Msaada: Mpenzi mpya kazira nifanyaje?

Msaada: Mpenzi mpya kazira nifanyaje?

Tanya

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2013
Posts
340
Reaction score
159
Habari wapendwa.

Hapa Niko kwenye kizingumkuti sielewi nifanyaje. Kuna mwanaume amekuwa akinitafuta kwa muda mrefu baadaye nikamkubalia lakini akawa anaishi Dar na Mimi Niko Mbeya, HV karibu ni kama wiki hivi akaniambia unakuja Mbeya ili tufanye makubaliano vizuri maana tokea namkubalia hatujakutana tupange mikakati ya maisha yetu ya mapenzi.

Jana Ijumaa kakwea pipa kutoka Dar kuja Mbeya kwa dhumuni hilo kwamba atakaa ijumaa,jumamosi na kugeuza Dar siku ya Jumapili.
Ukiwa njiani nilimuomba nije kumpokea nikiwa na rafiki yangu wa kike akakubali.

Alipofika muda wa SAA kumi na mbili kasoro tulimpokea vizuri na kumpeleka kwenye hotel ambayo nilimfanyia booking na alipopumzika km dk kumi tukatoka nae kwenda sehemu ya kula ambayo iko mbali kidogo na hapo alipofikia. Tulikaa hapo hadi SAA tatu usiku tukiwa na rafiki yangu na hakuna maongezi yoyote ya Mimi na yeye yaliyoendelea pale.

Baada ya hapo tayari usiku tulimuaga kuondoka ili na yeye akapumzike alipofikia akaanza kukataa akitaka nikakutane nae kimwili, nikakataa kwa kuwa nyumbani si kuwa nimeaga na bado sio makubaliano yetu kufika na kuanzia Kudo kabla hatijaongea chochote kilichomleta.

Alikuwa serious kunitaka nikalale nae ili hali sina wazo wala kujua kuwa kaka kwa hilo so si kujiandaa kuaga nyumbani kuwa sintarudi hivyo nilimsihi asibiri kesho yake ndo tutajua vizuri kama nitalala nae au la.

Alikubali tukaondoka na rafiki yangu, na kwa kuwa ilikuwa usiku nilimsihi rafiki yangu anisindikize nyumbani ili wazazi wasiwe na maswali mengi juu ya kuchelewa kurudi.

Cha kushangaza baada tu ya kuachana jamaa alibadilisha mawazo kuwa anaondoka kesho yake kabla hata hatujapngea chochote kilichomleta Mbeya kisa nimemnyima mchezo.

sasa naomba ushauri; Je huyu ni mwanaume nzuri wa future kweli kama kasusa kisa kukosa mchezo ambao hata haukuwepo kwenye makubaliano yetu?
Je ,ananipenda kwa that?

Nini haswa kilichomkwaza hadi akasusa akaamua kuondoka kabla azma yake haijatimia?
Je nimfuate Dar tukayajenge huko????
ASANTENI IN ADVANCE KWA USHAURI
 
First suala sex na mahusiano ni kila mtu na mtazamo wake
wapo ambao sex ni sehemu muhimu tu ya kujuana na kuimarisha uhusiano
wapo wengine sex lazima isubiri kwanza wafahamiane vizuri

Ulipaswa kumwambia kabla hata hajasafiri kuja kuwa akija hamta sex
ili ajue na aamue kuja au asije...

La pili ulikosea sana kwenda na rafiki yako ukakaa nae masaa matatu kiasi wewe na mtu wako mkashindwa
kuongea yenu na kuzoeana na kufahamiana na kuelewana

yawezekana jamaa alijikuta tu 'ameboreka' na kila kitu
 
First suala sex na mahusiano ni kila mtu na mtazamo wake
wapo ambao sex ni sehemu muhimu tu ya kujuana na kuimarisha uhusiano
wapo wengine sex lazima isubiri kwanza wafahamiane vizuri

Ulipaswa kumwambia kabla hata hajasafiri kuja kuwa akija hamta sex
ili ajue na aamue kuja au asije...

