Msaada: Nataka kupika mlenda, nitafute vitu gani?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,783
Wasalaam ndugu zangu,
Kuna mboga fulani inaitwa mlenda niliwahi kula zamani kidogo,
inakuwa imelojeka sana. Sasa kutokana na kuisoma namba nataka nijifunze kupika hii kitu ili kubana matumizi. Naomba msaada wa viungo vyake.
Natanguliza Shukrani.
 
Wasalaam ndugu zangu,
Kuna mboga fulani inaitwa mlenda niliwahi kula zamani kidogo,
inakuwa imelojeka sana. Sasa kutokana na kuisoma namba nataka nijifunze kupika hii kitu ili kubana matumizi. Naomba msaada wa viungo vyake.
Natanguliza Shukrani.
Bamia, magadi, chumvi, karanga....

Hivyo ni viungo vyake....


Jinsi ya uandaaji, ukihitaji utajuzwa,
 
Kama ni mlenda wa asili huwa hauna viungo. Tayarisha sufuria (Ila chungu ndio safi zaidi), weka maji vikombe viwili vya chai kisha chota mlenda vijiko vikubwa viwili. Washa jiko na injika sufuria au chungu kwenye jiko. Koroga taratibu huku ukiangalia mabadiliko ya vinavyopikwa. Tia chumvi. Vikichemka sana, ipua.
 
Mlenda upi unaongelea? Upo ule wa asili, upo wa kupika bamia peke yake, upo wa bamia na majani ya maboga au mchicha.
 
Back
Top Bottom