Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

Msaada: Mtoto wangu ana hasira sana

nitonye

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2011
Posts
7,349
Reaction score
3,904
Ndugu wana-Jamvi,

Mwanangu ana umri wa mwaka mmoja na miezi nane lakini anakabiliwa na tatizo la kuwa na hasira hasa pale anapoona amecheleweshewa kupewa kitu mfano kama uji au juice.

Unaweza kumpa juice ikiisha anakitupa kikombe au chupa au anaenda kwenye kabati anatoa kikombe anakipasua basi roho yake inakuwa imetulia. Sasa jambo hili linanipa wasiwasi endapo ataendelea kuwa na hasira za namna hii.

Kama kuna tiba yoyote naombeni msaada.
 
Swala dogo hilo. Mpe adhabu kulingana umri wake kila anapokua ameharibu kitu kwa hasira zake na isiwe Mara kwa mara inatakiwa iwe Mara chache uwezavyo ataacha.
 
nitonye

Kama baba yake mtoto ni mkurya kazi ipo.Ni kopi ya mura hiyo.

Hasira ni kitu cha kawaida.Ila kama anaanza kuvunja vitu (destructive anger) hapo inabidi uanze kumdhibiti mapema kwa kumwonyesha umechukia na kumvuta aisifanye kile atakach😵f course atalia sana ukimvuta na kumzuia anachotaka kufanya lakini baadaye akivutwa vutwa mara nyingi ataacha.usimpe nafasi ya kutekeleza azima yake akiendelea hivyo atakuja haribika mno mbeleni.

Ila akikua kidogo ni vizuri kuanza kumchapa kidogo kidogo anapokosea ili ajue kila kosa lina adhabu.Ataacha hivyo vi hasira koko vyake na akikua ataogopa kulipuka hasira mno akijua kuwa atashughulikiwa kama mzazi ulivyokuwa ukimshughulia.Usipomshughulikia atakua akijiona yeye mfalme anayeweza fanya chochote na asifanywe chochote.Ndio maana adhabu muhimu hasa kwa mtoto anapokuwa mdogo anapokosea.
 
Last edited by a moderator:
nitonye

Udongo uwahi ungali maji/mbichi. Huyu mtoto unatakiwa umdhibiti kabla hivyo anavyovifanya havijawa tabia, mazoea au kawaida.

Siku akifanya huo ujinga hebu chukua kafimbo mtandike na umwambie hiyo tabia ni mbaya na asirudie tena. Pia mwambie madhara ya kuharibu vitu nini ili aelewe ni kwa nini umemwadhibu. Pia siku kakikililia uji mweleze avumilie wanamwandalia atulie. Baadae katakuja kuwa kasumbufu kwani hakana subira, inaweza kupelekea kwenye udokozi kwani hawezi kusubiri maana anataka muda huo huo apate anachotaka. Hili nalo si dalili njema kwa mwanao idhibiti mapema.

Huyu mtoto dhibiti mapema hizo tabia zote mbili anazoonyesha sio njema kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Udongo uwahi ungali maji/mbichi. Huyu mtoto unatakiwa umdhibiti kabla hivyo anavyovifanya havijawa tabia, mazoea au kawaida.

Siku akifanya huo ujinga hebu chukua kafimbo mtandike na umwambie hiyo tabia ni mbaya na asirudie tena. Pia mwambie madhara ya kuharibu vitu nini ili aelewe ni kwa nini umemwadhibu. Pia siku kakikililia uji mweleze avumilie wanamwandalia atulie. Baadae katakuja kuwa kasumbufu kwani hakana subira, inaweza kupelekea kwenye udokozi kwani hawezi kusubiri maana anataka muda huo huo apate anachotaka. Hili nalo si dalili njema kwa mwanao idhibiti mapema.

Huyu mtoto dhibiti mapema hizo tabia zote mbili anazoonyesha sio njema kabisa.
Thanks mkuu ubarikiwe
 
Kama baba yake mtoto ni mkurya kazi ipo.Ni kopi ya mura hiyo.

Hasira ni kitu cha kawaida.Ila kama anaanza kuvunja vitu (destructive anger) hapo inabidi uanze kumdhibiti mapema kwa kumwonyesha umechukia na kumvuta aisifanye kile atakach😵f course atalia sana ukimvuta na kumzuia anachotaka kufanya lakini baadaye akivutwa vutwa mara nyingi ataacha.usimpe nafasi ya kutekeleza azima yake akiendelea hivyo atakuja haribika mno mbeleni.

Ila akikua kidogo ni vizuri kuanza kumchapa kidogo kidogo anapokosea ili ajue kila kosa lina adhabu.Ataacha hivyo vi hasira koko vyake na akikua ataogopa kulipuka hasira mno akijua kuwa atashughulikiwa kama mzazi ulivyokuwa ukimshughulia.Usipomshughulikia atakua akijiona yeye mfalme anayeweza fanya chochote na asifanywe chochote.Ndio maana adhabu muhimu hasa kwa mtoto anapokuwa mdogo anapokosea.

Nashukuru sana mkuu naamini nitajitahidi kufanya hivyo
 
Tabia ni moja kati ya traits ambazo mtoto hurithishwa kutoka kwa wazazi, hivyo hasira kama tabia nayo mtoto hurithi...

Pia inaaminika kuwa watoto wa kiume huwa na tabia ya kufanya vurugu za hapa na pale wanapokuwa wakikua, kuvunjavunja vitu ni moja ya vurugu hizo...

Je mwanao ni jinsia gani?

Kama ni wa kiume basi kwa sasa ni ngumu kujua kuwa hicho alichonacho ni tabia ya hasira auni sehemu tu ya ukuaji?
 
Tabia ni moja kati ya traits ambazo mtoto hurithishwa kutoka kwa wazazi, hivyo hasira kama tabia nayo mtoto hurithi...

Pia inaaminika kuwa watoto wa kiume huwa na tabia ya kufanya vurugu za hapa na pale wanapokuwa wakikua, kuvunjavunja vitu ni moja ya vurugu hizo...

Je mwanao ni jinsia gani?

Kama ni wa kiume basi kwa sasa ni ngumu kujua kuwa hicho alichonacho ni tabia ya hasira auni sehemu tu ya ukuaji?

Ni wakiume mkuu watu8
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hilo suala limekaa kisaikolojia zaidi, binafsi nakushauri kama utapata muda wa ziada mpeleke kwa wataalamu wa saikolojia watakupa ufumbuzi wa maana.
 
Ndugu wana-Jamvi,

Mwanangu ana umri wa mwaka mmoja na miezi nane lakini anakabiliwa na tatizo la kuwa na hasira hasa pale anapoona amecheleweshewa kupewa kitu mfano kama uji au juice.

Unaweza kumpa juice ikiisha anakitupa kikombe au chupa au anaenda kwenye kabati anatoa kikombe anakipasua basi roho yake inakuwa imetulia. Sasa jambo hili linanipa wasiwasi endapo ataendelea kuwa na hasira za namna hii.

Kama kuna tiba yoyote naombeni msaada.

je wakati wa ujauzito wako, baba wa mtoto alikuwa anaku treat vp, au wewe mwenyewe ulimuonesha upendo tangu akiwa tumboni au ulikuwa mkali mkali?
 
Ana mapepo.

Mi nadhani si kila kitu kinaweza kuhusishwa na imani za kishirikina. Hiyo inaweza kuwa tabia tu na ikidhibitiwa mapema inaweza kuisha tu unless kama kuna vitu vingine havijasemwa.
 
Back
Top Bottom