Msaada, nahitaji kujua lugha ya mume wangu

Msaada, nahitaji kujua lugha ya mume wangu

Khaaa tena wewe na kina mwallu mkianza kunichakachua mnanichakachua haswaa...



Hahahaaaaaa

Unawasingizia tu hao! Mbona mi Na wewe tunaongea sn kigamboshi?!!
 
Last edited by a moderator:
Habari zenu jamani,mimi ni mwanamke mwenye watoto 3 na mume wa ndoa!ndoa yetu namshukuru Mungu anatusaidia tunaishi vizuri kwa maelewano!
Shida yangu ni kuwa mume wangu ni kabila tofauti na mimi,sasa yeye anapenda kweli kuongea kilugha na ndugu zake either kwa simu au hata wakija nyumbani kutusalimia!yeye haoni kama ni shida na nalielewa hilo,tatizo ni kwamba wakati mwingine natamani kusikia wanachokiongea ila ndo hivyo nashindwa.Kumuambia nahisi kama namnyima raha.
Ninachoomba ni msaada wa jinsi ya kumuapproach kumweleza natamani na mimi nichangie katika maongezi bila yeye kufikiri vibaya maana ni mtu anapenda kuongea sana kikwao yani.

Prax ukipenda jifunze lugha ya mumeo upanue wigo, hilo la kuongea kiluga na nduguze lisikusumbue fanya yako, wakipenda kukushirikisha watakusemesha kwa lugha ambayo unaielewa.
 
Hivi tulikubalianaaje kuhusu stalking me? Paw simuachi miaka laki 8, na nduguze wakija nawapa juisi washushie kilugha wakati nawapikia chakula cha kwao. Tafuta kichaka ufyeke, ukiona matuta ujue ni bustani ya wenyewe. Muone kwanza!
Kwa maana hiyo mimi nimekuwa kama fisi amfuataye binadamu anayetembea akitegemea atadondosha mkono ili auchukue? Haya bwana, siku paw akikumwaga ukija kwangu hutanipata tena! Na hivi jamaa anavyopenda dogo dogo!? Utaisoma namba si muda mrefu!
 
Inaonekana mmbea sana we mdada uchangie nini, yangekuhusu si wangeongea lugha unayojua? Kwani wakiongea hivyo mwishowe tatizo linakuwa nini? Jifunze hiyo lugha kama unataka sana kujua wanaongea nini.
 
Pole ndugu kwa fikra mbaya uliyonayo, acha wasiwasi hawakusemi, mboni una mashaka hivyo. Wakati unaolewa si ulijua ni kabila hilo na lugha yake ni hiyo sasa unataka abadilike ghafla? Lugha aliyokulia mtu ni sawa na ranginya ngozi yake haibadiliki. Ila nakushangaa hadi watoto 3 hujajifunza hata maneno machache ili usitetwe! Jifunze maana umeolewa huko. Wengine wazazi wetu hawajui kiswahili na wakija kusalimia lazima niongee nao kilugha sasa unataka mama mkwe wako atafutiwe mkalimani kwasababu wewe hupendi kilugha? Hapana wakati mwingine inabidi wewe mke ujifunze ili ujue uwahudumie vipi. Jiamini usichukie lugha ya watu maana ndo kabila la watoto wako.
 
Mmmhhhh unahisi kusemwa.....huyo mume ni kabila gani na wewe kabila gani??ukitaja kabila itakuwa rahis kushaur maana kuna makabila wakiwa hata ofisin ni lugha ya kwao

ooh kama si mjaluooo
Ber ber
 
ah nilisahau!
Usengwile ni ahsante!
Ukitaka umalize weka hii ,na chilau mewawa!(na kesho tena)wabantu sie atiii!
Kwa mwanamke akigalagala chini ndo daaaaah!
Wenyewe tunasema kugalauka!

mweee mnanikumbusha mbaliiii
kunasiku mwanamama kagalauka nilivyomuona nilistuka nikahisi sijui amepatwa na nini ghafla mwingine chin hee bwana wewee, palinoga penyewe pale lol
 
Mwambie kwa lugha nzuri kuwa unapenda wanavyoongea hivyo ungependa kujifunza maana kwasasa huko ndo kwenu, hakika atakufundisha na wakati wanaongea anaweza kukuuliza Vipi unatupata? Akakutafsiria na maisha yakasonga ila hutowanyima kuongea chakwao, japo Kama hataki usikie basi hatokuwa tayari kukuruhusu ujifunze.

usiwe na shauku saaana kiasi kwamba mpaka itie watu wasiwasi kuwa unahisi kutetwa. Kuwa mvumilivu na mwenye upendo kwa watu wote wala hutokuwa na hofu maana muda wote utahisi amani hata mumeo atakuwa anakuambia walikuwa wanazungumzia nini hata bila wewe kumuuliza maana anatambua umuhimu wako.
 
Wenzio wanajifunza lugha...tena ndani ya muda mfupi lol...
ingawa si kwa lengo la ku spy...

wanasema ni malovedave eti...
 
Wenzio wanajifunza lugha...tena ndani ya muda mfupi lol...
ingawa si kwa lengo la ku spy...

wanasema ni malovedave eti...


Nina mjomba wangu alioa mzungu
mzungu so fast akajifunza kiswahili
tukafikiri anatupenda sana waswahili kumbee alikuwa na lengo

barua zote za kulilia shida za kumuomba mjomba atume dollars mzungu anazisoma zote
na ni full unoko kwenye kutuma tuma pesa ovyo haha haaa

ukoo wacha wamlaani mzungu .....
 
aaahhh...hao wazungu ndio noma kwenye lugha...

Tena wanaweza ku pretend hawajuhi...

Kuna mtu alinisimulia alivyoumbuka baada ya kumteta mzungu kumbe anawasikiliza mwanzo mwisho...kasubiri wamalize ndio kawalipua...

Yani ujifanye kuongea kiswahili eti hakuna anayenisikia...imekula kwako...
Nina mjomba wangu alioa mzungu
mzungu so fast akajifunza kiswahili
tukafikiri anatupenda sana waswahili kumbee alikuwa na lengo

barua zote za kulilia shida za kumuomba mjomba atume dollars mzungu anazisoma zote
na ni full unoko kwenye kutuma tuma pesa ovyo haha haaa

ukoo wacha wamlaani mzungu .....
 
huyo mume atakuwa mhaya au msukuma, ndo wanapenda sana kuongea lugha zao. anyway, sio ishu sana. jifunze lugha ya mmeo mambo yaende sawa.
 
ulikuwa wapi mpaka mnazaa watoto watatu hata kujifunza kusalimia tu?
 
Back
Top Bottom