Natumai ulimaanisha kumuathiri.
Jibu ni ndio, anaweza kuathirika kisaikolojia na hata kimwili kwani anaweza kuiga mambo yanayofanywa na vikatuni akajiumiza au kuumiza wenzake.
Kila kitu kina limit zake. Anza kumbadilishia utaratibu, awe na wakati maalum wa kutazama katuni, nzuri zaidi ni zile zenye kufundisha. Awe na muda wa kusoma, hii unaanza kumzowesha kwa wewe kumsomea vitabu vyenye hadithi za kitoto zenye mafunzo, kumbuka, siyo kumhadithia, kumsomea. Awe na wakati wa kucheza, awe na wakati wa kupumzika.
Na
Pole sana mkuu. Huyo mtoto wako ni photocopy ya mtoto wangu. Yeye ana miaka 4, anasoma chekechea. Tabia zake ni photocopy ya hizo za mtoto wako. Na bahati mbaya hata TANESCO wakikata umeme, yeye haelewi--ni kilio tu akitaka TV iwashwe aendelee kutazama katuni. Kama ni kuathirika kwa katuni, basi huyu wa kwangu ndiye atakayeathirika zaidi. Tatizo ni kwamba hata umeme ukikatika bado ni shida--dada hawezi kumdhibiti kwani ni mtundu sana. Akikaa kwenye katuni siku nzima inakuwa ni nafuu kwa upande wa kumdhibiti lakini nadhani katuni hizi zitamharibu. Msaada tafadhali wadau. Watoto kama hawa dawa yao ya kuacha ulevi wa katuni ni ipi. Let us share the experience among one another.
kushauri google "child rearing" utapata kujifunza mengi, kuna kila aina ya mafunzo kuhusu kulea mtoto vyema.
Kama ana bibi, shangazi au ahli zake wako shamba (kijijini) mpeleke akakae nao kwa muda wa miezi miwili au mitatu atabadilika.