La pili ulikosea sana kwenda na rafiki yako ukakaa nae masaa matatu kiasi wewe na mtu wako mkashindwa
kuongea yenu na kuzoeana na kufahamiana na kuelewana

yawezekana jamaa alijikuta tu 'ameboreka' na kila kitu
Ni kweli I regret
 
Khaaaa!
Kiukweli ni mazito kweli haya.
Yote kwa yote hakupaswa kuwa na maamuz ya ghafla kiasi hicho, Subira ilipaswa ichukuwe nafasi kwa pande zote mbili.

Japo hujaeleza kama keshaondoka ama laa?
Ila kama kaondoka, basi mpotee tu, maana anaonekana huyo ni wa kuchovya tu.
Maana wanaume wa Dar ndivyo walivyo hivyo.
Ha ha ha ha ha hahaha.
 
First suala sex na mahusiano ni kila mtu na mtazamo wake
wapo ambao sex ni sehemu muhimu tu ya kujuana na kuimarisha uhusiano
wapo wengine sex lazima isubiri kwanza wafahamiane vizuri

Ulipaswa kumwambia kabla hata hajasafiri kuja kuwa akija hamta sex
ili ajue na aamue kuja au asije...

La pili ulikosea sana kwenda na rafiki yako ukakaa nae masaa matatu kiasi wewe na mtu wako mkashindwa
kuongea yenu na kuzoeana na kufahamiana na kuelewana

yawezekana jamaa alijikuta tu 'ameboreka' na kila kitu
Na hili la pili ndio tatizo hasa
 
Icho kitu ndio uwa kinaniboa kwa wanawake wengi unamwambia njoo tukutane au njoo nikuone,then unamsikia ntakuja na rafiki yangu,hakuna kitu nachochukia kama hiki.

Kibaya zaidi anaweza kuja na rafiki kimbelembele mjuaji..
rafiki anaemshikia akili

yeye kakupenda but rafiki yake akikuponda tu baasi...
 
Duuuhhhh kazi kweli kweli.

Lengo la kuonana ni kuongea kuhusu maisha yenu. Unaenda na rafiki, tafsiri lahisi ni kuwa wewe si mtu mwenye uwezo wa kujisimamia. Kwa maneno mengine una akili ya kushikiwa jambo ambalo limekupunguzia "credit".

Wagombanao ndio wapatanao, jitahidini kumuomba radhi kwa yote ili mpange ya mbeleni.
 
Kibaya zaidi anaweza kuja na rafiki kimbelembele mjuaji..
rafiki anaemshikia akili

yeye kakupenda but rafiki yake akikuponda tu baasi...
Ndio hivyo rafiki mwenyewe unakuta kichwani empty,na kiukweli hapo mchawi hata sio sex bali ni rafiki yake maana angekuwa wameshinda wote kwa huo mda hata kama angekataa jamaa angemuelewa coz ameshamsoma kwa hayo masaa kadhaa.
 
aisee unabahati kweli kweli, mtu kapanda na pipa kabisa halafu kalala pekeyake😡😡😡
 
Ulichokosea ni kwenda na rafiki yako. Mtu amekuja kukutembelea kisha na ww unajifanya kwenda na rafiki.
Nahisi pia ht umri wako huenda ni mdogo ndio maana bado hujajua madhara ya marafiki ww. Mi ushauri wangu ni huo tu, mengine watakushauri wadau.
 
Khaaaa!
Kiukweli ni mazito kweli haya.
Yote kwa yote hakupaswa kuwa na maamuz ya ghafla kiasi hicho, Subira ilipaswa ichukuwe nafasi kwa pande zote mbili.

Japo hujaeleza kama keshaondoka ama laa?
Ila kama kaondoka, basi mpotee tu, maana anaonekana huyo ni wa kuchovya tu.
Maana wanaume wa Dar ndivyo walivyo hivyo.
Ha ha ha ha ha hahaha.
Kashaondoka
 
Back
Top Bottom