Habarini wanajamvi!!
Katika harakati za hapa na pale nilikwaruzana na mpenzi wangu, ofcourse nilimpenda nae alinikubali japo sikumwamini sana na ishu ya kuzinguana ni kwa sababu alimtukana mtu ninaemtegemea katika mambo kadha wa kadha.
Nilivyojaribu kumwambia kwamba sijapenda lile suala akaanza kunikashfu actually ikaniuma so tukaacha kuwasiliana na kila mtu akawa na mishe zake. After one year nimekutana nae tena, she is pregnant na kaniomba tuzungumze.
Nilivopata mda tukakaa, akaanza kulia oooooh umefanya maisha yangu yawe magumu, sikutaka kuzaa na mwanamme mwingine zaid yako na bado nakupenda sana na lazima nije nizae na wewe.
Wakuu nifanyajeee?