Msaada Namtafuta baba yangu

Msaada Namtafuta baba yangu

salichuma

Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
29
Reaction score
29
Habari wana JamiiForum, naitwa Christina umri miaka 28. Namtafuta baba yangu mzazi kwani toka nimezaliwa sijawahi kumuona zaidi ya kuambiwa alipokuwa akiishi na mama yangu alishafariki lakini kabla ya kufariki nikiwa na miaka 12 alinambia kwamba baba yangu alimpa ujauzito wakati akiwa anafanya kazi kama house girl mtaa wa Keko Machungwa kwenye kota na majina sina hakika ila kumbukumbu zangu alinitajia kuwa ni Nyalusi Kikoti. Naomba kwa yeyote ambae atakuwa anafahamiana au anaweza kuniunganisha nae anisaidie kwani haja yangu kubwa ni kumfahamu baba yangu na si vinginevyo. Kwa mawasiliano kuhusiana na jambo hili namba yangu ni 0758905911 hii namba inapatikana whatsapp tu. Mungu awabariki
 
Hii inanikumbusha dogo mmoja aliwahi kuwauliza ndg wa mama yake alipo baba yake. Ndg wa mama wakaona labda ni kwa sababu ya ugumu wa maisha kijijini, wakaamua kumpeleka mjini.
Huku mjini walimpeleka shule. Huko shuleni alikutana na kijana wakawa marafiki na hivyo akawa anaenda nae kwao. Siku moja walimkuta mama wa rafiki yake, akawa anamwangalia sana yule kijana. Hatimaye alimuuliza jina lake na asili ya baba na mama yake. Dogo akaeleza asili ya mama yake na jina lake ila baba alisema hamjui hana historia yoyote juu ya baba.
Mama wa rafiki yake aliposikia jina la mama wa dogo, akajua dogo ni motto wa kaka yake, kwani alimpa mimba mwanafunzi akiwa kidato cha pili miaka ya 1988 na hasa jinsi dogo alivyokuwa anafanana na kaka yake.
Kwa mtindo huo dogo aliweza kukutana na baba yake.
Mungu huwa akipanga jambo, litawezekana, hivyo nawe jitahidi utampata baba siku moja
 
Tuma kwenye magrupu ya wosapu utampata tu. Wanapatikana watoto waliopotea sembuse mtu mzima ambaye hajapotea
 
Pole sana ,wababa mliowajiri house girl msiwatie mimba hawa house girl mkawatelekeza
 
Habari wana JamiiForum, naitwa Christina umri miaka 28. Namtafuta baba yangu mzazi kwani toka nimezaliwa sijawahi kumuona zaidi ya kuambiwa alipokuwa akiishi na mama yangu alishafariki lakini kabla ya kufariki nikiwa na miaka 12 alinambia kwamba baba yangu alimpa ujauzito wakati akiwa anafanya kazi kama house girl mtaa wa Keko Machungwa kwenye kota na majina sina hakika ila kumbukumbu zangu alinitajia kuwa ni Nyalusi Kikoti. Naomba kwa yeyote ambae atakuwa anafahamiana au anaweza kuniunganisha nae anisaidie kwani haja yangu kubwa ni kumfahamu baba yangu na si vinginevyo. Kwa mawasiliano kuhusiana na jambo hili namba yangu ni 0758905911 hii namba inapatikana whatsapp tu. Mungu awabariki

Kama unaweza kufanya marekebisho madogo, tumia hii post niliyokunukuu, haina haja ya kueleza kwa undani sana mambo mengine. Nakutakia kila la kheri umpate Mzazi. Pole sana
 
Tumia facebook mkuu.. Huko kila mtu utampata..ndugu zangu watatu wamepatana na baba zao kupitia huko. Nenda seach jina itakuja list anza kuwatumia massage mmoja baada ya mwngne. Kama ulifanya hivyo na hukufanikiwa jaribu Instagram pia
 
Mkuu wewe ni mtu wa nyasirori???
Hii inanikumbusha dogo mmoja aliwahi kuwauliza ndg wa mama yake alipo baba yake. Ndg wa mama wakaona labda ni kwa sababu ya ugumu wa maisha kijijini, wakaamua kumpeleka mjini.
Huku mjini walimpeleka shule. Huko shuleni alikutana na kijana wakawa marafiki na hivyo akawa anaenda nae kwao. Siku moja walimkuta mama wa rafiki yake, akawa anamwangalia sana yule kijana. Hatimaye alimuuliza jina lake na asili ya baba na mama yake. Dogo akaeleza asili ya mama yake na jina lake ila baba alisema hamjui hana historia yoyote juu ya baba.
Mama wa rafiki yake aliposikia jina la mama wa dogo, akajua dogo ni motto wa kaka yake, kwani alimpa mimba mwanafunzi akiwa kidato cha pili miaka ya 1988 na hasa jinsi dogo alivyokuwa anafanana na kaka yake.
Kwa mtindo huo dogo aliweza kukutana na baba yake.
Mungu huwa akipanga jambo, litawezekana, hivyo nawe jitahidi utampata baba siku moja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom