msaada meatu na lindi wapi kwa kwenda

msaada meatu na lindi wapi kwa kwenda

Negrodemus

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2010
Posts
2,318
Reaction score
688
nina mdogo wangu kachaguliwa sehemu mbili na nafasi ni hiyo hiyo moja kachaguliwa lindi kama afisa maendeleo ya jamii daraja la ii na pia meatu kama afisa maendeleo ya jamii daraja la pili ingawa kwenye interview alifanya katika nafasi mbili ya afisa maendeleo ya jamii na afisa maendeleo ya vijana na kote alifanya vizuri. majibu kutoka naona nafasi zote ni afisa maendeleo ya jamii, lindi anatakiwa kuripoti kwa katibu tawala wa mkoa wa lindi na meatu kwa mkurigenzi wa halmashauri ya wilaya ya meatu. kaniomba ushauri aende wapi kati ya hizo sehemu mbili. naomba wenye uzoefu na haya maeneo mpate kunisaidia nimuelekeze my mdogo.
 
Hahaaaaa I know the person,his first name starts with S nad the last one ends with B.i would advice him to report/work in Lindi.
 
Lindi aende
Japo Meatu napafaham sana na nimeenda sana ila Lindi at least kuna mengi na karibu na Dar mambo yatakuwa super
Ila akienda Meatu ajiandae kupambana na vumbi aise maana kule lami bado ni ndoto mbali na makao makuu ya mkoa ambapo ni Bariadi na hata shinyanga ila uwezekano wa kupata mengi kutoka mwanza ambapo japo ni mbali ila panainuka sana uwezekano wa yeye kwenda mwanza weekend na kurudi upo pia
 
Lindi mwambie. Ndiko maendeleo yamechelewa, akashirikiane na wenzake kuyainua
 
Aende lindi, Meatu hakuna issue nina rafiki yangu yupo huko. Community development officers wapo 5 ofisini wamebanana zaidi watamtupa kijijini?
 
aende lindi,ila isije ikawa lindi kumbe akifika lindi anapelekwa ndani zaidi,kama ni hivyo bora meatu akalime na pamba
 
Aende lindi, Meatu hakuna issue nina rafiki yangu yupo huko. Community development officers wapo 5 ofisini wamebanana zaidi watamtupa kijijini?

Wewe unataka akae mjini afanye nini? Hivi unategemea unaenda kuanza kazi wakuache mjini uwabanie nafasi zao? Thubutu!! Hata huko Lindi watamtupa vijijini tu!!!

Jamii inayohitaji maendeleo iko vijijini na ndo kazi aliyosomea hiyo, acha kumtisha bwana kwani akikaa kijijini hawezi kupga kazi? Mkuu mwambie aje Meatu tubanane mwanawane! Hii wilaya inaitwa MEA-TU (Maana yake ukiwa hapa wewe una mea-tu hakuna kunyauka). Maafisa wengi wakiisikia huwa hawaitaki lakini wakishafika huwa hawataki tena kuhama/kuondoka.
 
zamani 2kifika njia panda kama hapo huwa 2na weka mate kiganjani na kuyachapa yakielekea kusini aende lindi yakielekea northern rock aje meatu.
 
nina mdogo wangu kachaguliwa sehemu mbili na nafasi ni hiyo hiyo moja kachaguliwa lindi kama afisa maendeleo ya jamii daraja la ii na pia meatu kama afisa maendeleo ya jamii daraja la pili ingawa kwenye interview alifanya katika nafasi mbili ya afisa maendeleo ya jamii na afisa maendeleo ya vijana na kote alifanya vizuri. majibu kutoka naona nafasi zote ni afisa maendeleo ya jamii, lindi anatakiwa kuripoti kwa katibu tawala wa mkoa wa lindi na meatu kwa mkurigenzi wa halmashauri ya wilaya ya meatu. kaniomba ushauri aende wapi kati ya hizo sehemu mbili. naomba wenye uzoefu na haya maeneo mpate kunisaidia nimuelekeze my mdogo.
kwa experienc ya mkoa wa lind na maafisa maendeleo lazima atapelekwa kati ya wilaya 6 za lind,wakimpanga kilwa ni kuzur sana,lind mjin c kubaya,lind vijijin nako c kubaya pako mjin,ruangwa na nachingwea nako ndio panaanza kuendelea,liwale kubaya,mwambie aje lind,kwanza karibu na dar kama mfuko utamruhusu kila wk end ni dar,ni masaa sita tu
 
Aende Lindi, pamoja na hayo naomba kuuliza inakuaje mtu mmoja anachanguliwa nafasi moja sehemu tofauti? au ataweza kwenda sehemu zote mbili?
 
Wewe unataka akae mjini afanye nini? Hivi unategemea unaenda kuanza kazi wakuache mjini uwabanie nafasi zao? Thubutu!! Hata huko Lindi watamtupa vijijini tu!!!

Jamii inayohitaji maendeleo iko vijijini na ndo kazi aliyosomea hiyo, acha kumtisha bwana kwani akikaa kijijini hawezi kupga kazi? Mkuu mwambie aje Meatu tubanane mwanawane! Hii wilaya inaitwa MEA-TU (Maana yake ukiwa hapa wewe una mea-tu hakuna kunyauka). Maafisa wengi wakiisikia huwa hawaitaki lakini wakishafika huwa hawataki tena kuhama/kuondoka.

kaka fafanua maafisa wa vyeo gani labda wakurugenzi ndiyo huwa hawataki kuhama, mimi kwa ushauri wangu aende Lindi maana Meatu watampeleka Bukundi atapigwa vumbi mpaka basi Kikwete mwenyewe anakujua anakwambia ukiwa unaingia Meatu utaona ukungu kwa mbali utafikiri mvua inataka kunyesha kumbe vumbi jeupe.
 
Aende Lindi, pamoja na hayo naomba kuuliza inakuaje mtu mmoja anachanguliwa nafasi moja sehemu tofauti? au ataweza kwenda sehemu zote mbili?

mungu wake tu mkubwa na hakuna kubebwa ni vile tu amekaza
 
Back
Top Bottom