Msaada Namtafuta baba yangu

Msaada Namtafuta baba yangu

Habari wana JamiiForum, naitwa Christina umri miaka 28. Namtafuta baba yangu mzazi kwani toka nimezaliwa sijawahi kumuona zaidi ya kuambiwa alipokuwa akiishi na mama yangu alishafariki lakini kabla ya kufariki nikiwa na miaka 12 alinambia kwamba baba yangu alimpa ujauzito wakati akiwa anafanya kazi kama house girl mtaa wa Keko Machungwa kwenye kota na majina sina hakika ila kumbukumbu zangu alinitajia kuwa ni Nyalusi Kikoti. Naomba kwa yeyote ambae atakuwa anafahamiana au anaweza kuniunganisha nae anisaidie kwani haja yangu kubwa ni kumfahamu baba yangu na si vinginevyo. Kwa mawasiliano kuhusiana na jambo hili namba yangu ni 0758905911 hii namba inapatikana whatsapp tu. Mungu awabariki
Upatikani nilikuwa nataka nikuunge na ukoo wa kikoti
 
Ukoo wa kikoti heb kujeni hapa muongeze idadi
Pole sanaaa utampata mshua au dingilai au mzee baba
 
Hii inanikumbusha dogo mmoja aliwahi kuwauliza ndg wa mama yake alipo baba yake. Ndg wa mama wakaona labda ni kwa sababu ya ugumu wa maisha kijijini, wakaamua kumpeleka mjini.
Huku mjini walimpeleka shule. Huko shuleni alikutana na kijana wakawa marafiki na hivyo akawa anaenda nae kwao. Siku moja walimkuta mama wa rafiki yake, akawa anamwangalia sana yule kijana. Hatimaye alimuuliza jina lake na asili ya baba na mama yake. Dogo akaeleza asili ya mama yake na jina lake ila baba alisema hamjui hana historia yoyote juu ya baba.
Mama wa rafiki yake aliposikia jina la mama wa dogo, akajua dogo ni motto wa kaka yake, kwani alimpa mimba mwanafunzi akiwa kidato cha pili miaka ya 1988 na hasa jinsi dogo alivyokuwa anafanana na kaka yake.
Kwa mtindo huo dogo aliweza kukutana na baba yake.
Mungu huwa akipanga jambo, litawezekana, hivyo nawe jitahidi utampata baba siku moja
the world is small watu hukutana ...yani acha tu..tena katika hali ya ajabu ajabu tu hukuitarajia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom