Msaada Nataka kwenda Marekani kutafuta maisha

Msaada Nataka kwenda Marekani kutafuta maisha

Jamani nataka kwenda Marekani kutafuta Maisha nauli ninayo kwa anaejua Prosees za kufika kule na michongo ilivyo amtired Bongo maana sina ndugu yeyote anaekaa ulaya naombeni msaada jamani
Kama umeshindwa maisha TZ utaweza Marekani?usidanganyike na picha za kwenye FB au Insta,muulize Le Mutuz atakwambia,Marekani ipo hapa hapa kaka.Kazi zilizobaki huko labda labda kuviosha vibabu
 
Ni kweli mkuu...watu wengi wanafuata mkumbo...America bila kazi inayoeleweka na papers ni Hell....kuna watanzania wengi sana wanaishi barabarani hawana papers...tatizo la nchi zilizoendelea ni kama unavyosema kila kitu kiko structured hamna loopholes...kwa hiyo no matter how much you earn inaishia kwenye kodi na bills...na kama hauna skills utakoma....msimu huu wa winta kazi ni kuzoa barafu...dola 10 kwa saa...ni kazi ngumu sana unakuwa hoi kabisa
Nawashangaa wanaotaka kwenda Marekani eti kwenda kutafuta kazi,kazi ipi,na una ujuzi gani ambao utakupa ajira?vijana acheni ndoto za mabaharia za kuzamia meli kwenda Ugiriki,maisha yapo Tanzania,ni bidii yako tu,kazi sio lazima uende ofisini asubuhi na jioni hata ukianza kilimo cha mbogamboga mbona unapata cash kibao tu na hakuna cha kulipa kodi,Ulaya au Marekani si lelemama hakuna mambo ya mjomba sijui ulale hadi saa nne asubuhi au ukabom kwa mshikaji,nenda kaka utarudi na jeans mpauko ,na tafadhali usije kuomba uchangiwe nauli ya kurudi Bongo
 
Mkuu piga kazi hapa'hapa alafu huko marekani utakwenda kubadirisha mazingira tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom