Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

Mkuu hilo suala limekaa kisaikolojia zaidi, binafsi nakushauri kama utapata muda wa ziada mpeleke kwa wataalamu wa saikolojia watakupa ufumbuzi wa maana.

Nami naunga mkono hoja hii. Ni vema kuomba ushauri kwani huenda ni dalili ya maradhi ambayo yakijulikana mapema bi vizuri. Endapo ni hasira za kawaida ( according to wataalam) basi watakushauri ufanye nini kama mzazi kwani hatua nyingine zinaweza zidisha tatizo.
 
Mpeni vitu anavyovihitaji kwa wakati.....hata mimi huwa nauzika nikiwa nataka kitu lakini sikipati kwa wakati......hasa hasa nikiwa na njaa....na ndio ulikuwa ugomvi mkubwa kati yangu mimi na mama.....

Mi mpaka kesho nikiwa na njaa nakuwa na hasira kinoma maelewano yanakua hamna so it's natural. Sio ukorofi Ama jeuri 😄
 
Dah, mimi nina dume langu lina miaka 2 linasumbua kweli mpaka wakati mwingine inabidi nilichape! Lina dada yake ana miaka 4 huwa linamfanyia fujo hadi anabaki analia tu mda wote yaani tabu tupu! Ngoja tuone I hope kadri linavyokua litatulia!

usisubiri uone kama akikua ataacha. Na asipoacha? Samaki mkunje angali mbichi. Watoto hujifunza tabia kwa kuiga na kujaribu. Akijaribu kitu akiona hamna noma anaweka tiki kuwa kinafaa, anaendelea na tabia mpaka inakomaa. Wakati mwingine akijaribu akaona hamjafurahishwa anaacha, kesho anajaribu tena aone kama mta-react kama jana. Msipozingatia kesho anajaribu tena, mkimkoromea anaacha, kesho anajaribu tena, mkinyamaza anaona hamko serious na hicho kitu anaendelea kukifanya. Kuzima tabia mbaya kwa mtoto hata kama ni ndogo si kazi rahisi sana lakini mzazi ukijua madhara ya hiyo tabia utavaa ujasiri. Cha msingi usimuumize. Kama ni mdogo mpe adhabu za kumnyima vitu anavyopenda mara tu anapoleta ugomvi wake. Ukiweza kuwa consistent hucheki cheki, mwezi mmoja unaweza kuona mabadiliko.

Mama mleta mada google "how to control tantrum in/to? ...umri wa mwanao" kwa msaada zaidi. baba google namna ya kudhibiti aggression. Wakati mwingine watoto hatuwapi attention, kwa hiyo wakati mwingine wanafanya vitu vitakavyotufanya tuache vyote tushughulike nao. Sababu ziko nyingi.
 
Uwe na kafimbo kepesi kila akifanya tendo baya unamtandika. Hakika ataacha haraka. Ukizembea akifika over 5 years ataanza kukusumbua sana.
 
Ana mapepo.

Ana mapepo kweli unajua muda mwingine ibilisi anawatumia wale tunaowapenda kutukosesha amani nikiwa standard six mdogo wangu alikuwa na umri wa miaka miwili alikuwa analia sana yaani mpk anasimamia vidole analia mpk sauti inakauka na ukiangalia ni kitu kidogo
siku moja pastor alikuja kumtembelea mama nyumbani babuu akawa anachezea chupa ya soda ukiitoa anaifuata anachezea kitendo cha kufokewa alilia vile vile huku ana mvamia mama mwilini mmh pastor akashtuka yaani alipo muombea haikutokea tena.
 
Pole...
Huyo ni wa kumkanya, ana akili ya kujifunza huyo, unaweza kumchapa kidogo mkononi au kumfinya kidogo.
Pia kumwambia kua kufanya hivi ni tabia mbaya. Na kuna lile jicho ukimuangalia anajua hujapenda.
Kila la heri mkuu
 
nenda kaonane na daktari wa magonjwa ya akili kwa watoto, mwanao inaelekea ana tatizo. serious mkuu maana kwa hasira hizi ukipata mtoto mwingine si utakuta keshamchoma kisu cha tumboni? achana na ushauri wa kienyeji mara mapepo mara nini. sisi waafrika tuliweka mbele sana imani za kishirikina ndio maana hatukundelea. pia achana na habari ya kumpiga mwanao, inampa unyonge na matatizo ya kisaikolojia ambayo yatamsumbua maisha yake yote zaidi sana ukubwani, atakua ni mtu asiyejiamini na mnyonge. jiulize kwanini wazungu hawawapigi watoto wao lakini bado wanakua na kua watu wazuri wenye akili? as a young generation we are supposed to leave the old school of thoughts "corporal punishment" also we are required to think critically and not to be judgemental
 
Pole kwa tatizo,but jaribu kutofautisha kati ya hasira na kiburi,psychologically 1-3 years age ni rahis mtoto kuwa na kiburi zaid kuliko hasira,do something kwenye adhabu kwan ndio muda ambao mwanao anajenga msingi wa tabia,unles otherwise uwe huo ndio uamuz wa maisha yake,but remind u that yeye hajui nn anafanya,kwa ziada tafuta wanasihi wa afya ya ukuaji wa watoto wakusaidie,or pm nikuunishe na baadhi ya watu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Pole, wakwangu ana miaka mitatu kasoro alikuwaga na hasira mno, akikasirika anapigiza kichwa chini bahati alikua akijipigiza sakafuni, nilikua naumia mno, siku moja akiwa mgonjwa akakasirika, nikajua kinochofwata ni kujipigiza sakafuni, namshukuru Mungu nikamwahi nikamdaka, nikawaza angejipigiza ingekuwaje?! Nilimchapa sana na kuanzia ile siku hajarudia teena, hivyo adhabu inasaidia.
Pia nimekua nikimpeleka kwenye ibada za watoto huko anakutana na wenzake wanacheza wanafurahi, imemsaidia sana kupunguza hasira, na anaendelea vizuri
 
hako katoto katakuja kuwa komandoo katavnja matofali kama makomandoo wetu...kakikua...
 
Ndugu wana-Jamvi,

Mwanangu ana umri wa mwaka mmoja na miezi nane lakini anakabiliwa na tatizo la kuwa na hasira hasa pale anapoona amecheleweshewa kupewa kitu mfano kama uji au juice.

Unaweza kumpa juice ikiisha anakitupa kikombe au chupa au anaenda kwenye kabati anatoa kikombe anakipasua basi roho yake inakuwa imetulia. Sasa jambo hili linanipa wasiwasi endapo ataendelea kuwa na hasira za namna hii.

Kama kuna tiba yoyote naombeni msaada.

ungempata housegirl wa uganda ingekuwa poa
 
Mwanangu wa pili alikuwa na hiyo tabia...hatukuchoka kumkanya...sasa hivi ameacha na ni the brightest...

Ilikuwa ni shida maana anarusha popote sasa kikkuute pande alizorushia....
Na inakuwa kama automatic maana saa ingine ukimuangalia anaenda kuchukua kitu arushe anashtuka anaacha...

Sasa hivi ana miaka minne na nusu...
Nilikuwa nimeanza kusahau hii tabia niliiona wapi...imechukua muda kukumbuka kuwa mwanangu alikuwa hivyo akiwa mdogo...

Juzi babake ananambia amekuta ukuta umechorwa...akauliza nani kachora ukuta...kimya...akawaambia watafute fimbo...wako wawili...huyu mdogo eti baada ya muda kamfata chumbani babake anamwambia "I have an idea... I am going to clean it"...kuepuka kisago...na maanake ni yeye ndio kachora

Kuna vitu si vya kupanic si pepo wala nini ni stage kwa baadhi ya watoto ...unatakiwa tu usichoke kumkanya...

Huyu mwanangu toka aanze shule amekuwa anakuwa wa kwanza tu na alianza katikati ya mwaka akiwa mdogo kuliko wote darasani. Anaingi pre-unit sasa...

Ndugu wana-Jamvi,

Mwanangu ana umri wa mwaka mmoja na miezi nane lakini anakabiliwa na tatizo la kuwa na hasira hasa pale anapoona amecheleweshewa kupewa kitu mfano kama uji au juice.

Unaweza kumpa juice ikiisha anakitupa kikombe au chupa au anaenda kwenye kabati anatoa kikombe anakipasua basi roho yake inakuwa imetulia. Sasa jambo hili linanipa wasiwasi endapo ataendelea kuwa na hasira za namna hii.

Kama kuna tiba yoyote naombeni msaada.
 
Ila wakati mwingine nikiwa nachat nao skype (niko mbali) namuona amekunja uso...nikimuuliza vipi? Ananambia I am just angry...lakini kwa kuwa ameacha kurusha vitu na wala sijawai pata kesi shuleni anakosoma ...naona hana tatizo tena...
Na hana maneno mengi kama kaka yake...yuko serious muda mwingi...ila akiongea utajua kuwa ni kichwa...
 
Kupiga mtoto kwa kiasi lakini sikatai...hata mwanangu fimbo ndio zilimyoosha...kila akitupa kitu alikuwa anapata bakora...
Lakini wanangu wakikua fimbo ni big No...nachapa mwisho miaka 7...

Chapaaa_

Mimi nilikuwaga na hasira za namna hiyo, sitashangaa mwanangu wa kiume akiwa nazo. Ila nilitandikwaga aisee...hasira zenyeweee.

Fimbo na Maonyo hutia hekima, Bali mwana "alieachiliwa" (sasa hapo Neno linamaana kubwa) ni mzigo wa mamaye,
Quoted from Mithali (sikumbuki ngapi)
 
......mimi huyu wangu naye ni hasira na ubishi. Mtoto yupo 4 yrs lakini anafanya vitu kama mkubwa.

Alivyokuwa na 2 yrs ukimuudhi au akitaka kitu apate muda huo huo, otherwise anajiangusha.......nikaanza kumpa viadhabu akaacha.

Sasa tokea miaka 3 hadi sasa 4 kaanzisha tabia ya kurusha vitu na kubamiza milango, yaani ukimuudhi lazima atafute kitu cha kuharibu kwa kurusha au kubamiza milango.

.....nimeanza kumstua kwa kumchapa sometimes, basi ukimchapa atakwambia stop hitting me! Namwambia nakuchapa kwa sababu umefanya hivi, ni kosa.

Wiki 2 hizi naona kama ameanza kustop kurusha vitu, ila milango anabamiza na kanasema leave me alone. Hii bado nafanyia kazi.

Usione watu tumekuwa, kumbe wazazi walifanya kazi sana kulea. Kulea mtoto ni another full-time job, unatakiwa ufanye kwa hekima kweli.
 
Ninajaribu kufanya hivyo ila anabaki na kisirani
Tafuta kisu au kiwembe, akivunja kikombe au gilasi mweke chanjo/chale usoni kama ya wamakonde halafu msogezee kioo ajione. Kama atapenda kuona chanjo/chale hizo zinavyoengezeka na zinavyopamba uso wake ataendelea kuvunja, vyenginevyo ataacha kihererehere,kisirani kitayeyuka na hasira zake zitaisha..
 
nenda kaonane na daktari wa magonjwa ya akili kwa watoto, mwanao inaelekea ana tatizo. serious mkuu maana kwa hasira hizi ukipata mtoto mwingine si utakuta keshamchoma kisu cha tumboni? achana na ushauri wa kienyeji mara mapepo mara nini. sisi waafrika tuliweka mbele sana imani za kishirikina ndio maana hatukundelea. pia achana na habari ya kumpiga mwanao, inampa unyonge na matatizo ya kisaikolojia ambayo yatamsumbua maisha yake yote zaidi sana ukubwani, atakua ni mtu asiyejiamini na mnyonge. jiulize kwanini wazungu hawawapigi watoto wao lakini bado wanakua na kua watu wazuri wenye akili? as a young generation we are supposed to leave the old school of thoughts "corporal punishment" also we are required to think critically and not to be judgemental

.....aliokwambia wazungu hawachapi mtoto nani? Shuleni nitakubali, ila si majumbani mwao. Wanaadhibu watoto kwa kiasi, sio huku kwetu basi mtoto atakula mboko hadi apate vidonda.
 
Tafuta kisu au kiwembe, akivunja kikombe au gilasi mweke chanjo/chale usoni kama ya wamakonde halafu msogezee kioo ajione. Kama atapenda kuona chanjo/chale hizo zinavyoengezeka na zinavyopamba uso wake ataendelea kuvunja, vyenginevyo ataacha kihererehere,kisirani kitayeyuka na hasira zake zitaisha..

......sasa huku ni kumuabuse mtoto, seriously! Umkwaruze mtoto na viwembe? Huu ni uonevu.
 
......sasa huku ni kumuabuse mtoto, seriously! Umkwaruze mtoto na viwembe? Huu ni uonevu.
Unataka kusema wamakonde na wanaojitia tatoo wanafanya abuse?
Kama ni wewe katika hiyo avatar, jaribu kuweka chale uone utakavyozidi kuwa mrembo.
 
Back
Top Bottom