Msaada: Naomba tiba ya maumivu haya

Msaada: Naomba tiba ya maumivu haya

scolastika

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2019
Posts
3,863
Reaction score
5,736
Kuna ndugu yangu ana tatizo yaani ana maumivu makali kuanzia sehemu ya chini ya shingo upande mmoja kuja begani mpaka kwenye mkono(ni sehemu ndogo tu) valianza kusikia maumivu kidogo kama wiki moja akadhani labda analala vibaya lakini kadri siku zinavyokwenda maumivu yakazidi, ikabidi aende hospitali.

Alivyomuona Daktari wa mifupa akampa dawa na akaendelea na mazoezi ya viungo ma massage za kutosha lakini tatizo ni kama linaongezeka yaani maumivu ni makali, mchana usiku ni maumivu tu.

Kwenu wataalamu wa afya je unaweza kuwa ni ugonjwa gani?

Je, afanye nini?
 
Take her to the hospital. JF doctors will waste your time for this going there twice it's not a bad thing you're are still looking for the solution.
 
Mwambie akapime cholesterol.
Inawezekana kiwango cha cholesterol kiko juu.
Amwone dk huenda akaandikiwa dawa za kushusha cholesterol.
 
mpaka nimekuja huku basi mambo sio mazuri,
Take her to the hospital. JF doctors will waste your time for this going there twice it's not a bad thing you're are still looking for the solution.
ahsante
Mwambie akapime cholesterol.
Onawezekana kiwango cha cholesterol kiko juu.
Amwone dk huenda akaandikiwa dawa za kushusha cholesterol
mpaka nimeamua kuja hapa mambo yashachanganya maana daktari bingwa ametoa yake,na wengine mambo yashakuwa mengi kwakweli
Mwambie akapime cholesterol.
Onawezekana kiwango cha cholesterol kiko juu.
Amwone dk huenda akaandikiwa dawa za kushusha cholesterol.
nashukuru mkuu
 
Maumivu yanaishia wapi ?

Ukifanya Nini maumivu yanaongezeka zaidi na Nini ukifanya maumivu yanapungua?

Kuna kipimo chochote ukifanya ?

Je huyo daktari alikwambia tatizo ni Nini au alikuandikia dawa pasipo wewe kujua tatizo lako ?
ahsante mkuu,maumivu yanakuja bila kufanya chochote ni automatic
kuhusu vipimo hakufanya kipimo chochote
kuhusu tatizo daktari alimwambia ni misuli imesinyaa akampa dawa za folic acid na ya kuchua na pia kumwelekeza chumba cha physiothelapy,anasiku tano tangu afanyiwe huduma hiyo ila tatizo linazidi
 
Huo ugonjwa upon na huenda unaambukizwa kwa njia ya hewa kutoka mtu kwenda mtu.

Dawa zote za kutuliza maumivu kama volini, fastum gel hazisaidii

Kwa sasa unaweza kupunguza maumivu hayo kwa kukanda sehemu husika kwa maji ya moto na kuogea maji ya moto asubuhi na jioni.
 
Ndio anapatiwa matibabu ila haoni maendeleo yoyote tatizo linazidi
akapime magonjwa ya moyo, hiyo ni dalili za angina na akichelewa inaweza ikampelekea kupata stroke huo upande anaopata maumivuu.

mkuu, usizembee ushauri huu.
 
Misuli imesinyaa !!!! Sidhani


Kwenye issue ya Maumivu labda hujanielewa
Yani yanauma mda wote ( yapo constant)
Au Yana badilika labda ukikunja shingo kuelekea mbele, nyuma, kulia au kushoto
maumivu kuna mda yanatulia ni mda kidogo sana kama lisaa lizima then yanaendelea yaani tuseme yapo costant
 
Huo ugonjwa upon na huenda unaambukizwa kwa njia ya hewa kutoka mtu kwenda mtu.

Dawa zote za kutuliza maumivu kama volini, fastum gel hazisaidii

Kwa sasa unaweza kupunguza maumivu hayo kwa kukanda sehemu husika kwa maji ya moto na kuogea maji ya moto asubuhi na jioni.
asante mkuu ntamwambia aendelee na zoezi la kukanda
 
Huo ugonjwa upon na huenda unaambukizwa kwa njia ya hewa kutoka mtu kwenda mtu.

Dawa zote za kutuliza maumivu kama volini, fastum gel hazisaidii

Kwa sasa unaweza kupunguza maumivu hayo kwa kukanda sehemu husika kwa maji ya moto na kuogea maji ya moto asubuhi na jioni.
kwa hiyo suluhisho ni maji tu na je unaitwaje?
 
akapime magonjwa ya moyo, hiyo ni dalili za angina na akichelewa inaweza ikampelekea kupata stroke huo upande anaopata maumivuu.

mkuu, usizembee ushauri huu.
ahsante mkuu ntafikisha ujumbe
 
Fuata Ushauri wa wataalamu
Huu ugonjwa ni mpya na hao wataalamu hawaujui.
Matibabu wanayotoa ni ya kubahatisha kwani maumivu badala ya kupungua au kuisha, yanaongezeka
Kukanda kwa maji ya moto kwa maoni yangu ndiyo tiba nafuu na sahihi kwa sasa.
Mimi ni muadhirika wa huo ugonjwa na siyo daktari
 
Back
Top Bottom