisi ni third pary tu.
yaan mkuu nawashukuru sana ila kusema ukweli nahisi ndo nitaharibu kabisa sababu binti pia ataonekana mhuni...ni bora kukataa au kuwa na njia nyingine nje na ukweli..!!!
 
Fanya kama alivyokwambia mkuu hapo juu, yani ulikua na stress then ukakubidi ule monde kupunguza mawazo. Wakizingua sentensi yako ya mwisho iwe waamini au wasiamini ni juu yao ila huo ndio ukweli. Unamaliza kwa kusema shithole afu unatambaa ukiwa unadunda kama tozi nyangema...
yaan hapo ulipomalizia umenifanya nicheke sana.... watajua huyu jamaa inawezekana na bange anavuta..!!!
 
Jifanye tu ulikuwa na usingizi na kilevi kichwani, baada ya kikao ulete mrejesho.
enheeee nishapata akili kwani nikiwaambia hivyo wakanikomalia kwangu kuna hasara gani si nishasema sababu eti...!!!
 
Du Pole sana mkuu kwa janga hilo usiogope ww ni Boy yataisha tu
kuisha najua yataisha mkuu ila yaishe vizuri sasa maana kuna kuisha vibaya mwisho nionekane sina maana.. nipeni akili ya kujikwamua kwenye kikao yule shangazi kamaindi sana anapiga piga simu ovyo tu kwa ndugu zake sijui alijua nataka kumbaka..!!!
 
Sasa wakijua unakula na ganja ndio wataamini kabisa kwamba bange zilimfanya akapotea mlango
mkuu hii kesi imenikalia kushoto aisee... hv haiwezi kuniletea shida kweli maana hadi wanaitwa wazee wenye heshima zao si tayari msala huu...!!!
 
mkuu hii kesi imenikalia kushoto aisee... hv haiwezi kuniletea shida kweli maana hadi wanaitwa wazee wenye heshima zao si tayari msala huu...!!!
Sio kesi hiyo ni kitu kidogo sana hicho, shikilia msimamo wako usikubali kupelekwa hovyo.
 
Ataanza kukuvizia ukimshinda apo nzuri ya tungi
ngoja niseme nilipiga tungi kimtindo tukishindwana basi... ninachojiuliza yeye ananiwazia nini sababu vitu vingine vinaongeleka sema kujichetua tu...!!!
 
Point iko hapo, ilitokea ulikuwa na msongo wa mawazo ukashauriwa kunywa, sasa ulipotoka chooni ukajikuta umekosea chumba. Na hii imetokea kuchanganywa na pombe kwa sababu ni mara yako ya kwanza kunywa.

Nunua na chupa ya konyagi kubwa, imwage nusu ili ukiulizwa ushahidi uoyeshe kiasi kilichobaki.
Mkuu usiimwage niite nije niipige nusu tu ndio uitumie
 
Point iko hapo, ilitokea ulikuwa na msongo wa mawazo ukashauriwa kunywa, sasa ulipotoka chooni ukajikuta umekosea chumba. Na hii imetokea kuchanganywa na pombe kwa sababu ni mara yako ya kwanza kunywa.

Nunua na chupa ya konyagi kubwa, imwage nusu ili ukiulizwa ushahidi uoyeshe kiasi kilichobaki.
Aseme tu ilikua bange!
 
Back
Top Bottom