Msaada Nimegundua Fundi anaweza ua kabisa gari yangu

mzizi1

JF-Expert Member
Oct 9, 2017
255
692
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini
 
shida ilianzia hapo. Hiyo ni oil yenye viscosity kubwa yafaa kuweka katika fuso au magari ya mizigo mikubwa wewe umeweka katika Ractis.

Tafuta ya 5w30 liduimoly, castrol, total au oryx. Hiyo oil mwaga haraka fanya service ya gearbox pia.
Shukran, na piah hapo kwenye gearbox ndo kuna kipengere mafundi hawaelewi kama ni CVT ama sio, Trans code yake ni K411, fundi anasema oil ya kuweka ni ATF T IV
 
fundi kaweka oil 20w-50
Kawaida gari ikija kutoka Japan huwa ishafanyiwa service na sticker yake huwekwa mlango wa dereva mara nyingi gari ndogo huwa 5w-30w.
Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.
kabadilishe oil na filter yake weka 5w-30w.
piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush",
Hapa inahitaji wheel balance.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox
Transmission fluid mara nyingi hubadili ikifika 100,000 mileage sasa kwa maelezo yako ipo 20k. Kwanini unataka ubadili?.

Ushauri wangu change oil na filter tu. Na fanya wheels balance. Suali umeangalia oil ipoje purple color au pink?.
 
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini
Google hiyo engine I e Toyota 1NR engine utapata kila kitu kuanzia oil ya engine Hadi ya gearbox na mazagazaga kibao.
Thank me later.
 
Nilipomiliki gari mara ya kwanza jamaa wa Befoward aliniambia "USIJE UKAAMBIWA UBADILISHE OIL YA GEARBOX, USIIGUSE"

Daah nimetoa gari nje pale nikabana kila kona nikapigwa kwenye tairi

Niliwahi kutumia hiyo oil, aisee nilimwaga kesho yake nikarudia 5W-30
 
Kawaida gari ikija kutoka Japan huwa ishafanyiwa service na sticker yake huwekwa mlango wa dereva mara nyingi gari ndogo huwa 5w-30w.

kabadilishe oil na filter yake weka 5w-30w.

Hapa inahitaji wheel balance.

Transmission fluid mara nyingi hubadili ikifika 100,000 mileage sasa kwa maelezo yako ipo 20k. Kwanini unataka ubadili?.

Ushauri wangu change oil na filter tu. Na fanya wheels balance. Suali umeangalia oil ipoje purple color au pink?.
Ishaanza kuwa nyeusi mkuu, fundi alisema next service yaweza badirishwa
 
Nilipomiliki gari mara ya kwanza jamaa wa Befoward aliniambia "USIJE UKAAMBIWA UBADILISHE OIL YA GEARBOX, USIIGUSE"

Daah nimetoa gari nje pale nikabana kila kona nikapigwa kwenye tairi

Niliwahi kutumia hiyo oil, aisee nilimwaga kesho yake nikarudia 5W-30
Shukran mkuu
 
Sisi mafundi wa mtaani Huwa tunajifunzia ufundi kwenye magari yenu kwahiyo tuvumiliane mkuu usituchoke mkuu kama kuna shida ilete tu tunaweza kukuharibia gari ila mwingine akija hatutaharibu maana tutakua tumejifunza kutokana na makosa
 
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini
Achana na kuambiwa ufanye service ya oil ya gearbox... ukiigusa umeua. Oil nyingi uku afrika ni matatizo
 
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini



Bro i had the same issue na mm, fundi wangu kanitwanga 20w50 kasema hio ndio inafaa ila asee baada ya kusoma na kuchunguza sana nkaona ananiingiza mkenge huyu, soln ni 5w30 , nadhan inabd tufike hatua tuambiane tu ukweli mafundi sahihi wanapatikana wapi maana asee wajuaji huku mtaani ni wengi mno
 
Sometimes mnashindwa vipi hata kugoogle? Engine oil ya fuso unaweka kwenye ractis? Na hao mafundi wa chini ya mwembe unakubali vipi ukuelekeze
upo sahihi. Ila asilimia 80-90 ya mafundi ni longo longo./wapigaji/wababaishaji. Ndio sababu mtu mwingine mwenye uwezo anatumia gari baada ya miaka kama mitatu anauza kuepuka matatizo ya mafundi.
 
Pole sana naona umeingia anga za wapiga ramli, hiyo gari kuahama barabara nenda kafanya wheel alignment!
 
Sisi mafundi wa mtaani Huwa tunajifunzia ufundi kwenye magari yenu kwahiyo tuvumiliane mkuu usituchoke mkuu kama kuna shida ilete tu tunaweza kukuharibia gari ila mwingine akija hatutaharibu maana tutakua tumejifunza kutokana na makosa
halafu ukute gari ya mkopo utapigwa ngumi mpaka ukae chini
 
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini

Kuchelewa kuchanganya mara nyingi ni tatizo la engine yenyewe na si gearbox. Kwanza haishauriwi ku change oil ya gearbox na ili ku change inabidi gari iwe imetembea sana yan karibia km elf 60 huko google utaona hiki kitu na uki change nunua oil ile wanaita hydropress 68 nyeupe hivi . Angalia sana hao mafundi mchundo ndo wanaharibu magari

Ntakupa kisa changu , engine iliwahi nisumbua karibia miezi sita nimebadili sana oil, plug , coil n.k. Baadae nikaanza ku notice brake zinajishika zenyewe hasa nikitembea sana hapo fundi akasema tu change brake master, nika change ila baadae ikarudi. Siku nikaamua ku google nikapata majibu quora kwamba ni hose zinaweza kuwa na leakage, Mwisho nimekuja kutengeneza mwenyewe kwa issue ndogo tu horse ya engine kwenda kwenye brake booster ilikuwa ina leakage ambayo kwa macho huwezi ona ila engine ilikuwa haivuti vizuri toka kwenye master(iliungwa somewhere ). Nikatafuta hose nyingine kipande kwa buku 5 hapo temeke hata si cha hii gari nikakiweka jumapili moja , kuwasha gari imetulia sana na ina compression ya kutosha na ina change gear on time. Mwanzo wakati engine haiwaki vizuri na ina miss miss gear box pia ilikuwa haichange vizuri mpaka kuisikilizia. Nimekuja ku confirm mafundi ndo wanaharibu magari na wengi shule hawataki kwenda.

Kwenye haya matatizo ya magari always start with simple things kabla ya kukimbilia kwenye mambo ya gharama ambayo ndo huwa majibu ya mafundi muda wote.

Kuna jamaa yangu aliambiwa anunue engine mpya baada ya fundi mmoja ku husle siku mbili engine inagoma ku start, kama bahati nilienda kwake nikawakuta mafundi sasa katika kutizama huku na huko tukakuta kwenye camshaft kuna jino linevunjika, huwezi amini ilinunuliwa cam nyingine kwa elf 70 na tatizo likaishia hapo hapo. Kuna Mwingine alishawahi kupeleka hadi engineering tatizo la kuchemsha, kumbe ilikuwa water pump na ilikuja julikana baada ya kutumia ile leakage stopper ya rejeta, ile dawa inauzwa elf sita ila baada ya kuweka kesho yake engine ikawa inapiga kelele sana kuja kuchek kumbe ni water pump ya elf 30 tu na tatizo la kuchemsha hajawahi kulisikia tangia siku hiyo.
 
Wandugu habari zenu naomba msaada maana hapa ndipo lilipochimbuko la ukweli. Nimenunua Ractis new model ikiwa na genuine km (20k) kutoka japan ( certification ya mtu alonunua toka kiwandani nilipewa).

Engine 1NR-FE, sikufanikiwa kupewa user manual
Ilipofika katika kutembelea nikaenda kufanya service ya engine, picha linaanza fundi kaweka oil 20w-50 for high mileage cars (alidai gari km zimechezewa sio halisi, mimi sikumwambia kama nimenunua toka nje). Gari ni nzito na inaunguruma sana ukiwa unaiwasha.

Baada ya hapo akatoa ushauri kuwa gari inachelewa kuchanganya tubadilishe gearbox oil na piah gari inahama sana barabarani ukiachia power steering kwenye high speed hivyo tubadilishe "bush", hapo kwenye gearbox alishauri oil fulani nikapata wasiwasi kidogo, katika kuchake kibati kwenye gari, Trans ina namba hizi K411. Kwa ujuzi wa nyuzi kadhaa hapa JF hii gearbox yake ni CVT. Fundi zaidi ya wawili tofauti walishauri oil ya T- IV ambayo hii ni ATF.

So far kwa madini niliyokwisha kuyapata humu oil inayofaa kwenye hii gari ni 5W-30 na niko kwenye mchakato wa kubadili.
Naombeni msaada hapa kwenye aina ya oil ya gearbox maana nahisi dalili za kuuwa hii gari kabisa nisipokua makini
Kwenye upande wa selection ya oil sioni tatizo la fundi chief. 20w-50 au 5w-30 zote zinafaa kwa matumizi ya gari yako. Uchaguzi wa oil gani kati ya hizo itategemea mazingira gani unatumia gari lako.

Oil ya 20W-50: tuanze na neno 20W. Hii maana yake oil itabaki na ubora wake katika nyuzi joto 20 wakati wa winter mpaka nyuzi joto 50.

Kwaiyo kama gari yako unalitumia katika maeneo yenye joto kali, kama Dar es salaam kipindi cha kiangazi, ambapo nyuzi joto hufikia zaiid ya 35 degree, Hii ndo Oil ya kuweka kwenye gari yako katika kipindi icho.

Oil ya 5W-30: hii maana yake oil inabaki na viscocity yake katika nyuzi joto 5 wakati wa winter, na kumaintain viscocity yake hata nyuzi joto likifika 30.

5w-30 This is the best oil ya magari yanayutumika sehemu zenye baridi kali. Hasa kwa wenzetu uko ulaya, baadhi ya maeneo ya nyanda za juu kusini, arusha au Njombe. Maana yake ni kwamba, hata baridi ikiwa kali, bado engine oil iliyo kwenye gari yako haitaganda, na itafaa kwenye matumizi ya engine yako.

Hizi namba za kwenye oil zina maana kubwa sana, tujitahidi kuzielewa. 20W-50 was the best choice kama unatumia gari yako maeneo yenye joto kali hasa Dar es salaam.

Iyo option uliochagua ya 5W-30 jua la Dar likikomaa kama ilivyokuwa mwezi october...Temperature ikifika above 30 degrees iyo oil itaanza kupoteza ubora wake. Na utatakiwa kuimwaga hata kabla haijamaliza service life yake.
 
Back
Top Bottom