Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

huyo mtoto jinsia gani?mpe kaadhabu kanakolingana na yeye pole...
ila mtoto anaelilia msosi safi sana hongera kwa hilo
afu umeadimika kumbe unalea!!!!

Ahsante mamito, yaani kulea kazi kwelikweli maana siku za weekend nakamatika kwelikweli
 
Kwa uelewa wangu mtoto anaweza kuwa na hasira sababu kuu zikiwa mbili.
1-wakati mama akiwa mjamzito hamkua na mawasiliano mazuri hiyo ikamfanya mwanamke kuwa na hasira muda mwingi na stress zisizoisha,hii humuathiri mtoto moja kwa moja,tiba hapa ni kuwa karibu na mtoto na kumwonyesha upendo ili kupunguza msongo aliozaliwa nao.
2-Malezi limekua tatizo kubwa,unamlea mtoto kama yai,lazima ujue mtoto anaanza kuwa na utambuzi akiwa na miezi 4 mpaka 5 pale anapoanza hata kuchagua watu wa kumbeba,ukichunguza kipindi hicho akifanya kitu kibaya ukimfoka atalia au ataogopa na hapo ndo tunapofanya makosa,mtoto anakosea kitu hata kumwonyesha kwamba hakufanya vizuri unamwacha ukijidai bado mdogo,tabia hukuzwa,nimekuwa na jirani yangu ana kitoto kina mwaka na nusu kina tabia mbaya sana,kinampiga makofi mama yake,kina kiburi yani tabu tupu,ukimwambia mbona mwanao hivyo anasema bado mdogo ataacha,mpaka majirani hawataki acheze na watoto wenzake,akikosea ukamfoka au kumfinya umenunua kesi kwa mama yake,mnakosana kabisaa,me binafsi nina kijana ana mwaka na nusu ila anajua kwamba hiki baba hataki na hiki nitafinywa na mama yuko well kabisa,ila kwa kosa ambalo najua umri wake bado huwa natafuta namna ya kumsaidia,sio unaona kitoto kinavuruga nyumba kinagombana na wenzake na matusi juu bado unasema akikua ataacha pole.

Thanks mkuu
 
Huyo atakuja kuwa mwanajeshi ha ha haaaa...Anza kupanga vitu vyako vya thamani vinavyovunjika kulingana na height yake just in case akiwa na hasira ashindwe kuvifikia, na ikiwezekana mtengenezee ngao ili kuwanusuru wengine pindi awapo na hasira!
 
nakushauri mpeleke kwenye maombi ya kiroho huko ataponeka
(hizi ni tiba za kiMungu)

kingine nakushauri mwite mwanasaikolojia au mpelekea kwa mwanasaikolojia atamtibu
(hizi ni tiba za kibinadamu)

kingine jichunguzeni nyie wazazi uenda mna kasoro kwa mtoto wenu juu ya malezi
Ndugu wana-Jamvi,

Mwanangu ana umri wa mwaka mmoja na miezi nane lakini anakabiliwa na tatizo la kuwa na hasira hasa pale anapoona amecheleweshewa kupewa kitu mfano kama uji au juice.

Unaweza kumpa juice ikiisha anakitupa kikombe au chupa au anaenda kwenye kabati anatoa kikombe anakipasua basi roho yake inakuwa imetulia. Sasa jambo hili linanipa wasiwasi endapo ataendelea kuwa na hasira za namna hii.

Kama kuna tiba yoyote naombeni msaada.
 
nakushauri mpeleke kwenye maombi ya kiroho huko ataponeka
(hizi ni tiba za kiMungu)

kingine nakushauri mwite mwanasaikolojia au mpelekea kwa mwanasaikolojia atamtibu
(hizi ni tiba za kibinadamu)

kingine jichunguzeni nyie wazazi uenda mna kasoro kwa mtoto wenu juu ya malezi

Ahsante kwa ushauri mzuri naamini mwanangu atapata tiba itakayomsaidia kwenye maisha yake
 
afadhali wako,kuna dogo hata kutembea shida akikasirika anajirusha au kujipigiza chini
 
nenda kwa doctor hospital, hao ni bacteria hushambulia sana kichwani, na hata mtu mzima unaweza kuwa na hasira za ajabu ajabu utadhani mwanamke mjamzito, mpeleke akapigwe antibiotic, ni ugonjwa huo mkuu, mie ulishawahi nikumba, nilienda nikapima kipimo kinaitwa Full blood picture, nikachezea sindano mpaka leo, niko ok, manake kitu kidogo tu mie nachukulia ugomvi tena valangati la juu najiona mbabe mie
 
nitonye na mie nakabilia na hili ,yaani ukimcheleweshea nyonyo atakukwaluza na kuvuta nguo na vituko vya ajabu labda nimpeleke kwenye maombi
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri baada ya kujua kuongea na kusema anachotaka ataacha..... pia akifanya hivo jaribu kumfinya kdg.
...yes hapo kwenye kumfinya kidogo umepatia kabisaaaa!mambo ya kuwadekeza watoto bila kuwaonya kwa fimbo au kucha ni mabaya sanaaaa
 
yaani hebu tusaidieni maana wa kwangu ten months ila daah huo mziki wake hatarii
akililia kitu usipompa atalia na kukufinya juu
mbishi na ana hasira hatari
 
Angalia karithi kwa nani suala zima la genetics kuzingatiwa kuna ukorofi unaambiwa ah kama babu yake.
 
Huyo mtoto anaweza akawa diabetic. It is very important you seek medical check up.
 
Chapaaa_

Mimi nilikuwaga na hasira za namna hiyo, sitashangaa mwanangu wa kiume akiwa nazo. Ila nilitandikwaga aisee...hasira zenyeweee.

Fimbo na Maonyo hutia hekima, Bali mwana "alieachiliwa" (sasa hapo Neno linamaana kubwa) ni mzigo wa mamaye,
Quoted from Mithali (sikumbuki ngapi)
 
Back
Top Bottom