Msaada: Mdomo Wa Simu Umekatika

Msaada: Mdomo Wa Simu Umekatika

JAYJAY

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2008
Posts
9,025
Reaction score
9,598
wadau wa JF simu yangu ya tecno imekatika ule mdomo wake ambao charger au usb cable huchomekwa. Dogo alilazimisha kuchaji kwa kutumia chaja ambayo sio sahihi.

Kwa sasa kuchaji simu ni mpaka nitoe battery na kuichaji kwa kobe.

Je, tatizo linarekebishika?
 
kama kamechomoka tu ndio linatibika around 10,000 nilirekebisha yangu.
 
kama kamechomoka tu ndio linatibika around 10,000 nilirekebisha yangu.

baada ya dogo kulazimisha aina tofauti ya charger kale kaulimi kakawa kamepinda katika kukirudisha sawa ndio kikakatika.
 
baada ya dogo kulazimisha aina tofauti ya charger kale kaulimi kakawa kamepinda katika kukirudisha sawa ndio kikakatika.

ndio kitatolewa chote hiko ki usb utaekewa chengine. ni kazi ya dk 5 tu.
 
Back
Top Bottom